Mhubiri 9 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 9:1-18

Hatima Ya Wote

19:1 Mhu 8:14; 10:14; Kum 33:3; Ay 12:10Kwa hiyo niliyatafakari yote haya nikafikia uamuzi kwamba waadilifu na wenye hekima na yale wanayoyafanya yako mikononi mwa Mungu, lakini hakuna mtu ajuaye kama anangojewa na upendo au chuki. 29:2 Ay 9:22; Mhu 2:14; 6:6Wote wanayo hatima inayofanana, mwadilifu na mwovu, mwema na mbaya, aliye safi na aliye najisi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa.

Kama ilivyo kwa mtu mwema,

ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye dhambi;

kama ilivyo kwa wale wanaoapa,

ndivyo ilivyo kwa wale wasioapa.

39:3 Mhu 2:14; Yer 11:8; 17:9; Ay 21:26; 9:22; Yer 13:10; 16:12Huu ni ubaya ulio katika kila kitu kinachotendeka chini ya jua: Mwisho unaofanana huwapata wote. Zaidi ya hayo, mioyo ya watu, imejaa ubaya na kuna wazimu mioyoni mwao wangali hai, hatimaye huungana na waliokufa. 4Yeyote aliye miongoni mwa walio hai analo tumaini, hata mbwa hai ni bora kuliko simba aliyekufa!

59:5 Ay 14:21; Mhu 2:16; Za 9:6; Isa 26:14; 63:16Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa,

lakini wafu hawajui chochote,

hawana tuzo zaidi,

hata kumbukumbu yao imesahaulika.

69:6 Ay 21:21Upendo wao, chuki yao na wivu wao

vimetoweka tangu kitambo,

kamwe hawatakuwa tena na sehemu

katika lolote linalotendeka chini ya jua.

79:7 Mhu 2:24; 8:15; Hes 6:20Nenda, kula chakula chako kwa furaha, unywe divai yako kwa moyo wa shangwe, kwa maana sasa Mungu anakubali unachofanya. 89:8 Za 23:5; Ufu 3:4Daima uvae nguo nyeupe na daima upake kichwa chako mafuta. 99:9 Mit 5:18; Ay 31:2Furahia maisha na mke wako, umpendaye, siku zote za maisha ya ubatili uliyopewa na Mungu chini ya jua, siku zote za ubatili. Kwa maana hili ndilo fungu lako katika maisha na katika kazi yako ya taabu chini ya jua. 109:10 Isa 38:18; 1Sam 10:7; Rum 12:11; Za 6:5; Mhu 2:24; 11:6; Hes 16:33Lolote mkono wako upatalo kufanya, fanya kwa nguvu zako zote, kwa kuwa huko kuzimu, unakokwenda, hakuna kufanya kazi wala mipango wala maarifa wala hekima.

119:11 Amo 2:14-15; Yer 9:23; Kum 8:18; Ay 32:13; Isa 47:10; Mhu 2:14Nimeona kitu kingine tena chini ya jua:

Si wenye mbio washindao mashindano

au wenye nguvu washindao vita,

wala si wenye hekima wapatao chakula

au wenye akili nyingi wapatao mali,

wala wenye elimu wapatao upendeleo,

lakini fursa huwapata wote.

129:12 Mit 29:6; Za 73:22; Mhu 8:7; 2:14Zaidi ya hayo, hakuna mwanadamu ajuaye wakati saa yake itakapokuja:

Kama vile samaki wavuliwavyo katika wavu mkatili,

au ndege wanaswavyo kwenye mtego,

vivyo hivyo wanadamu hunaswa na nyakati mbaya

zinazowaangukia bila kutazamia.

Hekima Ni Bora Kuliko Upumbavu

139:13 2Sam 20:16-22Pia niliona chini ya jua mfano huu wa hekima ambao ulinivutia sana: 14Palikuwa na mji mdogo uliokuwa na watu wachache ndani yake. Mfalme mwenye nguvu akainuka dhidi yake, akauzunguka akaweka jeshi kubwa dhidi yake. 159:15 Mwa 40:14; Mhu 1:11; 2:16Katika mji huo kulikuwepo mtu mmoja maskini lakini mwenye hekima, naye akauokoa ule mji kwa hekima yake. Lakini hakuna aliyemkumbuka yule maskini. 169:16 Mhu 7:19; Mit 21:22; Es 6:3Kwa hiyo, nikasema, “Hekima ni bora kuliko nguvu.” Lakini hekima ya maskini imedharauliwa, wala hakuna anayesikiliza maneno yake.

179:17 2Sam 20:17; Dan 5:10Maneno ya utulivu ya mwenye hekima

husikiwa kuliko makelele ya mtawala wa wapumbavu.

189:18 Mhu 2:13; Rum 6:12, 16-23Hekima ni bora kuliko silaha za vita,

lakini mwenye dhambi mmoja

huharibu mema mengi.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

傳道書 9:1-18

1我仔細思想、探究這些事,就知道義人、智者及他們的行事為人都由上帝掌管,人無法知道前面等待自己的是愛還是恨。 2義人和惡人、好人和壞人、潔淨的和污穢的、獻祭的和不獻祭的、行善的和犯罪的、敢於起誓的和不敢起誓的人,最終的命運都一樣。 3在日光之下有一件可悲的事,就是人最終的命運都一樣。再者,人內心都充滿邪惡,活著的時候行事狂妄,最後都步入死亡。 4有生命就有希望,一條活狗總比一頭死獅子強。 5因為活著的人還知道自己終有一死,但死了的人什麼都不知道,再也得不到任何賞賜,他們被忘得一乾二淨。 6他們的愛、恨和嫉妒早已不復存在,他們再也無法參與日光之下的事。

7去歡歡喜喜、快快樂樂地吃喝吧!因為上帝已經悅納你所做的。 8你的衣服要經常保持潔白,頭上也不要缺少膏油。 9在你虛空的人生中,就是在上帝所賜、日光之下虛空的歲月裡,你要與愛妻快樂度日,因為這是你一生在日光之下的勞碌中所當得的。 10凡你的手能做的,都要盡力去做,因為在你要去的陰間沒有工作,沒有計劃,也沒有知識和智慧。 11我又發現,日光之下,跑得快的未必能得獎,強大的未必能得勝,智者未必得溫飽,聰明人未必有財富,博學者未必受愛戴,因為時機和境遇左右眾人。 12再者,人無法知道何時大難臨頭。禍患突然臨到時,人根本無法擺脫,就像魚落入險惡的網中,又像鳥兒陷入網羅。 13我看見日光之下有一種智慧,對我來說意義深遠。 14有一個勢力強大的君王來攻擊一個人口不多的小城,他建造營壘圍困這城。 15這城裡有一個貧窮的智者,他用智慧拯救了這城,但事後人們卻把他遺忘了。 16我認為智慧勝過武力,然而那位窮人的智慧卻被輕視,他所說的話也無人理會。 17智者的細語勝過官長在愚人中的喊叫。 18智慧勝過兵器,但一個罪人卻能破壞許多善事。