Mika 5 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 5:1-15

Mtawala Aliyeahidiwa Kutoka Bethlehemu

15:1 Ay 16:10; Mt 27:30; Mao 3:30Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi,

kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu.

Watampiga mtawala wa Israeli

shavuni kwa fimbo.

25:2 Yn 7:42; Mwa 35:19; 48:7; 1Sam 13:14; Hes 24:19; 2Sam 6:21; 2Nya 7:18; Za 90:2; 132:6; 102:25; Isa 9:6; Mit 8:22; Yn 1:1; Mt 2:6“Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi,

ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda,

kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu

yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,

ambaye asili yake ni kutoka zamani,

kutoka milele.”

35:3 Yer 7:29Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati

mwanamke aliye na utungu atakapozaa

na ndugu zake wengine warudi

kujiunga na Waisraeli.

45:4 Isa 40:11; 49:9; 52:13; Za 72:8; Zek 9:10; Mik 7:14; Eze 34:11-15; Lk 1:32Atasimama na kulichunga kundi lake

katika nguvu ya Bwana,

katika utukufu wa jina la Bwana Mungu wake.

Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo

ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.

55:5 Isa 8:7; 9:6; 10:24-27; Lk 2:14; Efe 2:14; Kol 1:19-20Naye atakuwa amani yao.

Ukombozi Na Uharibifu

Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu

na kupita katika ngome zetu,

tutawainua wachungaji saba dhidi yake,

hata viongozi wanane wa watu.

65:6 Mwa 10:8; Sef 2:13; Lk 1:71; Nah 2:11-13Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga,

nchi ya Nimrodi kwa upanga.

Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru

atakapoivamia nchi yetu

na kuingia katika mipaka yetu.

75:7 Amo 5:15; Mik 2:12; Isa 44:4; Za 110:3; 133:3Mabaki ya Yakobo yatakuwa

katikati ya mataifa mengi

kama umande kutoka kwa Bwana,

kama manyunyu juu ya majani,

ambayo hayamngoji mtu

wala kukawia kwa mwanadamu.

85:8 Mwa 49:9; Mik 4:13; Zek 10:5; Isa 5:29; Za 50:22; Hos 5:14Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa,

katikati ya mataifa mengi,

kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni,

kama mwana simba miongoni

mwa makundi ya kondoo,

ambaye anaumiza vibaya na kuwararua

kila anapopita katikati yao,

wala hakuna awezaye kuokoa.

95:9 Za 10:12Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako,

nao adui zako wote wataangamizwa.

105:10 Kut 15:4, 19; Hos 14:3; Hag 2:22; Zek 9:10“Katika siku ile,” asema Bwana,

“nitaangamiza farasi zenu katikati yenu

na kubomoa magari yenu ya vita.

115:11 Kum 29:23; Isa 6:11; Mao 2:2; Hos 10:14; Amo 5:9Nitaiangamiza miji ya nchi yenu

na kuziangusha chini ngome zenu zote.

125:12 Kum 18:10-12; Isa 8:19; 2:9Nitaangamiza uchawi wenu

na hamtapiga tena ramli.

135:13 Nah 1:14; Hos 2:10; Isa 2:8; 2:18; Eze 6:9; Zek 13:2Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga

na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu;

hamtasujudia tena

kazi ya mikono yenu.

145:14 Kut 34:13; Amu 3:7; 2Fal 17:10Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu

na kubomoa miji yenu.

155:15 Isa 65:12Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu

juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”

New International Version

Micah 5:1-15

A Promised Ruler From Bethlehem

5:0 In Hebrew texts 5:1 is numbered 4:14, and 5:2-15 is numbered 5:1-14. 1Marshal your troops now, city of troops,

for a siege is laid against us.

They will strike Israel’s ruler

on the cheek with a rod.

2“But you, Bethlehem Ephrathah,

though you are small among the clans5:2 Or rulers of Judah,

out of you will come for me

one who will be ruler over Israel,

whose origins are from of old,

from ancient times.”

3Therefore Israel will be abandoned

until the time when she who is in labor bears a son,

and the rest of his brothers return

to join the Israelites.

4He will stand and shepherd his flock

in the strength of the Lord,

in the majesty of the name of the Lord his God.

And they will live securely, for then his greatness

will reach to the ends of the earth.

5And he will be our peace

when the Assyrians invade our land

and march through our fortresses.

We will raise against them seven shepherds,

even eight commanders,

6who will rule5:6 Or crush the land of Assyria with the sword,

the land of Nimrod with drawn sword.5:6 Or Nimrod in its gates

He will deliver us from the Assyrians

when they invade our land

and march across our borders.

7The remnant of Jacob will be

in the midst of many peoples

like dew from the Lord,

like showers on the grass,

which do not wait for anyone

or depend on man.

8The remnant of Jacob will be among the nations,

in the midst of many peoples,

like a lion among the beasts of the forest,

like a young lion among flocks of sheep,

which mauls and mangles as it goes,

and no one can rescue.

9Your hand will be lifted up in triumph over your enemies,

and all your foes will be destroyed.

10“In that day,” declares the Lord,

“I will destroy your horses from among you

and demolish your chariots.

11I will destroy the cities of your land

and tear down all your strongholds.

12I will destroy your witchcraft

and you will no longer cast spells.

13I will destroy your idols

and your sacred stones from among you;

you will no longer bow down

to the work of your hands.

14I will uproot from among you your Asherah poles5:14 That is, wooden symbols of the goddess Asherah

when I demolish your cities.

15I will take vengeance in anger and wrath

on the nations that have not obeyed me.”