Mika 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 1:1-16

11:1 Yer 26:18; 2Pet 1:21; 1Nya 3:12-13; Hos 1:1; Isa 1:1Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.

21:2 Kum 4:26; 32:1; Yer 6:19; Mwa 31:50; Za 11:4; Isa 1:2Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote,

sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake,

ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu,

Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.

Hukumu Dhidi Ya Samaria Na Yerusalemu

31:3 Isa 18:4; 64:1; 26:21; Eze 3:12; Ebr 12:18, 19; Amo 4:13Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake;

anashuka na kukanyaga

mahali palipoinuka juu pa dunia.

41:4 Za 46:2-6; Hes 16:31; Nah 1:5Milima inayeyuka chini yake

na mabonde yanagawanyika

kama nta mbele ya moto,

kama maji yatiririkayo kasi

kwenye mteremko.

51:5 Amo 8:14; Hos 5:5; Yer 2:18-19Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo,

ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli.

Kosa la Yakobo ni lipi?

Je, sio Samaria?

Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini?

Je, sio Yerusalemu?

61:6 Kum 20:6; Amo 5:11“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto,

mahali pa kuotesha mizabibu.

Nitayamwaga mawe yake katika bonde

na kuacha wazi misingi yake.

71:7 Eze 6:6; Kut 32:20; Kum 9:21; 23:17-18Sanamu zake zote

zitavunjwa vipande vipande;

zawadi zake zote za Hekalu

zitachomwa kwa moto;

nitaharibu vinyago vyake vyote.

Kwa kuwa alikusanya zawadi zake

kutokana na ujira wa kahaba,

nazo zitatumika tena

kulipa mishahara ya kahaba.”

Kulia Na Kuomboleza

81:8 Isa 15:3; 20:2Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza;

nitatembea bila viatu na tena uchi.

Nitabweka kama mbweha

na kuomboleza kama bundi.

91:9 Yer 46:11; 10:19; 2Fal 18:13; Isa 3:26Kwa sababu jeraha lake halitibiki;

limekuja Yuda.

Limefika hasa kwenye lango la watu wangu,

hata Yerusalemu kwenyewe.

10Usiliseme hili huko Gathi;

usilie hata kidogo.

Huko Beth-le-Afra

gaagaa mavumbini.

111:11 Eze 23:29Piteni mkiwa uchi na wenye aibu,

ninyi mkaao Shafiri.

Wale waishio Saanani

hawatatoka nje.

Beth-Eseli iko katika maombolezo;

kinga yake imeondolewa kwako.

121:12 Yer 14:19; 40:2Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu

wakingoja msaada,

kwa sababu maangamizi yamekuja

kutoka kwa Bwana,

hata katika lango la Yerusalemu.

131:13 Yos 10:3; Za 9:14Enyi mkaao Lakishi,

fungeni farasi kwenye magari ya vita.

Mlikuwa chanzo cha dhambi

kwa Binti Sayuni,

kwa kuwa makosa ya Israeli

yalikutwa kwako.

141:14 2Fal 16:8; Yos 15:44; Yer 15:18Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi

zawadi za kuagana.

Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu

kwa wafalme wa Israeli.

151:15 Yos 15:44; 12:15Nitawaleteeni atakayewashinda

ninyi mnaoishi Maresha.

Yeye aliye utukufu wa Israeli

atakuja Adulamu.

161:16 Law 13:40; Ay 1:20; 2Fal 18:13; Amo 5:27; Kum 4:27Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza

kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia;

jifanyieni upara kama tai,

kwa kuwa watawaacha

na kwenda uhamishoni.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

彌迦書 1:1-16

1猶大約坦亞哈斯希西迦執政期間,耶和華把祂的話傳給了摩利沙彌迦。他看到了有關撒瑪利亞耶路撒冷的異象。

審判將臨

2萬民啊,

你們都要聽!

大地和地上的萬物啊,

你們要側耳傾聽!

主耶和華從祂的聖殿裡作證指控你們。

3看啊,耶和華離開祂的居所,

從天降臨,

腳踏大地的高處。

4群山在祂腳下熔化,

猶如火中的蠟;

山谷崩裂,

岩石如水沿山坡傾瀉。

5這一切都是因為雅各的叛逆,

以色列家的罪惡。

雅各的叛逆在哪裡呢?

豈不是在撒瑪利亞嗎?

猶大的邱壇在哪裡呢?

豈不是在耶路撒冷嗎?

6「所以,我耶和華要使撒瑪利亞淪為荒野的廢墟,

成為種葡萄的地方。

我要把她的石頭拋進山谷,

直到露出她的根基。

7她所有的神像都要被打碎,

她所得的淫資都要化為灰燼;

我要毀滅她的一切偶像。

她以淫資得來的偶像,

也要被用作妓女的淫資。」

先知的哀傷

8為此,我要痛哭哀號,

我要赤身光腳而行,

像豺狼哀嚎,

如鴕鳥悲鳴。

9因為撒瑪利亞的創傷無法救治,

已經禍及猶大

直逼我百姓的城門,直逼耶路撒冷

10不要在迦特宣揚,

也不要哭泣,

要在伯·亞弗拉的灰塵中打滾。

11沙斐的居民啊,

你們將赤身露體,

被羞辱地擄去。

撒南的居民不敢出城,

伯·以薛在痛哭,

你們已失去它的庇護。

12瑪律的居民痛苦不堪,

渴望得到拯救,

因為耶和華已把災難降到耶路撒冷的城門。

13拉吉的居民啊,

用駿馬套車逃命吧!

是你們首先唆使錫安城犯罪,

在你們身上看到了以色列的罪惡。

14去向摩利設·迦特贈送告別禮物吧!

亞革悉人必令以色列諸王受騙上當。

15瑪利沙的居民啊,

我要使征服者到你們那裡。

以色列的領袖1·15 以色列的領袖」希伯來文是「以色列的榮耀」。要躲到亞杜蘭

16猶大人啊,你們要剃光頭髮,

為你們所愛的兒女悲傷;

要剃得如禿鷹一樣光禿,

因為他們要被擄到遠方。