Mithali 11 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 11:1-31

111:1 Law 19:36; Ay 6:2; Mit 16:11; Eze 45:10Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu,

bali vipimo sahihi ni furaha yake.

211:2 Dan 4:30; Mit 16:18; 18:12Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu,

bali unyenyekevu huja na hekima.

311:3 Mit 13:6Uadilifu wa wenye haki huwaongoza,

bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.

411:4 Ay 20:20; Eze 7:19; Sef 1:18Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu,

bali haki huokoa kutoka mautini.

511:5 1Fal 8:36; Mit 5:21-23; 13:6; 21:7Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka,

bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.

611:6 Es 7:9; 1Tim 4:8; Mhu 10:8Haki ya wanyofu huwaokoa,

bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.

711:7 Ay 8:13; Mit 10:28Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka;

yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.

811:8 Mit 21:8Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu,

naye mtu mwovu huingia humo badala yake.

911:9 Mit 12:6; Yer 45:5; Ay 8:13Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu

humwangamiza jirani yake,

bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.

1011:10 2Fal 11:20; Mit 28:12; Es 8:15Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi;

mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.

1111:11 Mit 14:34; 29:8Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa,

bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.

1211:12 Mit 14:21; Ay 6:24Mtu asiye na akili humdharau jirani yake,

bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

1311:13 Law 19:16; 1Tim 5:13; Mit 20:19; 10:14Masengenyo husaliti tumaini,

bali mtu mwaminifu hutunza siri.

1411:14 Mit 20:18; 24:6; 2Sam 15:34; 1Fal 12:1; Mit 20:18; 2Sam 15:34; Mit 15:22; 24:6; 1Fal 12:1Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka,

bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.

1511:15 Mit 6:1; 17:18; 22:26-27Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka,

bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.

1611:16 Mit 31:31Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima,

bali wanaume wakorofi hupata mali tu.

1711:17 Mt 25:34Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe,

bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.

1811:18 Hos 10:12; Kut 1:20; Ay 4:8Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu,

bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.

1911:19 Kum 30:15; Mit 10:2; 1Sam 2:6; Za 89:48; Mit 1:18-19; Mhu 7:2; Yer 43:1Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima,

bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.

2011:20 1Nya 29:17; Za 52:7Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu,

bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.

2111:21 Mit 16:5; Za 112:2Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa,

bali wenye haki watakuwa huru.

22Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe

ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.

2311:23 Rum 2:8, 9Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema,

bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.

2411:24 Za 112:9Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi,

mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

2511:25 Mit 22:9; 2Kor 9:6-9; Mt 5:7Mtu mkarimu atastawi;

yeye awaburudishaye wengine

ataburudishwa mwenyewe.

2611:26 Amo 8:5; Ay 29:13Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka,

bali baraka itamkalia kichwani kama taji

yeye aliye radhi kuiuza.

2711:27 Es 7:10; Za 7:15-16Yeye atafutaye mema hupata ukarimu,

bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.

2811:28 Yer 9:23; 17:8; Mk 10:25; Za 52:8Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka,

bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.

2911:29 Mhu 5:16; Mit 14:19Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo,

naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.

3011:30 Mwa 2:9; Yak 5:20Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima,

naye mwenye hekima huvuta roho za watu.

3111:31 Yer 25:29; 49:12; 1Pet 4:18Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani,

si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

New International Version – UK

Proverbs 11:1-31

1The Lord detests dishonest scales,

but accurate weights find favour with him.

2When pride comes, then comes disgrace,

but with humility comes wisdom.

3The integrity of the upright guides them,

but the unfaithful are destroyed by their duplicity.

4Wealth is worthless in the day of wrath,

but righteousness delivers from death.

5The righteousness of the blameless makes their paths straight,

but the wicked are brought down by their own wickedness.

6The righteousness of the upright delivers them,

but the unfaithful are trapped by evil desires.

7Hopes placed in mortals die with them;

all the promise of11:7 Two Hebrew manuscripts; most Hebrew manuscripts, Vulgate, Syriac and Targum When the wicked die, their hope perishes; / all they expected from their power comes to nothing.

8The righteous person is rescued from trouble,

and it falls on the wicked instead.

9With their mouths the godless destroy their neighbours,

but through knowledge the righteous escape.

10When the righteous prosper, the city rejoices;

when the wicked perish, there are shouts of joy.

11Through the blessing of the upright a city is exalted,

but by the mouth of the wicked it is destroyed.

12Whoever derides their neighbour has no sense,

but the one who has understanding holds their tongue.

13A gossip betrays a confidence,

but a trustworthy person keeps a secret.

14For lack of guidance a nation falls,

but victory is won through many advisors.

15Whoever puts up security for a stranger will surely suffer,

but whoever refuses to shake hands in pledge is safe.

16A kind-hearted woman gains honour,

but ruthless men gain only wealth.

17Those who are kind benefit themselves,

but the cruel bring ruin on themselves.

18A wicked person earns deceptive wages,

but the one who sows righteousness reaps a sure reward.

19Truly the righteous attain life,

but whoever pursues evil finds death.

20The Lord detests those whose hearts are perverse,

but he delights in those whose ways are blameless.

21Be sure of this: the wicked will not go unpunished,

but those who are righteous will go free.

22Like a gold ring in a pig’s snout

is a beautiful woman who shows no discretion.

23The desire of the righteous ends only in good,

but the hope of the wicked only in wrath.

24One person gives freely, yet gains even more;

another withholds unduly, but comes to poverty.

25A generous person will prosper;

whoever refreshes others will be refreshed.

26People curse the one who hoards grain,

but they pray God’s blessing on the one who is willing to sell.

27Whoever seeks good finds favour,

but evil comes to one who searches for it.

28Those who trust in their riches will fall,

but the righteous will thrive like a green leaf.

29Whoever brings ruin on their family will inherit only wind,

and the fool will be servant to the wise.

30The fruit of the righteous is a tree of life,

and the one who is wise saves lives.

31If the righteous receive their due on earth,

how much more the ungodly and the sinner!