116:1 Mt 10:19; Mit 19:21Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu,
bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana.
216:2 1Sam 16:7; 2Nya 6:30; Lk 16:15; Dan 5:27Njia zote za mtu huonekana safi machoni pake mwenyewe,
bali makusudi hupimwa na Bwana.
316:3 2Nya 20:20; Za 20:4Mkabidhi Bwana lolote ufanyalo,
nayo mipango yako itafanikiwa.
416:4 Isa 43:7; Kut 9:16; 2Nya 34:24; Rum 9:22Bwana hufanya kila kitu kwa kusudi lake mwenyewe;
hata waovu kwa siku ya maangamizi.
516:5 Za 40:4; Mit 6:16; 11:20-21Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo.
Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.
616:6 Kut 20:20; Mit 14:16; Dan 4:26Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa;
kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya.
716:7 Kol 1:10; Mwa 39:21; Za 105:15; Yer 39:12; 40:1; 42:12; Dan 1:9Njia za mtu zinapompendeza Bwana,
huwafanya hata adui zake waishi naye kwa amani.
816:8 Za 37:16; Mit 15:16; 17:1; Mhu 4:6Afadhali kitu kidogo pamoja na haki
kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
916:9 Yer 10:23Moyo wa mtu huifikiri njia yake,
bali Bwana huelekeza hatua zake.
1016:10 Mit 17:7Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu,
wala kinywa chake hakipotoshi haki.
1116:11 Law 19:36; Mit 11:1; Eze 45:10Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana;
mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye.
1216:12 Mit 26:28; 25:5; 29:14; 31:5Wafalme huchukia sana kutenda maovu,
kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki.
1316:13 Mit 22:11Wafalme hufurahia midomo ya uaminifu;
humthamini mtu asemaye kweli.
1416:14 Mwa 40:2; Ay 29:24Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti,
bali mtu mwenye hekima ataituliza.
1516:15 2Nya 36:16; Mit 29:1; Yer 19:1116:15 Mwa 40:2; Ay 29:24; Mit 19:12; 25:2-7Uso wa mfalme ungʼaapo, inamaanisha uhai;
upendeleo wake ni kama wingu la mvua wakati wa vuli.
1616:16 Za 49:20; Ay 28:15; Mit 3:13-14Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu,
kuchagua ufahamu kuliko fedha!
1716:17 Mit 4:24-27; Isa 35:8; Mdo 24:16Njia kuu ya wanyofu huepuka ubaya;
yeye aichungaye njia yake, huchunga maisha yake.
1816:18 Es 5:12; Mit 29:23Kiburi hutangulia maangamizi,
roho ya majivuno hutangulia maanguko.
19Ni afadhali kuwa mnyenyekevu katika roho
miongoni mwa walioonewa
kuliko kugawana nyara pamoja na wenye kiburi.
2016:20 Isa 30:18; Za 32:10; Yer 17:7Yeyote anayekubali mafundisho hustawi,
tena amebarikiwa yeye anayemtumaini Bwana.
2116:21 Mit 16:23Wenye hekima moyoni huitwa wenye ufahamu,
na maneno ya kupendeza huchochea mafundisho.
2216:22 Mit 10:11Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wale walio nao,
bali upumbavu huleta adhabu kwa wapumbavu.
2316:23 Ay 15:5; Mit 16:21Moyo wa mtu mwenye hekima huongoza kinywa chake,
na midomo yake huchochea mafundisho.
2416:24 Mit 24:13-14Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali,
ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa.
2516:25 Mit 12:15; 14:12; Es 3:6Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,
bali mwisho wake huelekeza mautini.
2616:26 Mit 9:12; Mhu 6:7Shauku ya mfanyakazi humhimiza kufanya kazi;
njaa yake humsukuma aendelee.
2716:27 Yak 3:6Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya,
maneno yake ni kama moto uunguzao.
2816:28 Mit 14:17; 17:9Mtu mpotovu huchochea ugomvi,
nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu.
29Mtu mkali humvuta jirani yake
na kumwongoza katika mapito yale mabaya.
3016:30 Mit 6:13Yeye akonyezaye kwa jicho lake anapanga upotovu;
naye akazaye midomo yake amenuia mabaya.
3116:31 Mit 20:29Mvi ni taji ya utukufu;
hupatikana kwa maisha ya uadilifu.
3216:32 Mit 19:11Ni afadhali mtu mstahimilivu kuliko shujaa,
mtu anayeitawala hasira yake kuliko yule autekaye mji.
3316:33 Yos 7:14; Yn 1:7Kura hupigwa kwa siri,
lakini kila uamuzi wake hutoka kwa Bwana.
1心中的策划在于人,
应对之言来自耶和华。
2人看自己的行为都纯全,
但是耶和华却衡量人心。
3把你的事交托耶和华,
你的计划必实现。
4耶和华所造的万物各有其用,
连恶人也是为灾难之日所造。
5耶和华厌恶心骄气傲者,
他们必逃不过祂的责罚。
6慈爱和忠信可让罪恶得赎,
敬畏耶和华使人远离罪恶。
7人所行的若蒙耶和华喜悦,
耶和华必使仇敌与他和好。
8财物虽少但行事公义,
胜过家财万贯却不公义。
9人心中筹划自己的道路,
但耶和华决定他的脚步。
10王口中有上帝的话,
断案时必无差错。
11公道的秤与天平属于耶和华,
袋中一切的砝码由祂制定。
12君王憎恨恶行,
因王位靠公义而立。
13王喜爱公义的言词,
器重说话正直的人。
14王的烈怒如死亡使者,
然而智者能平息王怒。
15王的笑容带给人生命,
他的恩惠像春雨之云。
16得智慧胜过得黄金,
获悟性胜过获白银。
17正直人的大道远离罪恶,
坚守正道的保全性命。
18骄横是沦亡的前奏,
狂傲是败落的预兆。
19宁可谦卑地与贫寒人相处,
也不跟狂傲人共享战利品。
20听从训言的人受益匪浅,
信靠耶和华的人蒙祝福。
21智者以明辨著称,
甜言能说服人心。
22智慧是智者的生命泉,
愚昧为愚人带来惩罚。
23智者三思而后言,
其言使人长见识。
24良言如蜜,
使人心灵甘甜、身体康健。
25有一条路看似正确,
最终却通向死亡。
26工人的胃口促他工作,
口腹之需是他的动力。
27不务正业的人图谋恶事,
他的口舌如烈焰般危险。
28邪僻的人散播纷争,
造谣的人破坏友情。
29残暴之徒引诱邻舍走入歧途。
30恶人眯起眼睛图谋不轨,
歹徒咬着嘴唇策划恶事。
31白发是荣耀的冠冕,
行为公义方能得到。
32不轻易发怒者胜过勇士,
能自我控制胜过攻陷城池。
33人可以摇签求问,
但耶和华决定一切。