Mithali 14 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 14:1-35

114:1 Rut 3:11; Mit 24:3Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,

bali mpumbavu huibomoa nyumba yake

kwa mikono yake mwenyewe.

214:2 Ay 12:4Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana,

bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.

314:3 Mit 12:6; 10:13Mazungumzo ya mpumbavu huleta fimbo mgongoni mwake,

bali mwenye hekima hulindwa na maneno ya midomo yake.

414:4 Za 12:2; Mit 12:17Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu,

bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.

514:5 Kut 20:16; Za 12:2; Mit 6:19Shahidi mwaminifu hadanganyi,

bali shahidi wa uongo humimina uongo.

614:6 Mit 9:9; 17:24Mwenye mzaha huitafuta hekima na haipati,

bali maarifa huja kwa urahisi kwa anayepambanua.

7Kaa mbali na mtu mpumbavu,

kwa maana hutapata maarifa katika midomo yake.

814:8 Lk 12:20; 1Kor 3:19; Mit 15:28; 21:29Hekima ya mwenye busara ni kufikiria njia zake,

bali upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

914:9 Mit 1:22; 10:23Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi,

bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.

10Kila moyo hujua uchungu wake wenyewe,

wala hakuna yeyote awezaye kushiriki furaha yake.

1114:11 Za 72:7; Ay 8:15; Mit 3:33Nyumba ya mwovu itaangamizwa,

bali hema la mnyofu litastawi.

1214:12 Rum 6:21; Mit 12:15; 16:25Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,

bali mwisho wake huelekeza mautini.

1314:13 Mhu 2:2; 7:3-6Hata katika kicheko moyo waweza kuuma,

nayo furaha yaweza kuishia katika majonzi.

1414:14 2Nya 15:7; Mit 12:14Wasio na imani watapatilizwa kikamilifu kwa ajili ya njia zao,

naye mtu mwema atapewa thawabu kwa ajili ya njia yake.

1514:15 Mit 14:8Mtu mjinga huamini kila kitu,

bali mwenye busara hufikiria hatua zake.

1614:16 Kut 20:20; Mit 22:3Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya,

bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.

1714:17 Mit 28:25; 29:22Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu,

naye mtu wa hila huchukiwa.

18Mjinga hurithi upumbavu,

bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.

1914:19 Mit 11:29Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema,

nao waovu kwenye malango ya wenye haki.

2014:20 Mit 19:4, 7Maskini huepukwa hata na majirani zao,

bali matajiri wana marafiki wengi.

2114:21 Mit 11:12; 19:17; Za 41:1Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi,

bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

2214:22 Mit 4:16-17Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki?

Bali wale wanaopanga kilicho chema

hupata upendo na uaminifu.

23Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida,

bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.

2414:24 Mit 14:8Utajiri wa wenye hekima ni taji yao,

bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.

2514:25 Mit 12:17Shahidi wa kweli huokoa maisha,

bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.

2614:26 Mit 19:23; Isa 33:6Yeye amchaye Bwana ana ngome salama,

na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.

2714:27 Za 18:5; Mit 13:14Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima,

ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.

2814:28 2Sam 19:7Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme,

bali pasipo watu mkuu huangamia.

2914:29 Mhu 7:8-9; Mit 15:18; Yak 1:19Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi,

bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.

3014:30 Ay 5:2; Mdo 7:9; Mit 12:4Moyo wenye amani huupa mwili uzima,

bali wivu huozesha mifupa.

3114:31 Ay 31:15-16; Mit 17:5Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao,

bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

3214:32 Za 34:21; Mit 6:15; Ay 13:15; 2Tim 4:18Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu,

bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.

3314:33 Mit 2:6-10Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu

bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.

3414:34 Mit 11:11Haki huinua taifa,

bali dhambi ni aibu kwa watu wote.

3514:35 Es 8:2; Mt 25:14-30Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima,

bali ghadhabu yake humwangukia

mtumishi mwenye kuaibisha.

Nueva Versión Internacional

Proverbios 14:1-35

1La mujer sabia edifica su casa;

la necia, con sus manos la destruye.

2El que va por buen camino teme al Señor;

el que va por malos caminos lo desprecia.

3De la boca del necio brota arrogancia;

los labios del sabio son su propia protección.

4Donde no hay bueyes el granero está vacío;

con la fuerza del buey aumenta la cosecha.

5El testigo veraz jamás miente;

el testigo falso propaga mentiras.

6El insolente busca sabiduría y no la halla;

para el entendido, el conocimiento es cosa fácil.

7Mantente a distancia del necio,

pues en sus labios no hallarás conocimiento.

8La sabiduría del prudente es discernir sus caminos,

pero al necio lo engaña su propia necedad.

9Los necios hacen mofa de sus propias faltas,

pero entre los íntegros hay buena voluntad.

10Cada corazón conoce sus propias amarguras,

y ningún extraño comparte su alegría.

11La casa del malvado será destruida,

pero la morada del justo prosperará.

12Hay un camino que al hombre le parece recto,

pero acaba por ser camino de muerte.

13Hasta de reírse duele el corazón

y hay alegrías que acaban en tristezas.

14El inconstante recibirá todo el pago de su inconstancia;

el hombre bueno, el premio de sus acciones.

15El inexperto cree todo lo que le dicen;

el prudente se fija por dónde va.

16El sabio teme al Señor y se aparta del mal,

pero el necio es arrogante y se pasa de confiado.

17El iracundo actúa neciamente

y el malvado es odiado.

18Herencia de los inexpertos es la necedad;

corona de los prudentes, el conocimiento.

19Los malvados se postrarán ante los buenos;

los impíos, ante las puertas de los justos.

20Al pobre hasta sus amigos lo aborrecen,

pero son muchos los que aman al rico.

21Es un pecado despreciar al prójimo;

¡dichoso el que se compadece de los pobres!

22Pierden el camino los que planean el mal,

pero hallan amor y verdad los que hacen el bien.

23Todo esfuerzo tiene su recompensa,

pero quedarse en las palabras solamente, lleva a la pobreza.

24La corona del sabio es su riqueza;

la de los necios, su necedad.

25El testigo veraz salva vidas,

pero el testigo falso miente.

26El temor del Señor es un baluarte seguro

que sirve de refugio a los hijos.

27El temor del Señor es fuente de vida

y libera de los lazos de la muerte.

28Gloria del rey es gobernar a una gran población;

un príncipe sin súbditos está arruinado.

29El que es paciente muestra gran inteligencia;

el que es agresivo muestra mucha insensatez.

30El corazón tranquilo da vida al cuerpo,

pero la envidia carcome los huesos.

31El que oprime al pobre ofende a su Creador,

pero honra a Dios quien se apiada del necesitado.

32El malvado cae por su propia maldad;

el justo, aun en su muerte, halla refugio en Dios.14:32 en Dios; en su propia piedad (LXX y Siríaca).

33En el corazón de los entendidos mora la sabiduría,

pero los necios ni siquiera la conocen.14:33 los necios … conocen (LXX y Siríaca); los necios la conocen (TM).

34La justicia enaltece a una nación,

pero el pecado deshonra a todos los pueblos.

35El rey favorece al siervo inteligente,

pero descarga su ira sobre el sinvergüenza.