Mithali 14 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 14:1-35

114:1 Rut 3:11; Mit 24:3Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,

bali mpumbavu huibomoa nyumba yake

kwa mikono yake mwenyewe.

214:2 Ay 12:4Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana,

bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.

314:3 Mit 12:6; 10:13Mazungumzo ya mpumbavu huleta fimbo mgongoni mwake,

bali mwenye hekima hulindwa na maneno ya midomo yake.

414:4 Za 12:2; Mit 12:17Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu,

bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.

514:5 Kut 20:16; Za 12:2; Mit 6:19Shahidi mwaminifu hadanganyi,

bali shahidi wa uongo humimina uongo.

614:6 Mit 9:9; 17:24Mwenye mzaha huitafuta hekima na haipati,

bali maarifa huja kwa urahisi kwa anayepambanua.

7Kaa mbali na mtu mpumbavu,

kwa maana hutapata maarifa katika midomo yake.

814:8 Lk 12:20; 1Kor 3:19; Mit 15:28; 21:29Hekima ya mwenye busara ni kufikiria njia zake,

bali upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

914:9 Mit 1:22; 10:23Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi,

bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.

10Kila moyo hujua uchungu wake wenyewe,

wala hakuna yeyote awezaye kushiriki furaha yake.

1114:11 Za 72:7; Ay 8:15; Mit 3:33Nyumba ya mwovu itaangamizwa,

bali hema la mnyofu litastawi.

1214:12 Rum 6:21; Mit 12:15; 16:25Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,

bali mwisho wake huelekeza mautini.

1314:13 Mhu 2:2; 7:3-6Hata katika kicheko moyo waweza kuuma,

nayo furaha yaweza kuishia katika majonzi.

1414:14 2Nya 15:7; Mit 12:14Wasio na imani watapatilizwa kikamilifu kwa ajili ya njia zao,

naye mtu mwema atapewa thawabu kwa ajili ya njia yake.

1514:15 Mit 14:8Mtu mjinga huamini kila kitu,

bali mwenye busara hufikiria hatua zake.

1614:16 Kut 20:20; Mit 22:3Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya,

bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.

1714:17 Mit 28:25; 29:22Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu,

naye mtu wa hila huchukiwa.

18Mjinga hurithi upumbavu,

bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.

1914:19 Mit 11:29Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema,

nao waovu kwenye malango ya wenye haki.

2014:20 Mit 19:4, 7Maskini huepukwa hata na majirani zao,

bali matajiri wana marafiki wengi.

2114:21 Mit 11:12; 19:17; Za 41:1Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi,

bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

2214:22 Mit 4:16-17Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki?

Bali wale wanaopanga kilicho chema

hupata upendo na uaminifu.

23Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida,

bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.

2414:24 Mit 14:8Utajiri wa wenye hekima ni taji yao,

bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.

2514:25 Mit 12:17Shahidi wa kweli huokoa maisha,

bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.

2614:26 Mit 19:23; Isa 33:6Yeye amchaye Bwana ana ngome salama,

na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.

2714:27 Za 18:5; Mit 13:14Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima,

ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.

2814:28 2Sam 19:7Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme,

bali pasipo watu mkuu huangamia.

2914:29 Mhu 7:8-9; Mit 15:18; Yak 1:19Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi,

bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.

3014:30 Ay 5:2; Mdo 7:9; Mit 12:4Moyo wenye amani huupa mwili uzima,

bali wivu huozesha mifupa.

3114:31 Ay 31:15-16; Mit 17:5Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao,

bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

3214:32 Za 34:21; Mit 6:15; Ay 13:15; 2Tim 4:18Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu,

bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.

3314:33 Mit 2:6-10Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu

bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.

3414:34 Mit 11:11Haki huinua taifa,

bali dhambi ni aibu kwa watu wote.

3514:35 Es 8:2; Mt 25:14-30Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima,

bali ghadhabu yake humwangukia

mtumishi mwenye kuaibisha.

Ketab El Hayat

الأمثال 14:1-35

1حِكْمَةُ الْمَرْأَةِ تَبْنِي بَيْتَهَا، وَحَمَاقَتُهَا تَهْدِمُهُ بِيَدَيْهَا. 2السَّالِكُ بِاسْتِقَامَتِهِ يَتَّقِي الرَّبَّ، وَذُو الطُّرُقِ الْمُعْوَجَّةِ يَسْتَخِفُّ بِهِ. 3فِي أَقْوَالِ فَمِ الْجَاهِلِ سَفَاهَةٌ تُخْزِي كِبْرِيَاءَهُ، أَمَّا شِفَاهُ الْحُكَمَاءِ فَتَصُونُهُمْ. 4الْحَظِيرَةُ الْخَاوِيَةُ مِنَ الْبَقَرِ مَعْلِفُهَا فَارِغٌ، وَوَفْرَةُ الْغِلالِ بِقُوَّةِ الثَّوْرِ. 5الشَّاهِدُ الأَمِينُ لَا يَكْذِبُ، وَالشَّاهِدُ الزُّورُ يَنْفُثُ كَذِباً. 6عَبَثاً يَلْتَمِسُ الأَحْمَقُ حِكْمَةً، أَمَّا الْعِلْمُ فَمُتَيَسِّرٌ لِلْفَطِنِ. 7انْصَرِفْ مِنْ حَضْرَةِ الْجَاهِلِ إِذْ لَا عِلْمَ فِي أَقْوَالِهِ. 8حِكْمَةُ الْعَاقِلِ فِي تَبَيُّنِ حُسْنِ مَسْلَكِهِ، وَغَبَاوَةُ الْجُهَّالِ فِي ارْتِكَابِ خِدَعِهِمْ. 9كُلُّ جَاهِلٍ يَسْتَهْزِئُ بِالإِثْمِ، أَمَّا بَيْنَ الْمُسْتَقِيمِينَ فَيَشِيعُ رِضَى اللهِ. 10الْقَلْبُ وَحْدَهُ يَعْرِفُ عُمْقَ مَرَارَةِ نَفْسِهِ، وَلا يُقَاسِمُهُ فَرَحَهُ غَرِيبٌ.

