Mhubiri 5 – NEN & TNCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 5:1-20

Simama Katika Kicho Cha Mungu

15:1 Za 89:7; Kut 3:5; Hos 6:6Linda hatua zako uendapo katika nyumba ya Mungu. Karibia usikilize kuliko kutoa dhabihu ya wapumbavu, ambao hawajui kuwa wanafanya kosa.

25:2 Amu 11:35; Ay 6:24; Mit 10:19; 20:25Usiwe mwepesi kuzungumza,

usiwe na haraka katika moyo wako

kuzungumza lolote mbele za Mungu.

Mungu yuko mbinguni

nawe uko duniani,

kwa hiyo maneno yako

na yawe machache.

35:3 Ay 20:8; Mhu 10:14Kama vile ndoto huja

wakati kuna shughuli nyingi,

ndivyo yalivyo mazungumzo ya mpumbavu

wakati kuna maneno mengi.

45:4 Mwa 28:20; Kum 23:21; Hes 30:2; Za 76:11; 119:60; Amu 11:35Wakati unapomwekea Mungu nadhiri, usikawie kuitimiza. Yeye hafurahii wapumbavu; timiza nadhiri yako. 55:5 Yon 2:9; Mdo 5:4; Hes 30:2-4Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuiweka na usiitimize. 6Usiruhusu kinywa chako kukuingiza dhambini. Tena usijitetee mbele ya huyo mjumbe wa hekaluni, ukisema, “Niliweka nadhiri kwa makosa.” Kwa nini Mungu akasirike kwa ajili ya yale unayosema na kuiharibu kazi ya mikono yako? 75:7 Kum 10:12; Mhu 3:14; 12:13Kuota ndoto kwingi na maneno mengi ni ubatili. Kwa hiyo simama katika kicho cha Mungu.

Utajiri Ni Ubatili

85:8 Mhu 3:16; 4:1; Za 12:5Kama ukiona maskini wanaonewa katika nchi, hukumu na haki vikipotoshwa, usishangazwe na mambo hayo, kwa maana afisa mmoja anaangaliwa na aliye juu yake zaidi na juu ya hao wawili kuna wengine walio juu zaidi yao. 9Mafanikio ya nchi ni kwa ajili ya wote, hata mfalme mwenyewe hufaidi kutoka mashambani.

10Yeyote apendaye fedha kamwe

hatosheki na fedha;

yeyote apendaye utajiri kamwe

hatosheki na kipato chake.

Hili nalo pia ni ubatili.

11Mali ikiongezeka, ndivyo walaji

wanavyoongezeka.

Hii nayo inamfaidia nini mwenye mali

isipokuwa ni kushibisha macho yake?

125:12 Ay 20:20Usingizi wa kibarua ni mtamu,

awe amekula kidogo au kingi,

lakini wingi wa mali

humnyima tajiri usingizi.

135:13 Mhu 6:1-2Nimeshaona uovu mzito chini ya jua:

Utajiri uliolimbikizwa kwa kujinyima

na kuleta madhara kwa mwenye mali,

14au utajiri uliopotea kwa bahati mbaya,

hivyo kwamba wakati akiwa na mwana

hakuna chochote kilichobaki kwa ajili yake.

155:15 Za 49:17; 1Tim 6:7; Ay 1:21; Mhu 1:3Mtu hutoka tumboni mwa mama yake uchi,

naye jinsi alivyokuja vivyo hivyo huondoka.

Hachukui chochote kutokana na kazi yake

ambacho anaweza kukibeba mkononi mwake.

165:16 Mit 11:29; Mhu 1:3Hili nalo ni baya la kusikitisha:

Kama vile mtu ajavyo, vivyo hivyo huondoka,

naye anapata faida gani,

maadamu hutaabika kwa ajili ya upepo?

17Siku zake zote hula gizani,

pamoja na fadhaa kubwa,

mateso na hasira.

185:18 Mhu 2:3, 10, 14, 24Ndipo nikatambua kwamba ni vyema na sahihi kwa mtu kula na kunywa na kutosheka katika kazi yake ngumu chini ya jua katika siku chache za maisha yake Mungu alizompa, kwa maana hili ndilo fungu lake. 195:19 1Nya 29:12; 2Nya 1:12; Ay 31:2; Mhu 2:24; 6:2Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu yeyote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu. 205:20 Kum 12:7, 18; Kut 23:25Mara chache mtu huzifikiri siku za maisha yake, kwa sababu Mungu humfanya ashikwe na furaha ya moyoni.

