Mithali 11 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 11:1-31

111:1 Law 19:36; Ay 6:2; Mit 16:11; Eze 45:10Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu,

bali vipimo sahihi ni furaha yake.

211:2 Dan 4:30; Mit 16:18; 18:12Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu,

bali unyenyekevu huja na hekima.

311:3 Mit 13:6Uadilifu wa wenye haki huwaongoza,

bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.

411:4 Ay 20:20; Eze 7:19; Sef 1:18Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu,

bali haki huokoa kutoka mautini.

511:5 1Fal 8:36; Mit 5:21-23; 13:6; 21:7Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka,

bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.

611:6 Es 7:9; 1Tim 4:8; Mhu 10:8Haki ya wanyofu huwaokoa,

bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.

711:7 Ay 8:13; Mit 10:28Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka;

yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.

811:8 Mit 21:8Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu,

naye mtu mwovu huingia humo badala yake.

911:9 Mit 12:6; Yer 45:5; Ay 8:13Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu

humwangamiza jirani yake,

bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.

1011:10 2Fal 11:20; Mit 28:12; Es 8:15Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi;

mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.

1111:11 Mit 14:34; 29:8Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa,

bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.

1211:12 Mit 14:21; Ay 6:24Mtu asiye na akili humdharau jirani yake,

bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

1311:13 Law 19:16; 1Tim 5:13; Mit 20:19; 10:14Masengenyo husaliti tumaini,

bali mtu mwaminifu hutunza siri.

1411:14 Mit 20:18; 24:6; 2Sam 15:34; 1Fal 12:1; Mit 20:18; 2Sam 15:34; Mit 15:22; 24:6; 1Fal 12:1Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka,

bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.

1511:15 Mit 6:1; 17:18; 22:26-27Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka,

bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.

1611:16 Mit 31:31Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima,

bali wanaume wakorofi hupata mali tu.

1711:17 Mt 25:34Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe,

bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.

1811:18 Hos 10:12; Kut 1:20; Ay 4:8Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu,

bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.

1911:19 Kum 30:15; Mit 10:2; 1Sam 2:6; Za 89:48; Mit 1:18-19; Mhu 7:2; Yer 43:1Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima,

bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.

2011:20 1Nya 29:17; Za 52:7Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu,

bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.

2111:21 Mit 16:5; Za 112:2Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa,

bali wenye haki watakuwa huru.

22Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe

ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.

2311:23 Rum 2:8, 9Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema,

bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.

2411:24 Za 112:9Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi,

mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

2511:25 Mit 22:9; 2Kor 9:6-9; Mt 5:7Mtu mkarimu atastawi;

yeye awaburudishaye wengine

ataburudishwa mwenyewe.

2611:26 Amo 8:5; Ay 29:13Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka,

bali baraka itamkalia kichwani kama taji

yeye aliye radhi kuiuza.

2711:27 Es 7:10; Za 7:15-16Yeye atafutaye mema hupata ukarimu,

bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.

2811:28 Yer 9:23; 17:8; Mk 10:25; Za 52:8Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka,

bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.

2911:29 Mhu 5:16; Mit 14:19Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo,

naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.

3011:30 Mwa 2:9; Yak 5:20Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima,

naye mwenye hekima huvuta roho za watu.

3111:31 Yer 25:29; 49:12; 1Pet 4:18Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani,

si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

Nueva Versión Internacional

Proverbios 11:1-31

1El Señor aborrece las balanzas adulteradas,

pero aprueba las pesas exactas.

2Con el orgullo viene la deshonra;

con la humildad, la sabiduría.

3A los justos los guía su integridad;

a los infieles los destruye su perversidad.

4En el día de la ira de nada sirve ser rico,

pero la justicia libra de la muerte.

5La justicia endereza el camino de los íntegros,

pero la maldad hace caer a los malvados.

6La justicia de los íntegros los libra,

pero la codicia atrapa a los traidores.

7Muere el malvado y con él, su esperanza;

muere también su ilusión de poder.

8El justo se salva de la calamidad,

pero la desgracia le sobreviene al malvado.

9Con la boca el impío destruye a su prójimo,

pero los justos se libran por el conocimiento.

10Cuando los justos prosperan, la ciudad se alegra;

cuando los malvados perecen, hay gran regocijo.

11La bendición de los justos enaltece a la ciudad,

pero la boca de los malvados la destruye.

12El falto de juicio desprecia a su prójimo,

pero el entendido refrena su lengua.

13La gente chismosa revela los secretos;

la gente confiable es discreta.

14Sin dirección, la nación fracasa;

la victoria se alcanza con muchos consejeros.

15El fiador de un extraño saldrá perjudicado;

negarse a dar fianza11:15 a dar fianza. Lit. a estrechar la mano. es vivir seguro.

16La mujer bondadosa se gana el respeto;

los hombres violentos solo ganan riquezas.

17El que hace bien a otros se beneficia a sí mismo;

el que es cruel, a sí mismo se perjudica.

18El malvado obtiene ganancias ilusorias;

el que siembra justicia asegura su recompensa.

19El que es justo obtiene la vida;

el que persigue el mal se encamina a la muerte.

20El Señor aborrece a los de corazón perverso,

pero se complace en los que viven con integridad.

21Una cosa es segura:11:21 Una cosa es segura. Lit. Mano a mano. Los malvados no quedarán impunes,

pero los justos saldrán bien librados.

22Como argolla de oro en hocico de cerdo

es la mujer bella pero indiscreta.

23Los deseos de los justos terminan bien;

la esperanza de los malvados termina en ira.

24Unos dan a manos llenas y reciben más de lo que dan;

otros retienen indebidamente sus bienes y acaban en la miseria.

25El que es generoso prospera;

el que reanima a otros será reanimado.

26La gente maldice al que acapara el trigo,

pero colma de bendiciones al que gustoso lo vende.

27El que madruga para el bien halla buena voluntad;

el que anda tras el mal por el mal será alcanzado.

28El que confía en sus riquezas se marchita,

pero el justo se renueva como el follaje.

29El que perturba su casa no hereda más que el viento

y el necio termina sirviendo al sabio.

30El fruto del justo es árbol de vida;

y el sabio salva vidas.

31Si los justos reciben su pago aquí en la tierra,

¡cuánto más los impíos y los pecadores!