Mithali 17 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 17:1-28

117:1 Mit 15:16, 17; 16:8Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu

kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.

217:2 Mit 10:5; 19:26Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye,

naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.

317:3 Mit 27:21; Yer 17:10; 1Pet 1:7; Za 26:2Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,

bali Bwana huujaribu moyo.

4Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya;

mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.

517:5 Mit 14:31; Ay 31:39; Eze 25:3; Oba 1:12Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake;

yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.

617:6 Za 125:5; Mit 13:22Wana wa wana ni taji la wazee,

nao wazazi ni fahari ya watoto wao.

717:7 Mit 16:10Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu:

je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!

817:8 Mwa 39:21; Dan 6:3Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;

kokote kigeukiapo, hufanikiwa.

917:9 Mit 10:12; 16:28Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo,

bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.

10Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua

kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.

11Mtu mbaya hupenda kuasi tu;

mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.

1217:12 1Sam 25:25Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.

1317:13 Yer 18:20; 1Sam 19:4; Rum 12:17; Za 109:4-5Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema,

kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.

1417:14 Mit 20:3; Mt 5:25-26; Mdo 6:1Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji;

kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.

1517:15 Za 94:21; Kut 23:6-7; Mit 18:5; Mao 3:34-36; Isa 5:23Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki,

naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki:

Bwana huwachukia sana wote wawili.

1617:16 Mit 23:23Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu,

wakati yeye hana haja ya kupata hekima?

1717:17 2Sam 15:21; Mit 27:10Rafiki hupenda wakati wote

naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.

1817:18 Mit 6:1-5; 11:5Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani,

naye huweka dhamana kwa jirani yake.

19Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi;

naye ainuaye sana lango lake17:19 Kuinua lango maana yake ni kusema kwa majivuno. hutafuta uharibifu.

20Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa;

naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.

2117:21 Mit 10:1Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni;

hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.

2217:22 Kut 12:46; Za 22:15Moyo wenye furaha ni dawa nzuri,

bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.

2317:23 Kut 18:21; 1Sam 8:3Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri

ili kupotosha njia ya haki.

2417:24 Ay 31:1; Mhu 2:14Mtu wa ufahamu huitazama hekima,

lakini macho ya mpumbavu huhangaika

hadi kwenye miisho ya dunia.

2517:25 Mit 10:1Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake

na uchungu kwa yeye aliyemzaa.

2617:26 Za 94:21; Mit 18:5Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia,

au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.

2717:27 Ay 6:24; Mit 14:29Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia,

naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.

2817:28 Ay 2:13; Mit 10:19Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza,

na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Proverbios 17:1-28

1Más vale comer pan duro donde hay concordia

que hacer banquete17:1 banquete. Lit. sacrificios. donde hay discordia.

2El siervo sabio gobernará al hijo sinvergüenza,

y compartirá la herencia con los otros hermanos.

3En el crisol se prueba la plata

y en el horno se prueba el oro,

pero al corazón lo prueba el Señor.

4El malvado hace caso a los labios impíos,

y el mentiroso presta oído a la lengua maliciosa.

5El que se burla del pobre ofende a su creador;

el que se alegra de verlo en la ruina no quedará sin castigo.

6La corona del anciano son sus nietos;

el orgullo de los hijos son sus padres.

7No va bien con los necios el lenguaje refinado,

ni con los gobernantes, la mentira.

8Vara17:8 Vara. Lit. Piedra. mágica es el soborno para quien lo ofrece,

pues todo lo que emprende lo consigue.

9El que perdona la ofensa cultiva el amor;

el que insiste en la ofensa divide a los amigos.

10Cala más una reprensión en el hombre prudente

que cien latigazos en el obstinado.

11El revoltoso siempre anda buscando camorra,

pero se las verá con un mensajero cruel.

12Más vale toparse con una osa a la que le quitaron los cachorros

que con un necio empecinado en su necedad.

13El mal nunca se apartará

de la familia de aquel que devuelve mal por bien.

14Iniciar una pelea es romper una represa;

vale más retirarse que comenzarla.

15Absolver al culpable y condenar al inocente

son dos cosas que el Señor aborrece.

16¿De qué le sirve al necio poseer dinero?

¿Podrá adquirir sabiduría si le falta entendimiento?17:16 entendimiento. Lit. corazón.

17En todo tiempo ama el amigo;

para ayudar en la adversidad nació el hermano.

18El que es imprudente se compromete por otros,

y sale fiador de su prójimo.

19Al que le gusta pecar, le gusta pelear;

el que abre mucho la boca busca que se la rompan.17:19 el que abre … se la rompan. Lit. el que abre su puerta busca destrucción.

20El de corazón perverso jamás prospera;

el de lengua engañosa caerá en desgracia.

21Engendrar a un hijo necio es causa de pesar;

ser padre de un necio no es ninguna alegría.

22Gran remedio es el corazón alegre,

pero el ánimo decaído seca los huesos.

23El malvado acepta soborno en secreto,

con lo que tuerce el curso de la justicia.

24La meta del prudente es la sabiduría;

el necio divaga contemplando vanos horizontes.17:24 el necio … horizontes. Lit. y los ojos del necio en los confines de la tierra.

25El hijo necio irrita a su padre,

y causa amargura a su madre.

26No está bien castigar al inocente,

ni azotar por su rectitud a gente honorable.

27El que es entendido refrena sus palabras;

el que es prudente controla sus impulsos.

28Hasta un necio pasa por sabio si guarda silencio;

se le considera prudente si cierra la boca.