Mithali 15 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 15:1-33

115:1 Mit 25:15; 2Nya 10:7; 1Fal 12:7Jawabu la upole hugeuza ghadhabu,

bali neno liumizalo huchochea hasira.

215:2 Mit 12:23; Mhu 10:12; Za 59:7Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa,

bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.

315:3 2Nya 16:9; Ay 34:21; Ebr 4:13; Mit 5:21; Yer 16:17Macho ya Bwana yako kila mahali,

yakiwaangalia waovu na wema.

415:4 Za 5:9; Mit 10:11; 12:18Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima,

bali ulimi udanganyao huponda roho.

5Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake,

bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.

615:6 Mit 8:21; 10:16Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa,

bali mapato ya waovu huwaletea taabu.

715:7 Mit 15:2; 10:13Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa,

bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

815:8 Isa 61:8; Yer 6:20; Ay 35:13; Yn 9:31; Amo 5:22Bwana huchukia sana dhabihu za waovu,

bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.

915:9 Kum 7:13; 1Tim 6:11; Isa 51:1-7Bwana huchukia sana njia ya waovu,

bali huwapenda wale wafuatao haki.

1015:10 Mit 15:13; 17:22Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia;

yeye achukiaye maonyo atakufa.

1115:11 Ay 26:6; Za 139:8; Isa 2:3; Yn 2:24; Ufu 2:23Mauti15:11 Yaani Sheol, maana yake ni Kuzimu. na Uharibifu15:11 Kwa Kiebrania ni Abadon. viko wazi mbele za Bwana:

je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu!

12Mwenye mzaha huchukia maonyo;

hatataka shauri kwa mwenye hekima.

13Moyo wenye furaha hufanya uso uchangamke,

bali maumivu ya moyoni huponda roho.

14Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa,

bali kinywa cha mpumbavu hujilisha upumbavu.

15Siku zote za wanaoonewa ni za taabu,

bali moyo mchangamfu una karamu ya kudumu.

1615:16 Za 18:17; 1Tim 6:6; Mit 16:8Afadhali kuwa na kidogo pamoja na kumcha Bwana,

kuliko mali nyingi pamoja na ghasia.

1715:17 Mit 17:1; Mhu 4:6Afadhali chakula cha mboga mahali palipo na upendo

kuliko nyama ya ndama iliyonona pamoja na chuki.

1815:18 Mit 14:17; 26:21; Mwa 13:8; Mit 6:16-19; 14:17; Mwa 13:8Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi,

bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.

1915:19 Mit 22:5Njia ya mvivu imezibwa na miiba,

bali njia ya mwenye haki ni barabara kuu.

2015:20 Mit 10:1Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake,

bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.

2115:21 Mit 2:14; 10:23; Efe 5:15Upumbavu humfurahisha mtu ambaye hana akili,

bali mtu mwenye ufahamu hushika njia iliyonyooka.

2215:22 Mit 16:7; 1Fal 1:12; Mit 24:6; 11:14Mipango hushindwa kufanikiwa kwa ajili ya kukosa ushauri,

bali kukiwa na washauri wengi hufanikiwa.

2315:23 Mit 12:14; 25:11Mtu hupata furaha katika kutoa jibu linalofaa:

je, ni zuri namna gani neno lililotoka kwa wakati wake!

2415:24 Flp 3:20; 3:20Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima

kumwepusha asiende chini kaburini.

2515:25 Mit 12:7; Kum 19:14; Za 68:5-6; Kum 19:14; Mit 23:10-11Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi,

bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe.

2615:26 Za 59:7Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu,

bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye.

2715:27 Za 15:5; Isa 1:23; Yos 6:18; Zek 5:3; Za 94:11; Mit 6:16; Za 18:27Mtu mwenye tamaa huletea jamaa yake taabu,

bali yeye achukiaye rushwa ataishi.

2815:28 1Pet 3:15; Mit 14:8Moyo wa mwenye haki hupima majibu yake,

bali kinywa cha mwovu hufoka ubaya.

2915:29 Isa 59:2; Efe 2:12; Yn 9:21; Rum 8:26Bwana yuko mbali na waovu,

bali husikia maombi ya wenye haki.

3015:30 Mit 25:25Mtazamo wa tabasamu huleta furaha moyoni,

nazo habari njema huipa mifupa afya.

3115:31 Mit 9:7-9; 12:1Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima

atakuwa miongoni mwa wenye hekima.

3215:32 Mit 1:7; 12:1; Mhu 7:5Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe,

bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.

3315:33 Mit 29:23; Isa 66:2Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima,

nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

箴言 15:1-33

1温和的回答平息怒气,

粗暴的言词激起愤怒。

2智者的舌头传扬知识,

愚人的嘴巴吐露愚昧。

3耶和华的眼目无所不在,

善人和恶人都被祂鉴察。

4温和的言词带来生命,

乖谬的话语伤透人心。

5愚人蔑视父亲的管教,

接受责备的才算明智。

6义人家中财富充足,

恶人得利惹来祸患。

7智者的嘴传扬知识,

愚人的心并非如此。

8耶和华憎恨恶人的祭物,

悦纳正直人的祈祷。

9耶和华憎恨恶人的行径,

喜爱追求公义的人。

10背离正道,必遭严惩;

厌恶责备,必致死亡。

11阴间和冥府15:11 冥府”希伯来文是“亚巴顿”,参考启示录9:11在耶和华面前尚且无法隐藏,

何况世人的心思呢!

12嘲讽者不爱听责备,

也不愿请教智者。

13心中喜乐,容光焕发;

心里悲伤,精神颓丧。

14哲士渴慕知识,

愚人安于愚昧。

15困苦人天天受煎熬,

乐观者常常有喜乐。

16财物虽少但敬畏耶和华,

胜过家财万贯却充满烦恼。

17粗茶淡饭但彼此相爱,

胜过美酒佳肴却互相憎恨。

18脾气暴躁,惹起争端;

忍耐克制,平息纠纷。

19懒惰人的路布满荆棘,

正直人的道平坦宽阔。

20智慧之子使父亲欢喜,

愚昧的人却藐视母亲。

21无知者以愚昧为乐,

明哲人遵循正道。

22独断专行,计划失败;

集思广益,事无不成。

23应对得体,心中愉快;

言语合宜,何等美好!

24智者循生命之路上升,

以免坠入阴间。

25耶和华拆毁傲慢人的房屋,

祂使寡妇的地界完整无损。

26耶和华憎恨恶人的意念,

喜爱纯洁的言语。

27贪爱财富,自害己家;

厌恶贿赂,安然存活。

28义人三思而后答,

恶人张口吐恶言。

29耶和华远离恶人,

却听义人的祷告。

30笑颜令人心喜,

喜讯滋润骨头。

31倾听生命的训诫,

使人与智者同列。

32不受管教就是轻看自己,

听从责备才能得到智慧。

33敬畏耶和华使人得智慧,

学会谦卑后才能得尊荣。