Mithali 12 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 12:1-28

Mafundisho Ya Kifamilia Na Ya Kijamii

112:1 Mit 5:11-14; 9:7-9; 13:1, 18; 15:5, 10Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa,

bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.

212:2 Ay 33:26; Za 84:11; 2Sam 15:3; Mit 11:20Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana,

bali Bwana humhukumu mwenye hila.

312:3 Mit 10:25Mtu hathibitiki kutokana na uovu,

bali mwenye haki hataondolewa.

412:4 Mit 14:30; 31:23; 1Kor 11:7; Rum 3:11Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe,

bali aaibishaye ni kama uozo

katika mifupa ya mumewe.

5Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki,

bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.

612:6 Mit 11:9; 14:3Maneno ya waovu huotea kumwaga damu,

bali maneno ya waadilifu huwaokoa.

712:7 Mt 7:24; Za 37:34; Mit 14:11; 15:25Watu waovu huondolewa na kutoweka,

bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.

812:8 1Sam 13:13; Mal 2:8-9; Mt 27:4-5Mtu husifiwa kulingana na hekima yake,

bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.

9Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi,

kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.

1012:10 Kum 25:4; Hes 22:29Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake,

bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.

1112:11 Mwa 3:19; Efe 4:28Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,

bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.

1212:12 Za 1:3; Lk 8:15Waovu hutamani mateka ya watu wabaya,

bali shina la mwenye haki hustawi.

1312:13 Za 59:12; Mit 10:6; 21:23; 2Pet 2:9Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi,

bali mwenye haki huepuka taabu.

1412:14 Mit 15:23; 14:14; Isa 3:10-11Kutokana na tunda la midomo yake

mtu hujazwa na mambo mema,

hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.

1512:15 Mit 16:2, 25; Lk 18:11Njia ya mpumbavu huonekana sawa

machoni pake mwenyewe,

bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.

1612:16 1Sam 25:25; Ay 5:2; Mit 29:11Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja,

bali mtu wa busara hupuuza matukano.

1712:17 Za 12:2; Mit 14:5, 25Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika,

bali shahidi wa uongo husema uongo.

1812:18 Za 57:4; Mit 25:18; 15:4Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga,

bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.

1912:19 Zek 1:5, 6Midomo isemayo kweli hudumu milele,

bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.

2012:20 Rum 14:19Upo udanganyifu katika mioyo

ya wale ambao hupanga mabaya,

bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.

2112:21 Ay 4:7; Za 91:10; Rum 8:28Hakuna dhara linalompata mwenye haki,

bali waovu wana taabu nyingi.

2212:22 1Fal 13:18; Ufu 22:15; Mit 11:20Bwana anachukia sana midomo idanganyayo,

bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.

2312:23 Mit 10:14; Za 38:5; 59:7; Mit 18:2Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe,

bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.

2412:24 Mit 10:4; 1Fal 11:28Mikono yenye bidii itatawala,

bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.

2512:25 Mit 15:13; Isa 50:4Moyo wa wasiwasi humlemea mtu,

bali neno la huruma humfurahisha.

2612:26 Za 95:10Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki,

bali njia ya waovu huwapotosha.

27Mtu mvivu haoki mawindo yake,

bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.

2812:28 Kum 30:15; Rum 5:21; Mit 10:2Katika njia ya haki kuna uzima;

katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

King James Version

Proverbs 12:1-28

1Whoso loveth instruction loveth knowledge: but he that hateth reproof is brutish. 2A good man obtaineth favour of the LORD: but a man of wicked devices will he condemn. 3A man shall not be established by wickedness: but the root of the righteous shall not be moved. 4A virtuous woman is a crown to her husband: but she that maketh ashamed is as rottenness in his bones. 5The thoughts of the righteous are right: but the counsels of the wicked are deceit. 6The words of the wicked are to lie in wait for blood: but the mouth of the upright shall deliver them. 7The wicked are overthrown, and are not: but the house of the righteous shall stand. 8A man shall be commended according to his wisdom: but he that is of a perverse heart shall be despised.12.8 of a…: Heb. perverse of heart 9He that is despised, and hath a servant, is better than he that honoureth himself, and lacketh bread. 10A righteous man regardeth the life of his beast: but the tender mercies of the wicked are cruel.12.10 tender…: or, bowels 11He that tilleth his land shall be satisfied with bread: but he that followeth vain persons is void of understanding. 12The wicked desireth the net of evil men: but the root of the righteous yieldeth fruit.12.12 the net: or, the fortress 13The wicked is snared by the transgression of his lips: but the just shall come out of trouble.12.13 The wicked…: Heb. The snare of the wicked is in the transgression of lips 14A man shall be satisfied with good by the fruit of his mouth: and the recompence of a man’s hands shall be rendered unto him. 15The way of a fool is right in his own eyes: but he that hearkeneth unto counsel is wise. 16A fool’s wrath is presently known: but a prudent man covereth shame.12.16 presently: Heb. in that day 17He that speaketh truth sheweth forth righteousness: but a false witness deceit. 18There is that speaketh like the piercings of a sword: but the tongue of the wise is health. 19The lip of truth shall be established for ever: but a lying tongue is but for a moment. 20Deceit is in the heart of them that imagine evil: but to the counsellors of peace is joy. 21There shall no evil happen to the just: but the wicked shall be filled with mischief. 22Lying lips are abomination to the LORD: but they that deal truly are his delight. 23A prudent man concealeth knowledge: but the heart of fools proclaimeth foolishness. 24The hand of the diligent shall bear rule: but the slothful shall be under tribute.12.24 slothful: or, deceitful 25Heaviness in the heart of man maketh it stoop: but a good word maketh it glad. 26The righteous is more excellent than his neighbour: but the way of the wicked seduceth them.12.26 excellent: or, abundant 27The slothful man roasteth not that which he took in hunting: but the substance of a diligent man is precious. 28In the way of righteousness is life; and in the pathway thereof there is no death.