Mtawala Aliyeahidiwa Kutoka Bethlehemu
15:1 Ay 16:10; Mt 27:30; Mao 3:30Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi,
kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu.
Watampiga mtawala wa Israeli
shavuni kwa fimbo.
25:2 Yn 7:42; Mwa 35:19; 48:7; 1Sam 13:14; Hes 24:19; 2Sam 6:21; 2Nya 7:18; Za 90:2; 132:6; 102:25; Isa 9:6; Mit 8:22; Yn 1:1; Mt 2:6“Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi,
ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda,
kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu
yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,
ambaye asili yake ni kutoka zamani,
kutoka milele.”
35:3 Yer 7:29Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati
mwanamke aliye na utungu atakapozaa
na ndugu zake wengine warudi
kujiunga na Waisraeli.
45:4 Isa 40:11; 49:9; 52:13; Za 72:8; Zek 9:10; Mik 7:14; Eze 34:11-15; Lk 1:32Atasimama na kulichunga kundi lake
katika nguvu ya Bwana,
katika utukufu wa jina la Bwana Mungu wake.
Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo
ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.
55:5 Isa 8:7; 9:6; 10:24-27; Lk 2:14; Efe 2:14; Kol 1:19-20Naye atakuwa amani yao.
Ukombozi Na Uharibifu
Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu
na kupita katika ngome zetu,
tutawainua wachungaji saba dhidi yake,
hata viongozi wanane wa watu.
65:6 Mwa 10:8; Sef 2:13; Lk 1:71; Nah 2:11-13Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga,
nchi ya Nimrodi kwa upanga.
Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru
atakapoivamia nchi yetu
na kuingia katika mipaka yetu.
75:7 Amo 5:15; Mik 2:12; Isa 44:4; Za 110:3; 133:3Mabaki ya Yakobo yatakuwa
katikati ya mataifa mengi
kama umande kutoka kwa Bwana,
kama manyunyu juu ya majani,
ambayo hayamngoji mtu
wala kukawia kwa mwanadamu.
85:8 Mwa 49:9; Mik 4:13; Zek 10:5; Isa 5:29; Za 50:22; Hos 5:14Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa,
katikati ya mataifa mengi,
kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni,
kama mwana simba miongoni
mwa makundi ya kondoo,
ambaye anaumiza vibaya na kuwararua
kila anapopita katikati yao,
wala hakuna awezaye kuokoa.
95:9 Za 10:12Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako,
nao adui zako wote wataangamizwa.
105:10 Kut 15:4, 19; Hos 14:3; Hag 2:22; Zek 9:10“Katika siku ile,” asema Bwana,
“nitaangamiza farasi zenu katikati yenu
na kubomoa magari yenu ya vita.
115:11 Kum 29:23; Isa 6:11; Mao 2:2; Hos 10:14; Amo 5:9Nitaiangamiza miji ya nchi yenu
na kuziangusha chini ngome zenu zote.
125:12 Kum 18:10-12; Isa 8:19; 2:9Nitaangamiza uchawi wenu
na hamtapiga tena ramli.
135:13 Nah 1:14; Hos 2:10; Isa 2:8; 2:18; Eze 6:9; Zek 13:2Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga
na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu;
hamtasujudia tena
kazi ya mikono yenu.
145:14 Kut 34:13; Amu 3:7; 2Fal 17:10Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu
na kubomoa miji yenu.
155:15 Isa 65:12Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu
juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”
A Promised Ruler From Bethlehem
5:0 In Hebrew texts 5:1 is numbered 4:14, and 5:2-15 is numbered 5:1-14. 1Marshal your troops now, city of troops,
for a siege is laid against us.
They will strike Israel’s ruler
on the cheek with a rod.
2“But you, Bethlehem Ephrathah,
though you are small among the clans5:2 Or rulers of Judah,
out of you will come for me
one who will be ruler over Israel,
whose origins are from of old,
from ancient times.”
3Therefore Israel will be abandoned
until the time when she who is in labor bears a son,
and the rest of his brothers return
to join the Israelites.
4He will stand and shepherd his flock
in the strength of the Lord,
in the majesty of the name of the Lord his God.
And they will live securely, for then his greatness
will reach to the ends of the earth.
5And he will be our peace
when the Assyrians invade our land
and march through our fortresses.
We will raise against them seven shepherds,
even eight commanders,
6who will rule5:6 Or crush the land of Assyria with the sword,
the land of Nimrod with drawn sword.5:6 Or Nimrod in its gates
He will deliver us from the Assyrians
when they invade our land
and march across our borders.
7The remnant of Jacob will be
in the midst of many peoples
like dew from the Lord,
like showers on the grass,
which do not wait for anyone
or depend on man.
8The remnant of Jacob will be among the nations,
in the midst of many peoples,
like a lion among the beasts of the forest,
like a young lion among flocks of sheep,
which mauls and mangles as it goes,
and no one can rescue.
9Your hand will be lifted up in triumph over your enemies,
and all your foes will be destroyed.
10“In that day,” declares the Lord,
“I will destroy your horses from among you
and demolish your chariots.
11I will destroy the cities of your land
and tear down all your strongholds.
12I will destroy your witchcraft
and you will no longer cast spells.
13I will destroy your idols
and your sacred stones from among you;
you will no longer bow down
to the work of your hands.
14I will uproot from among you your Asherah poles5:14 That is, wooden symbols of the goddess Asherah
when I demolish your cities.
15I will take vengeance in anger and wrath
on the nations that have not obeyed me.”