Thai New Contemporary Bible

ปัญญาจารย์ 5:1-20

จงยำเกรงพระเจ้า

1จงระมัดระวังแต่ละย่างก้าวเมื่อท่านไปยังพระนิเวศของพระเจ้า เข้าไปฟังใกล้ๆ ก็ดีกว่าถวายเครื่องบูชาแบบคนโง่ ซึ่งไม่รู้ว่าตัวเองทำผิด

2อย่าปากไว

อย่าใจร้อนผลีผลาม

พลั้งปากพล่อยๆ ต่อหน้าพระเจ้า

พระเจ้าประทับในฟ้าสวรรค์

ส่วนท่านอยู่บนโลก

ฉะนั้นจงพูดแต่น้อยคำ

3ห่วงกังวลมากก็ฝันมาก

ยิ่งพูดมากก็ยิ่งพูดโง่ๆ

4เมื่อถวายปฏิญาณต่อพระเจ้าแล้ว จงรีบทำให้ครบถ้วน พระเจ้าไม่พอพระทัยคนโง่ จงทำตามที่ปฏิญาณไว้ 5ไม่ปฏิญาณยังดีกว่าปฏิญาณแล้วไม่ทำให้ครบถ้วน 6อย่าให้ปากพาตัวหลงทำบาป และอย่าแก้ตัวกับผู้สื่อสารของพระเจ้าว่า “ข้าพเจ้าเผลอปฏิญาณไป” จะให้พระเจ้าทรงพระพิโรธวาจาของท่านและทำลายกิจการจากน้ำมือของท่านทำไมเล่า? 7ฝันมากและพูดมากก็อนิจจัง ดังนั้นจงยำเกรงพระเจ้าเถิด

ความร่ำรวยก็อนิจจัง

8หากท่านเห็นคนจนในเมืองถูกข่มเหงรังแกและเห็นความยุติธรรมและสิทธิถูกละเลยในที่ใดก็ตาม อย่าฉงนสนเท่ห์เลย เพราะเจ้าหน้าที่ทุกคนอยู่ใต้บังคับบัญชาของผู้ที่อยู่เหนือเขาและเหนือกว่านั้นขึ้นไปก็ยังมีผู้บังคับบัญชาสูงขึ้นไปอีก 9ทุกคนฉวยเอาผลิตผลจากแผ่นดิน กษัตริย์เองทรงได้ประโยชน์จากเรือกสวนไร่นา

10ผู้รักเงินย่อมไม่อิ่มด้วยเงิน

ผู้รักสมบัติไม่เคยอิ่มด้วยรายได้

นี่ก็อนิจจัง

11เมื่อมีข้าวของเพิ่มขึ้น

ก็เพิ่มคนบริโภค

คนที่เป็นเจ้าของจะได้ประโยชน์อะไร

นอกจากชมเล่นเป็นขวัญตา?

12กรรมกรนอนหลับสบาย

ไม่ว่าเขาได้กินมากหรือกินน้อย

แต่ข้าวของเหลือเฟือของคนรวย

ไม่ช่วยให้เขาหลับได้

13ข้าพเจ้าได้เห็นความเลวร้ายที่น่าสลดใจภายใต้ดวงอาทิตย์คือ

ทรัพย์สมบัติที่สะสมไว้จนเป็นภัยอันตรายแก่เจ้าของ

14หรือทรัพย์สมบัติสูญสิ้นไปเนื่องจากเคราะห์กรรมบางอย่าง

จนไม่มีอะไรเหลือตกทอดให้ลูกหลาน

15คนเราเกิดมาจากท้องแม่ตัวเปล่าอย่างไรก็จะจากไปอย่างนั้น

เขาไม่อาจหยิบฉวยผลงานจากการตรากตรำติดมือไปได้เลย

16นี่ก็เป็นความเลวร้ายที่น่าสลดใจด้วย

คือคนเรามาอย่างไรก็จากไปอย่างนั้น

แล้วเขาได้ประโยชน์อะไรเล่า

ในเมื่อเขาตรากตรำไปอย่างลมๆ แล้งๆ?

17ตลอดชีวิตของเขา เขากินอยู่ในความมืดมน

เต็มไปด้วยความสับสนวุ่นวาย ความทุกข์ทรมานและความโกรธเคืองอย่างมาก

18แล้วข้าพเจ้าจึงตระหนักว่าดีแล้ว เหมาะสมแล้ว ที่มนุษย์จะกินดื่ม และหาความอิ่มใจในการตรากตรำทำงานภายใต้ดวงอาทิตย์ตลอดชั่วชีวิตสั้นๆ ซึ่งพระเจ้าประทานให้ เพราะนี่เป็นส่วนของเขา 19ยิ่งกว่านั้น เมื่อพระเจ้าประทานทรัพย์สมบัติและความมั่งคั่งให้ พระองค์ก็ทรงกระทำให้เขาชื่นชมกับสิ่งเหล่านั้น ให้รับส่วนของตนและเป็นสุขในงานของตนได้ นี่เป็นของขวัญของพระเจ้า 20เขาไม่ต้องหวนคิดถึงวันคืนแห่งชีวิตของตนมากนัก เพราะพระเจ้าทรงให้เขาง่วนอยู่กับความชื่นใจ