Mithali 12 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 12:1-28

Mafundisho Ya Kifamilia Na Ya Kijamii

112:1 Mit 5:11-14; 9:7-9; 13:1, 18; 15:5, 10Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa,

bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.

212:2 Ay 33:26; Za 84:11; 2Sam 15:3; Mit 11:20Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana,

bali Bwana humhukumu mwenye hila.

312:3 Mit 10:25Mtu hathibitiki kutokana na uovu,

bali mwenye haki hataondolewa.

412:4 Mit 14:30; 31:23; 1Kor 11:7; Rum 3:11Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe,

bali aaibishaye ni kama uozo

katika mifupa ya mumewe.

5Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki,

bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.

612:6 Mit 11:9; 14:3Maneno ya waovu huotea kumwaga damu,

bali maneno ya waadilifu huwaokoa.

712:7 Mt 7:24; Za 37:34; Mit 14:11; 15:25Watu waovu huondolewa na kutoweka,

bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.

812:8 1Sam 13:13; Mal 2:8-9; Mt 27:4-5Mtu husifiwa kulingana na hekima yake,

bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.

9Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi,

kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.

1012:10 Kum 25:4; Hes 22:29Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake,

bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.

1112:11 Mwa 3:19; Efe 4:28Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,

bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.

1212:12 Za 1:3; Lk 8:15Waovu hutamani mateka ya watu wabaya,

bali shina la mwenye haki hustawi.

1312:13 Za 59:12; Mit 10:6; 21:23; 2Pet 2:9Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi,

bali mwenye haki huepuka taabu.

1412:14 Mit 15:23; 14:14; Isa 3:10-11Kutokana na tunda la midomo yake

mtu hujazwa na mambo mema,

hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.

1512:15 Mit 16:2, 25; Lk 18:11Njia ya mpumbavu huonekana sawa

machoni pake mwenyewe,

bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.

1612:16 1Sam 25:25; Ay 5:2; Mit 29:11Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja,

bali mtu wa busara hupuuza matukano.

1712:17 Za 12:2; Mit 14:5, 25Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika,

bali shahidi wa uongo husema uongo.

1812:18 Za 57:4; Mit 25:18; 15:4Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga,

bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.

1912:19 Zek 1:5, 6Midomo isemayo kweli hudumu milele,

bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.

2012:20 Rum 14:19Upo udanganyifu katika mioyo

ya wale ambao hupanga mabaya,

bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.

2112:21 Ay 4:7; Za 91:10; Rum 8:28Hakuna dhara linalompata mwenye haki,

bali waovu wana taabu nyingi.

2212:22 1Fal 13:18; Ufu 22:15; Mit 11:20Bwana anachukia sana midomo idanganyayo,

bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.

2312:23 Mit 10:14; Za 38:5; 59:7; Mit 18:2Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe,

bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.

2412:24 Mit 10:4; 1Fal 11:28Mikono yenye bidii itatawala,

bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.

2512:25 Mit 15:13; Isa 50:4Moyo wa wasiwasi humlemea mtu,

bali neno la huruma humfurahisha.

2612:26 Za 95:10Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki,

bali njia ya waovu huwapotosha.

27Mtu mvivu haoki mawindo yake,

bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.

2812:28 Kum 30:15; Rum 5:21; Mit 10:2Katika njia ya haki kuna uzima;

katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Proverbios 12:1-28

1El que ama la disciplina ama el conocimiento,

pero el que la aborrece es un necio.

2El hombre bueno recibe el favor del Señor,

pero el intrigante recibe su condena.

3Nadie puede afirmarse por medio de la maldad;

solo queda firme la raíz de los justos.

4La mujer ejemplar12:4 ejemplar. Alt. fuerte; véase 31:10-31. es corona de su esposo;

la desvergonzada es carcoma en los huesos.

5En los planes del justo hay justicia,

pero en los consejos del malvado hay engaño.

6Las palabras del malvado son insidias de muerte,

pero la boca de los justos los pone a salvo.

7Los malvados se derrumban y dejan de existir,

pero los hijos de los justos permanecen.

8Al hombre se le alaba según su sabiduría,

pero al de mal corazón se le desprecia.

9Más vale menospreciado pero servido,

que reverenciado pero mal comido.

10El justo atiende a las necesidades de su bestia,

pero el malvado es de malas entrañas.

11El que labra su tierra tendrá abundante comida,

pero el que sueña despierto12:11 el que sueña despierto. Lit. el que persigue lo vacío; también en 28:19. es un imprudente.

12Los malos deseos son la trampa12:12 la trampa (texto probable); el botín (TM). de los malvados,

pero la raíz de los justos prospera.

13En el pecado de sus labios se enreda el malvado,

pero el justo sale del aprieto.

14Cada uno se sacia12:14 se sacia. Lit. se sacia de lo bueno. del fruto de sus labios,

y de la obra de sus manos recibe su recompensa.

15Al necio le parece bien lo que emprende,

pero el sabio escucha el consejo.

16El necio muestra en seguida su enojo,

pero el prudente pasa por alto el insulto.

17El testigo verdadero declara lo que es justo,

pero el testigo falso declara falsedades.

18El charlatán hiere con la lengua como con una espada,

pero la lengua del sabio brinda alivio.

19Los labios sinceros permanecen para siempre,

pero la lengua mentirosa dura solo un instante.

20En los que fraguan el mal habita el engaño,

pero hay gozo para los que promueven la paz.

21Al justo no le sobrevendrá ningún daño,

pero al malvado lo cubrirá la desgracia.

22El Señor aborrece a los de labios mentirosos,

pero se complace en los que actúan con lealtad.

23El hombre prudente no muestra lo que sabe,

pero el corazón de los necios proclama su necedad.

24El de manos diligentes gobernará;

pero el perezoso será subyugado.

25La angustia abate el corazón del hombre,

pero una palabra amable lo alegra.

26El justo es guía de su prójimo,12:26 Texto de difícil traducción.

pero el camino del malvado lleva a la perdición.

27El perezoso no atrapa presa,12:27 no atrapa presa. Alt. no pone a asar lo que ha cazado. Texto de difícil traducción.

pero el diligente ya posee una gran riqueza.

28En el camino de la justicia se halla la vida;

por ese camino se evita la muerte.