Mithali 17 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 17:1-28

117:1 Mit 15:16, 17; 16:8Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu

kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.

217:2 Mit 10:5; 19:26Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye,

naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.

317:3 Mit 27:21; Yer 17:10; 1Pet 1:7; Za 26:2Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,

bali Bwana huujaribu moyo.

4Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya;

mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.

517:5 Mit 14:31; Ay 31:39; Eze 25:3; Oba 1:12Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake;

yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.

617:6 Za 125:5; Mit 13:22Wana wa wana ni taji la wazee,

nao wazazi ni fahari ya watoto wao.

717:7 Mit 16:10Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu:

je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!

817:8 Mwa 39:21; Dan 6:3Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;

kokote kigeukiapo, hufanikiwa.

917:9 Mit 10:12; 16:28Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo,

bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.

10Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua

kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.

11Mtu mbaya hupenda kuasi tu;

mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.

1217:12 1Sam 25:25Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.

1317:13 Yer 18:20; 1Sam 19:4; Rum 12:17; Za 109:4-5Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema,

kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.

1417:14 Mit 20:3; Mt 5:25-26; Mdo 6:1Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji;

kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.

1517:15 Za 94:21; Kut 23:6-7; Mit 18:5; Mao 3:34-36; Isa 5:23Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki,

naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki:

Bwana huwachukia sana wote wawili.

1617:16 Mit 23:23Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu,

wakati yeye hana haja ya kupata hekima?

1717:17 2Sam 15:21; Mit 27:10Rafiki hupenda wakati wote

naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.

1817:18 Mit 6:1-5; 11:5Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani,

naye huweka dhamana kwa jirani yake.

19Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi;

naye ainuaye sana lango lake17:19 Kuinua lango maana yake ni kusema kwa majivuno. hutafuta uharibifu.

20Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa;

naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.

2117:21 Mit 10:1Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni;

hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.

2217:22 Kut 12:46; Za 22:15Moyo wenye furaha ni dawa nzuri,

bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.

2317:23 Kut 18:21; 1Sam 8:3Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri

ili kupotosha njia ya haki.

2417:24 Ay 31:1; Mhu 2:14Mtu wa ufahamu huitazama hekima,

lakini macho ya mpumbavu huhangaika

hadi kwenye miisho ya dunia.

2517:25 Mit 10:1Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake

na uchungu kwa yeye aliyemzaa.

2617:26 Za 94:21; Mit 18:5Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia,

au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.

2717:27 Ay 6:24; Mit 14:29Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia,

naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.

2817:28 Ay 2:13; Mit 10:19Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza,

na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

Hoffnung für Alle

Sprüche 17:1-28

Weisheit lässt sich nicht erkaufen

1Lieber in Ruhe und Frieden ein trockenes Stück Brot essen als ein Festmahl mit Zank und Streit!

2Ein fähiger Diener tritt an die Stelle eines nichtsnutzigen Sohnes, ja, er darf sich zusammen mit den anderen Söhnen das Erbe teilen.

3Gold und Silber prüft man durch Schmelzen, aber was im Herzen des Menschen vorgeht, das prüft der Herr.

4Ein Übeltäter hört gern zu, wenn Böses geredet wird, und einem Lügner gefallen betrügerische Worte, die andere ins Unglück stürzen.

5Wer den Armen verspottet, verhöhnt dessen Schöpfer. Wer sich am Unglück anderer freut, bekommt seine Strafe.

6Alte Menschen sind stolz auf ihre Enkelkinder, und Kinder sind stolz auf ihre Eltern.

7Zu einem Dummkopf passen keine vernünftigen Worte, wie viel weniger passt Lüge zu einem geachteten Menschen!

8Manche glauben, Bestechung sei ein Zaubermittel, das ihnen überall Erfolg verspricht.

9Wer über die Verfehlungen anderer hinwegsieht, gewinnt ihre Liebe; wer alte Fehler immer wieder ausgräbt, zerstört jede Freundschaft.

10Ein vernünftiger Mensch lernt durch einen Tadel mehr als ein Dummkopf durch hundert Schläge!

11Ein Unruhestifter sucht nur den Aufstand, darum wird ihn eine grausame Strafe treffen17,11 Wörtlich: ein grausamer Bote wird gegen ihn gesandt..

12Lieber einer Bärin begegnen, der man die Jungen geraubt hat, als einem Dummen, der nur Unsinn im Kopf hat!

13Wer Gutes mit Bösem vergilt, in dessen Familie ist das Unglück ein ständiger Gast.

14Ein angefangener Rechtsstreit ist so schwer aufzuhalten wie Wasserfluten, wenn der Damm einmal gebrochen ist – darum lass es gar nicht erst so weit kommen!

15Der Herr verabscheut es, wenn der Schuldige freigesprochen und der Unschuldige verurteilt wird.

16Ein Dummkopf kann sich Weisheit nicht erkaufen, sie würde ihm auch gar nichts nützen – er hat ja doch keinen Verstand!

17Ein guter Freund steht immer zu dir, und ein Bruder ist in Zeiten der Not für dich da.

18Wer sich mit Handschlag für die Schulden eines anderen verbürgt, hat den Verstand verloren!

19Der Streitsüchtige liebt die Bosheit; und wer zu hoch hinauswill, wird tief fallen17,19 Wörtlich: und wer seine Tür zu hoch baut, sucht den Einsturz..

20Ein verdorbener Mensch hat nichts Gutes zu erwarten; und wer Lügen verbreitet, stürzt sich ins Unglück.

21Wer einen nichtsnutzigen Sohn hat, kennt nur Sorge und Leid.

22Ein fröhliches Herz macht den Körper gesund; aber ein trauriges Gemüt macht kraftlos und krank.

23Ein gottloser Richter nimmt heimlich Bestechungsgelder an und verdreht das Recht.

24Ein vernünftiger Mensch bemüht sich um Weisheit, aber ein dummer hat nur andere Dinge im Kopf17,24 Wörtlich: aber die Augen des Dummkopfs sind am Ende der Erde..

25Ein leichtsinniger Sohn bereitet seinen Eltern viel Ärger und Enttäuschung.

26Es ist schlimm genug, wenn ein Unschuldiger mit einer Geldstrafe belegt wird; aber es verstößt gegen jedes Recht, wenn ein anständiger Mann eine Prügelstrafe bekommt!

27Ein weiser Mensch ist sparsam mit seinen Worten, denn wer sich selbst beherrschen kann, ist vernünftig.

28Sogar einen Dummkopf könnte man für klug halten – wenn er sich nicht durch seine eigenen Worte verraten würde!