11بَيْتُ الأَشْرَارِ يَنْهَارُ، وَخِبَاءُ الْمُسْتَقِيمِينَ يَزْدَهِرُ. 12رُبَّ طَرِيقٍ تَبْدُو لِلإِنْسَانِ قَوِيمَةً، وَلَكِنَّ عَاقِبَتَهَا هُوَّةُ الْمَوْتِ. 13فِي الضَّحِكِ أَيْضاً تَطْغَى الْكَآبَةُ عَلَى الْقَلْبِ، وَعَاقِبَةُ الْفَرَحِ الْغَمُّ. 14ذُو الْقَلْبِ الْمُرْتَدِّ يُجَازَى بِمُقْتَضَى طُرُقِهِ، وَالصَّالِحُ يُثَابُ. 15الْغَبِيُّ يُصَدِّقُ كُلَّ كَلِمَةٍ تُقَالُ لَهُ، وَالْعَاقِلُ يَتَنَبَّهُ إِلَى مَوْقِعِ خَطْوَاتِهِ. 16الْحَكِيمُ يَخْشَى الشَّرَّ وَيَتَفَادَاهُ، وَالْجَاهِلُ يَتَصَلَّفُ وَيَدَّعِي الثِّقَةَ بِالنَّفْسِ. 17ذُو الطَّبْعِ الْحَادِّ يَتَصَرَّفُ بِحُمْقٍ، وَذُو الْمَكَائِدِ مَمْقُوتٌ. 18يَرِثُ الأَغْبِيَاءُ الْحَمَاقَةَ، وَيُتَوَّجُ الْعُقَلاءُ بِالْعِلْمِ. 19يَنْحَنِي الأَشْرَارُ فِي مَحْضَرِ الأَخْيَارِ، وَالأَثَمَةُ لَدَى الصِّدِّيقِ.

20الْفَقِيرُ مَكْرُوهٌ حَتَّى عِنْدَ جَارِهِ، أَمَّا مُحِبُّو الْغَنِيِّ فَكَثِيرُونَ. 21مَنْ يَحْتَقِرُ صَاحِبَهُ يَأْثَمُ، وَطُوبَى لِمَنْ يَرْحَمُ الْبَائِسِينَ.

22أَلا يَضِلُّ مُخْتَرِعُو الشَّرِّ؟ أَمَّا الْعَامِلُونَ خَيْراً فَيُلاقُونَ رَحْمَةً وَصِدْقاً. 23فِي كُلِّ جَهْدٍ مَبْذُولٍ رِبْحٌ، أَمَّا مُجَرَّدُ الْكَلامِ فَيُؤَدِّي إِلَى الْفَقْرِ. 24تَاجُ الْحُكَمَاءِ غِنَى حِكْمَتِهِمْ، وَالْحَمَاقَةُ إِكْلِيلُ الْجُهَّالِ. 25شَاهِدُ الْحَقِّ يُنَجِّي النُّفُوسَ، وَالنَّاطِقُ بِالزُّورِ يَنْفُثُ كَذِباً. 26فِي تَقْوَى الرَّبِّ ثِقَةٌ شَدِيدَةٌ؛ فِيهَا يَجِدُ أَبْنَاؤُهُ مَلاذاً. 27تَقْوَى الرَّبِّ يَنْبُوعُ حَيَاةٍ لِتَفَادِي أَشْرَاكِ الْمَوْتِ. 28فِي كَثْرَةِ الشَّعْبِ فَخْرٌ لِلْمَلِكِ، وَفِي فُقْدَانِ الرَّعِيَّةِ دَمَارٌ لِمَقَامِ الأَمِيرِ. 29الْبَطِيءُ الْغَضَبِ ذُو فَهْمٍ كَثِيرٍ، أَمَّا السَّرِيعُ إِلَى السَّخْطِ فَيُبْدِي حَمَاقَةً. 30الْقَلْبُ الْمُطْمَئِنُّ يَهَبُ أَعْضَاءَ الْجَسَدِ حَيَاةً، وَالْحَسَدُ يَنْخُرُ فِي الْعِظَامِ. 31مَنْ يَجُورُ عَلَى الْفَقِيرِ يُهِينُ صَانِعَهُ، وَمَنْ يَرْحَمُ الْبَائِسَ يُكْرِمُ خَالِقَهُ، 32يُعَاقَبُ الشِّرِّيرُ بِمُقْتَضَى سُوءِ تَصَرُّفَاتِهِ، أَمَّا الصِّدِّيقُ فَلَهُ مُعْتَصَمٌ عِنْدَ مَوْتِهِ. 33فِي قَلْبِ الْفَطِنِ تَسْتَقِرُّ الْحِكْمَةُ، وَيَخْلُو مِنْهَا قَلْبُ الْجُهَّالِ. 34الْبِرُّ يَسْمُو بِالأُمَّةِ، وَالْخَطِيئَةُ عَارٌ لِكُلِّ شَعْبٍ. 35الْعَبْدُ الْعَاقِلُ يَحْظَى بِرِضَى الْمَلِكِ، وَالْعَبْدُ الْمُخْزِي يَسْتَجْلِبُ سُخْطَهُ.