Mika 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 6:1-16

Shauri La Bwana Dhidi Ya Israeli

16:1 Za 50:1; Eze 6:2Sikiliza asemalo Bwana:

“Simama, tetea shauri lako mbele ya milima;

vilima na visikie lile unalotaka kusema.

26:2 Kum 32:1; Hos 12:2; Isa 3:13; Za 50:7; Yer 9:7Sikilizeni, ee milima, mashtaka ya Bwana,

sikilizeni, enyi misingi ya milele ya dunia.

Kwa kuwa Bwana ana shauri dhidi ya watu wake;

anatoa mashtaka dhidi ya Israeli.

36:3 Za 50:7; Isa 5:3, 4; Yer 2:31; 2:5“Watu wangu, nimewatendea nini?

Nimewalemea kwa jinsi gani? Mnijibu.

46:4 Kum 7:8; Kut 3:10; 6:6; 4:16; 15:20; Hes 33:1; Za 77:20Nimewatoa kutoka Misri na kuwakomboa

kutoka nchi ya utumwa.

Nilimtuma Mose awaongoze,

pia Aroni na Miriamu.

56:5 Hes 22:2-6Watu wangu, kumbukeni jinsi Balaki mfalme wa Moabu

alivyofanya shauri

na kile Balaamu mwana wa Beori alichojibu.

Kumbukeni safari yenu kutoka Shitimu mpaka Gilgali,

ili mfahamu matendo ya haki ya Bwana.”

66:6 Yn 6:28; Za 15:1; 40:6-8; 95:2; 51:16-17Nimjie Bwana na kitu gani na kusujudu

mbele za Mungu aliyetukuka?

Je, nije mbele zake na sadaka za kuteketezwa,

nije na ndama za mwaka mmoja?

76:7 Isa 1:11; 40:16; Law 18:21; Za 50:8-10; 2Fal 3:27; 16:3; Amo 5:22; Hos 5:6Je, Bwana atafurahishwa na kondoo dume elfu,

au mito elfu kumi ya mafuta?

Je, nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu,

mtoto wangu mwenyewe

kwa ajili ya dhambi ya nafsi yangu?

86:8 Isa 1:17; Yer 22:3; 23:23; 2Fal 22:19; Isa 57:15; Mwa 5:22; 1Sam 15:22; Kum 10:12-13; Zek 7:9-10; Mt 9:13; Mk 12:33; Lk 11:42Amekuonyesha yaliyo mema, ee mwanadamu.

Bwana anataka nini kwako?

Ila kutenda kwa haki na kupenda rehema,

na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako.

Hatia Na Adhabu Ya Israeli

96:9 Mwa 17:1; Isa 11:4Sikiliza! Bwana anauita mji:

kulicha jina lako ni hekima:

“Tii hiyo fimbo na yeye aliyeiamuru.

106:10 Eze 45:9-10; Amo 3:10; 8:4-6Je, bado nisahau, ee nyumba ya uovu,

hazina yako uliyopata kwa udanganyifu

na vipimo vilivyopunguka,

ambavyo vimelaaniwa?

116:11 Law 19:36; Hos 12:7; Amu 3:10; Kum 25:13Je, naweza kuhukumu kuwa

mtu mwenye mizani ya udanganyifu hana hatia,

aliye na mfuko wa mawe ya kupimia ya uongo?

126:12 Isa 1:23; 3:8; Za 35:20; 116:11; Yer 9:5Matajiri wake ni wajeuri;

watu wake ni waongo

na ndimi zao zinazungumza

kwa udanganyifu.

13Kwa hiyo, nimeanza kukuharibu,

kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.

146:14 Isa 9:20; 30:6; Hos 4:10Mtakula lakini hamtashiba;

matumbo yenu bado yatakuwa matupu.

Mtaweka akiba lakini hamtaokoa chochote,

kwa sababu mtakachoweka akiba

nitatoa kwa upanga.

156:15 Kum 28:36-38; Yer 12:13; Ay 24:11; Amo 5:11; Sef 1:13Mtapanda lakini hamtavuna;

mtakamua zeituni lakini

hamtatumia mafuta yake.

Mtakamua zabibu

lakini hamtakunywa hiyo divai.

166:16 1Fal 16:25, 29-33; Yer 7:24; 25:9; 51:51; Mik 2:6Mmezishika sheria za Omri

na matendo yote ya nyumba ya Ahabu,

tena umefuata desturi zao.

Kwa hiyo nitakutoa kwa maangamizi

na watu wako kuwa dhihaka;

mtachukua dharau za mataifa.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

彌迦書 6:1-16

耶和華譴責以色列

1以色列人啊,

你們要聽耶和華的話:

「起來,你們要在高山面前申辯,

讓丘陵聽你們訴說。

2群山啊,大地永固的根基啊,

你們要聽耶和華的控告!

因為耶和華要控告祂的子民,

責備以色列人。

3「我的子民啊,

我做了什麼對不起你們的事?

我哪裡令你們厭煩?

回答我!

4我曾帶領你們離開埃及

把你們從受奴役之地救贖出來,

又差遣摩西亞倫米利暗引領你們。

5我的子民啊,

你們要回想摩押巴勒的陰謀以及比珥之子巴蘭給他的回答,

要回想你們從什亭吉甲途中的遭遇,

以便認識耶和華公義的作為。」

6我要拿什麼朝見耶和華,

在天上的上帝面前叩拜呢?

要獻上一歲的牛犢作燔祭嗎?

7耶和華會喜愛成千的公羊和萬條油河嗎?

我要因過犯而獻上自己的長子,

因心中的罪惡而獻上親生的骨肉嗎?

8世人啊,

耶和華已經指示你們何為良善。

祂向你們所要的是什麼呢?

是要你們行公義,好憐憫,

謙卑地與你們的上帝同行。

9耶和華在向耶路撒冷呼喊,

智者必敬畏祂的名。祂說:

「聚在城裡的眾人啊,你們要聽!

10我豈會忘記惡人家中的不義之財和可惡的小升斗?

11我豈會放過使用不公道的秤和法碼的人?

12城中的富人殘暴成性,

居民謊話連篇,

滿口詭詐之言。

13所以,我要重重地擊打你,

因你的罪惡而毀滅你。

14你吃,卻吃不飽,仍然腹中空空。

你聚斂錢財,卻保不住。

你保住的,我要交給拿刀的。

15你撒種,卻不得收割;

你榨橄欖,卻無油抹身;

你踩葡萄,卻無酒可喝。

16因為你遵守暗利的惡規,

效法亞哈家的惡行,

隨從他們的計謀,

所以我要使你荒涼,

讓你的居民成為笑柄。

你們要蒙受列國的羞辱。」