Mika 4 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 4:1-13

Mlima Wa Bwana

(Isaya 2:2-4)

14:1 Za 48:1; 86:9; Zek 8:3; Isa 2:2; Dan 2:35; 2:44; Eze 17:22; Yer 3:17; 31:12Katika siku za mwisho

mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa

kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote;

utainuliwa juu ya vilima,

na watu wa mataifa watamiminika humo.

24:2 Yer 31:6; Yn 6:45; Eze 20:40; Zek 2:11; 14:16; Isa 54:13; Za 25:8-9; 119:171Mataifa mengi yatakuja na kusema,

“Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana,

kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.

Atatufundisha njia zake,

ili tuweze kuenenda katika mapito yake.”

Sheria itatoka Sayuni,

neno la Bwana litatoka Yerusalemu.

34:3 Isa 2:4; 11:4; Yoe 3:10; Hos 2:18; Za 72:7; Zek 8:20-22; 9:10; Za 46:9Atahukumu kati ya mataifa mengi,

na ataamua migogoro ya mataifa

yenye nguvu na yaliyo mbali.

Watafua panga zao ziwe majembe,

na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi.

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine,

wala hawatajifunza vita tena.

44:4 1Fal 4:25; Law 26:6; Eze 39:26; Isa 1:20; 36:16; Yer 31:10; Zek 3:10Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake

na chini ya mtini wake,

wala hakuna mtu atakayewaogopesha,

kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.

54:5 2Fal 17:29; Mdo 14:16; Yos 24:14-15; Isa 26:8; Yer 2:11; Zek 10:12Mataifa yote yanaweza kutembea

katika jina la miungu yao;

sisi tutatembea katika jina la Bwana

Mungu wetu milele na milele.

Mpango Wa Bwana

64:6 Yer 31:8; Isa 56:8; Za 147:2; 106:47; Eze 34:13, 16; 37:21; Sef 3:19“Katika siku hiyo,” asema Bwana,

“nitawakusanya walemavu;

nitawakusanya walio uhamishoni

na wale niliowahuzunisha.

74:7 Yoe 2:32; Mik 2:12; Isa 9:6; Mwa 12:2; Dan 2:44; 7:14; Ufu 11:15; Lk 1:33Nitawafanya walemavu kuwa mabaki,

wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu.

Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni

kuanzia siku hiyo na hata milele.

84:8 Isa 1:26; Zek 9:9Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi,

ee ngome ya Binti Sayuni,

milki ya awali itarudishwa kwako,

ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”

94:9 Yer 8:19; 30:6; 48:41; Mwa 3:16Kwa nini sasa unalia kwa nguvu:

kwani huna mfalme?

Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate

kama ya mwanamke

aliye na utungu wa kuzaa?

104:10 Kum 21:10; 2Fal 20:18; Isa 43:14; 48:20Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni,

kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa,

kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji

ukapige kambi uwanjani.

Utakwenda Babeli;

huko utaokolewa.

Huko Bwana atakukomboa

kutoka mikononi mwa adui zako.

114:11 Mao 2:16; Oba 1:12; Mik 7:8Lakini sasa mataifa mengi

yamekusanyika dhidi yako.

Wanasema, “Mwache anajisiwe,

macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”

124:12 Mwa 50:20; Isa 55:8; Rum 11:33-34Lakini hawayajui

mawazo ya Bwana;

hawauelewi mpango wake,

yeye awakusanyaye kama miganda

kwenye sakafu ya kupuria.

134:13 Isa 21:10; 23:18; 45:1; Ufu 21:24; Dan 2:44“Inuka upure, ee Binti Sayuni,

kwa kuwa nitakupa pembe za chuma;

nitakupa kwato za shaba

na utavunja vipande vipande mataifa mengi.”

Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana,

utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.

New International Reader’s Version

Micah 4:1-13

People From Many Nations Will Worship at the Lord’s Mountain

1In the last days

the mountain where the Lord’s temple is located will be famous.

It will be the highest mountain of all.

It will be lifted up above the hills.

And nations will go to it.

2People from many nations will go there. They will say,

“Come, let us go up to the Lord’s mountain.

Let’s go to the temple of Jacob’s God.

He will teach us how we should live.

Then we will live the way he wants us to.”

The law of the Lord will be taught at Zion.

His message will go out from Jerusalem.

3He will judge between people from many nations.

He’ll settle problems among strong nations everywhere.

They will hammer their swords into plows.

They’ll hammer their spears into pruning tools.

Nations will not go to war against one another.

They won’t even train to fight anymore.

4Everyone will have

their own vine and fig tree.

And no one will make them afraid.

That’s what the Lord who rules over all has promised.

5Other nations worship and trust in their gods.

But we will worship and obey the Lord.

He will be our God for ever and ever.

The Lord’s Plan

6“The time is coming

when I will gather those who are disabled,”

announces the Lord.

“I will bring together those

who were taken away as prisoners.

I will gather those I have allowed to suffer.

7I will make the disabled my faithful people.

I will make into a strong nation those driven away from their homes.

I will rule over them on Mount Zion.

I will be their King from that time on and forever.

8Jerusalem, you used to be

like a guard tower for my flock.

City of Zion, you used to be

a place of safety for my people.

The glorious kingdom you had before

will be given back to you.

Once again a king will rule over your people.”

9Why are you crying out so loudly now?

Don’t you have a king?

Has your ruler died?

Is that why pain comes on you

like the pain of a woman having a baby?

10People of Zion, groan with pain.

Cry out like a woman having a baby.

Soon you must leave your city.

You must camp in the open fields.

You will have to go to the land of Babylon.

But that’s where the Lord will save you.

There he will set you free

from the power of your enemies.

11But now many nations

have gathered together to attack you.

They say, “Let Jerusalem be made ‘unclean.’

We want to laugh when Zion suffers!”

12But those nations don’t know

what the Lord has in mind.

They don’t understand his plan.

He has planned to gather them up like bundles of grain.

He has planned to take them to his threshing floor.

13The Lord says,

“People of Zion, get up

and crush your enemies.

I will make you like a threshing ox.

I will give you iron horns and bronze hooves.

So you will crush many nations.”

They got their money in the wrong way.

But you will set it apart to the Lord.

You will give their wealth

to the Lord of the whole earth.