Mhubiri 6 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 6:1-12

1Nimeona ubaya mwingine chini ya jua, nao unalemea sana wanadamu: 26:2 Kum 8:7-10; Za 17:14; Amu 18:10; Mhu 5:13-19Mungu humpa mwanadamu utajiri, mali na heshima, hivyo hakukosa chochote moyo wake unachokitamani. Lakini Mungu hamwezeshi kuvifurahia, badala yake mgeni ndiye anayevifurahia. Hili ni ubatili, ni ubaya unaosikitisha.

36:3 Ay 3:3, 16; Es 7:10; Mhu 4:3Mtu anaweza kuwa na watoto mia moja naye akaishi miaka mingi, lakini haidhuru kuwa ataishi muda mrefu kiasi gani, kama hawezi kufurahia mafanikio yake na kwamba hapati mazishi ya heshima, ninasema afadhali mtoto aliyezaliwa akiwa amekufa kuliko yeye. 4Kuzaliwa kwake hakuna maana, huondokea gizani na gizani jina lake hufunikwa. 5Ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye ana pumziko zaidi kuliko mtu huyo, 66:6 Mhu 2:16Hata kama huyo mtu ataishi miaka elfu mara mbili na zaidi, lakini akashindwa kufurahia mafanikio yake, je, wote hawaendi sehemu moja?

76:7 Mit 16:26; 27:20; 1Tim 6:6-8Juhudi zote za binadamu ni kwa ajili ya kinywa chake,

hata hivyo hamu yake kamwe haitoshelezwi.

86:8 Mhu 2:15Mtu mwenye hekima ana faida gani

zaidi ya mpumbavu?

Mtu maskini anapata faida gani

kwa kujua jinsi ya kujistahi

mbele ya watu wengine?

9Ni bora kile ambacho jicho linakiona

kuliko hamu isiyotoshelezwa.

Hili nalo ni ubatili,

ni kukimbiza upepo.

106:10 Ay 9:32; Isa 45:9; Mhu 3:15Lolote lililopo limekwisha kupewa jina,

naye mwanadamu alivyo ameshajulikana;

hakuna mtu awezaye kushindana

na mwenye nguvu kuliko yeye.

11Maneno yanavyokuwa mengi,

ndivyo yanavyokosa maana,

Je, hilo linamfaidia vipi yeyote?

126:12 Yak 4:14; Ay 10:20; 20:8; 14:2; 1Nya 29:15; Za 39:6Kwa maana ni nani anayejua lililo jema kwa ajili ya maisha ya mwanadamu, katika siku chache na za ubatili anazopita kama kivuli? Ni nani awezaye kumwambia yatakayotokea chini ya jua baada ya yeye kuondoka?

New International Version – UK

Ecclesiastes 6:1-12

1I have seen another evil under the sun, and it weighs heavily on mankind: 2God gives some people wealth, possessions and honour, so that they lack nothing their hearts desire, but God does not grant them the ability to enjoy them, and strangers enjoy them instead. This is meaningless, a grievous evil.

3A man may have a hundred children and live many years; yet no matter how long he lives, if he cannot enjoy his prosperity and does not receive proper burial, I say that a stillborn child is better off than he. 4It comes without meaning, it departs in darkness, and in darkness its name is shrouded. 5Though it never saw the sun or knew anything, it has more rest than does that man – 6even if he lives a thousand years twice over but fails to enjoy his prosperity. Do not all go to the same place?

7Everyone’s toil is for their mouth,

yet their appetite is never satisfied.

8What advantage have the wise over fools?

What do the poor gain

by knowing how to conduct themselves before others?

9Better what the eye sees

than the roving of the appetite.

This too is meaningless,

a chasing after the wind.

10Whatever exists has already been named,

and what humanity is has been known;

no-one can contend

with someone who is stronger.

11The more the words,

the less the meaning,

and how does that profit anyone?

12For who knows what is good for a person in life, during the few and meaningless days they pass through like a shadow? Who can tell them what will happen under the sun after they are gone?