Mithali 1 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 1:1-33

Utangulizi: Kusudi Na Kiini

11:1 1Fal 4:29-34Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:

2Kwa kupata hekima na nidhamu;

kwa kufahamu maneno ya busara;

31:3 Mit 2:1; 2:1, 9kwa kujipatia nidhamu na busara,

kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;

41:4 Mit 8:5, 12; 2:10-11huwapa busara wajinga,

maarifa na akili kwa vijana;

51:5 Mit 9:9wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,

wenye kupambanua na wapate mwongozo;

61:6 Za 78:2; Mt 13:10-17; Hes 12:8; Amu 14:12kwa kufahamu mithali na mifano,

misemo na vitendawili vya wenye hekima.

71:7 Kut 20:20; Ay 28:28Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa,

lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.

Onyo Dhidi Ya Ushawishi Wa Marafiki Waovu

81:8 Mit 6:20; 22:17; Kum 21:18Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

91:9 Mit 3:21-22; 4:1-9Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako,

na mkufu wa kuipamba shingo yako.

101:10 Mwa 39:7; Ay 24:15; Kum 13:8; Rum 16:18Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi,

usikubaliane nao.

111:11 Mit 12:6; Yer 5:26; Mik 7:2Kama wakisema, “Twende tufuatane;

tukamvizie mtu na kumwaga damu,

njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;

121:12 Ay 33:18; Mwa 38:25; Za 40:3tuwameze wakiwa hai kama kaburi,1:12 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.

13Tutapata aina zote za vitu vya thamani

na kujaza nyumba zetu kwa nyara.

141:14 Mit 1:19Njoo ushirikiane nasi,

vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”

151:15 Za 119:101; Mwa 49:6; Mit 4:14Mwanangu, usiandamane nao.

Usiweke mguu wako katika njia zao,

161:16 Mit 6:18; Isa 59:7kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,

ni wepesi kumwaga damu.

17Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu

wakati ndege wote wanakuona!

181:18 Za 71:10Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe;

hujivizia tu wenyewe!

191:19 Mit 11:19; 15:27; 2Fal 5:20-27Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila;

huuondoa uhai wa wale wenye mali.

Onyo Dhidi Ya Kukataa Hekima

201:20 Ay 28:12; Mt 7:10-13; 9:1-3, 13-15Hekima huita kwa sauti kuu barabarani,

hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;

21kwenye makutano ya barabara za mji

zenye makelele mengi hupaza sauti,

kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:

221:22 Mit 6:32; 7:7; 8:5; 9:4, 16; Za 50:17“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini?

Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha,

na wapumbavu kuchukia maarifa?

231:23 Yoe 2:28; Yn 7:37Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu,

ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu

na kuwafahamisha maneno yangu.

241:24 Isa 65:12; Zek 7:11Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita

na hakuna yeyote aliyekubali

niliponyoosha mkono wangu,

251:25 Lk 7:30kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote

na hamkukubali karipio langu,

261:26 Za 2:4; Kum 28:63; Mit 10:24mimi nami nitawacheka katika maafa yenu,

nitawadhihaki wakati janga litawapata:

271:27 Za 18:18; Mit 5:12-14wakati janga litawapata kama tufani,

wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,

wakati dhiki na taabu zitawalemea.

281:28 Isa 1:15; Mik 3:4; Eze 8:18; Hos 5:6“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu;

watanitafuta lakini hawatanipata.

291:29 Ay 21:14; Isa 27:11; Mdo 7:51Kwa kuwa walichukia maarifa,

wala hawakuchagua kumcha Bwana,

301:30 Ay 21:14; Za 81:11kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu,

na kukataa maonyo yangu,

311:31 2Nya 36:16; Yer 14:16watakula matunda ya njia zao,

na watashibishwa matunda ya hila zao.

321:32 Isa 66:4; Yer 2:19Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua,

nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.

331:33 Hes 24:21; Za 25:12; 112:8Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama,

atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

Japanese Contemporary Bible

箴言 知恵の泉 1:1-33

1

箴言の目的と主題

1ダビデ王の子、イスラエルの王ソロモンの教え。

2-3ソロモン王がこの教訓を書いたのは、

人々がどんな時にも物事を正しく判断し、

公正であってほしいと考えたからです。

4「未熟な人たちが賢くなってほしい。」

「若い人が正しい生活を送るように注意したい。」

5-6「賢い人には、

これらの知恵のことばの深い真理をもっと探究し、

より賢くなり、

人々を指導できるようになってほしい。」

それが彼の願いでした。

序文――知恵を求め、悪者には警戒しなさい

7-9では、どうしたら賢く

なれるのでしょう。

まず主を信じ、主を大切にすることです。

愚かな人は主の教えをさげすみます。

両親の忠告に従いなさい。

そうすれば、あとになって

人々にほめられるようになります。

10もし悪い仲間が、「われわれの仲間に入れ」

と言っても、きっぱり断りなさい。

11「待ち伏せして人を襲い、

身ぐるみ巻き上げ、殺そう、

12正しい者も悪い者も見境なく。

13盗んだ物はわれわれのものだ。

あらゆる物が!

14さあ、仲間に入れ。山分けしよう」と誘われても、

15決してその誘いにのってはいけません。

そんな者たちには近寄らないようにしなさい。

16彼らは悪いことをするだけが生きがいで、

人殺しは彼らの専売特許なのです。

17鳥は罠が仕掛けられているところを見れば、

近寄りません。

18ところが、彼らは自分で自分を罠にかけているのです。

愚かなことに、罠をかけて

自分のいのちをつけねらっているのです。

19暴力をふるったり人殺しをしたりする者たちは、

みなこうなるのです。

彼らには悲惨な死が待っています。

知恵の勧め

20知恵は町の中で叫んでいます。

21大通りの群衆や法廷の裁判官、

そして国中の人に呼びかけます。

22「愚か者よ、いつまで聞き分けがないのか。

いつまで知恵をさげすみ、素直に真実を認めないのか。

23さあ、わたしの言うことを聞きなさい。

あなたに知恵の霊を注ぎ、賢くしよう。

24わたしは何度も呼んだのに、

あなたがたはそばに来ようともしなかった。

嘆願までしたのに、知らん顔をしていた。

25わたしの忠告にも叱責にも、耳を貸そうとしない。

26あなたがたには、いつか災いが起こる。

そのとき、わたしはあなたがたを笑う。

27災いが嵐のように襲いかかり、

恐れや苦しみに打ちのめされそうになるとき、

28そのときになって助けてくれと言っても、

わたしはあなたがたを助けない。

わたしを懸命に捜しても、もう遅い。

29それはあなたがたが真実から目をそむけ、

主を信頼せず、

30わたしの忠告を聞かずに、

やりたいことをやっていたからだ。

31あなたがたは、その報いを受けなければならない。

自分で選んだ道なのだから、十分苦しみ、

恐ろしい思いをするがいい。

32わたしをきらうとは、全く愚かな人たちだ。

一歩一歩死に近づいているのも知らずに、

いい気になっている。

33しかし、わたしに聞き従う人は、

何の心配もなく、毎日を平和に暮らす。」