Mithali 11 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 11:1-31

111:1 Law 19:36; Ay 6:2; Mit 16:11; Eze 45:10Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu,

bali vipimo sahihi ni furaha yake.

211:2 Dan 4:30; Mit 16:18; 18:12Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu,

bali unyenyekevu huja na hekima.

311:3 Mit 13:6Uadilifu wa wenye haki huwaongoza,

bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.

411:4 Ay 20:20; Eze 7:19; Sef 1:18Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu,

bali haki huokoa kutoka mautini.

511:5 1Fal 8:36; Mit 5:21-23; 13:6; 21:7Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka,

bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.

611:6 Es 7:9; 1Tim 4:8; Mhu 10:8Haki ya wanyofu huwaokoa,

bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.

711:7 Ay 8:13; Mit 10:28Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka;

yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.

811:8 Mit 21:8Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu,

naye mtu mwovu huingia humo badala yake.

911:9 Mit 12:6; Yer 45:5; Ay 8:13Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu

humwangamiza jirani yake,

bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.

1011:10 2Fal 11:20; Mit 28:12; Es 8:15Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi;

mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.

1111:11 Mit 14:34; 29:8Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa,

bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.

1211:12 Mit 14:21; Ay 6:24Mtu asiye na akili humdharau jirani yake,

bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

1311:13 Law 19:16; 1Tim 5:13; Mit 20:19; 10:14Masengenyo husaliti tumaini,

bali mtu mwaminifu hutunza siri.

1411:14 Mit 20:18; 24:6; 2Sam 15:34; 1Fal 12:1; Mit 20:18; 2Sam 15:34; Mit 15:22; 24:6; 1Fal 12:1Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka,

bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.

1511:15 Mit 6:1; 17:18; 22:26-27Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka,

bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.

1611:16 Mit 31:31Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima,

bali wanaume wakorofi hupata mali tu.

1711:17 Mt 25:34Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe,

bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.

1811:18 Hos 10:12; Kut 1:20; Ay 4:8Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu,

bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.

1911:19 Kum 30:15; Mit 10:2; 1Sam 2:6; Za 89:48; Mit 1:18-19; Mhu 7:2; Yer 43:1Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima,

bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.

2011:20 1Nya 29:17; Za 52:7Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu,

bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.

2111:21 Mit 16:5; Za 112:2Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa,

bali wenye haki watakuwa huru.

22Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe

ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.

2311:23 Rum 2:8, 9Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema,

bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.

2411:24 Za 112:9Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi,

mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

2511:25 Mit 22:9; 2Kor 9:6-9; Mt 5:7Mtu mkarimu atastawi;

yeye awaburudishaye wengine

ataburudishwa mwenyewe.

2611:26 Amo 8:5; Ay 29:13Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka,

bali baraka itamkalia kichwani kama taji

yeye aliye radhi kuiuza.

2711:27 Es 7:10; Za 7:15-16Yeye atafutaye mema hupata ukarimu,

bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.

2811:28 Yer 9:23; 17:8; Mk 10:25; Za 52:8Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka,

bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.

2911:29 Mhu 5:16; Mit 14:19Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo,

naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.

3011:30 Mwa 2:9; Yak 5:20Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima,

naye mwenye hekima huvuta roho za watu.

3111:31 Yer 25:29; 49:12; 1Pet 4:18Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani,

si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

Священное Писание

Мудрые изречения 11:1-31

1Мерзость для Вечного – неверные весы,

а верный вес угоден Ему.

2Вслед за гордыней приходит позор,

а за смирением – мудрость.

3Прямодушных ведёт их непорочность,

а коварных губит их же лукавство.

4Бесполезно богатство в день гнева,

а праведность спасает от смерти.

5Праведность непорочных делает их пути прямыми,

а нечестивые падают от своего нечестия.

6Праведность прямодушных спасает их,

а вероломных захватывают злые страсти.

7Когда умирает грешник, гибнет его надежда;

ожидания нечестивых не сбудутся.

8Праведник избавляется от беды,

вместо него попадает в неё грешник.

9Своими устами безбожные губят ближнего,

но праведные спасаются своим знанием.

10Когда праведные процветают, город радуется;

когда гибнут грешные, звучат крики радости.

11Благословением праведных город превознесён,

но уста нечестивых его разрушают.

12Человек нерассудительный позорит ближнего,

а разумный сдерживает язык.

13Сплетник предаёт доверие,

а надёжный человек хранит тайну.

14При недостатке мудрого руководства народ гибнет,

а много советников обеспечивают победу.

15Всякий, ручающийся за чужого, накличет беду,

а избегающий поручительств – в безопасности.

16Добрая женщина приобретает славу,

и трудолюбивые мужчины скопят богатства11:16 Или: «а безжалостные мужчины скопят лишь богатства»..

17Милостивый человек сам себя вознаграждает,

а жестокий сам причиняет себе зло.

18Нечестивый трудится за призрачную награду,

а сеющий праведность получит верное вознаграждение.

19Держащийся праведности будет жить,

а гоняющийся за злом умрёт.

20Вечный гнушается сердцем лукавого,

но угодны Ему те, чей путь непорочен.

21Твёрдо знай: нечестивый не останется безнаказанным,

а те, кто праведен, спасутся.

22Что золотое кольцо у свиньи в пятачке,

то красивая, но безрассудная женщина.

23Ожидания праведных есть одно лишь благо,

а ожидания нечестивцев – гнев.

24Один даёт щедро, а всё богатеет;

другой бережлив непомерно, а впадает в нужду.

25Щедрая душа будет обогащена;

утоливший жажду другого и сам не будет жаждать.

26Того, кто прячет зерно, народ проклинает,

но кто готов продавать, увенчан благословением.

27Тот, кто стремится к добру, найдёт благоволение,

а зло придёт к тому, кто его искал.

28Надеющийся на богатства увянет,

а праведный будет цвести, как зелёная ветка.

29Наводящий беду на семью унаследует только ветер,

и глупец будет прислуживать мудрому.

30От плода праведных произрастает дерево жизни,

и мудрец привлекает души.

31Если праведным на земле воздаётся,

то нечестивцам и грешникам и подавно.