Mhubiri 5 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 5:1-20

Simama Katika Kicho Cha Mungu

15:1 Za 89:7; Kut 3:5; Hos 6:6Linda hatua zako uendapo katika nyumba ya Mungu. Karibia usikilize kuliko kutoa dhabihu ya wapumbavu, ambao hawajui kuwa wanafanya kosa.

25:2 Amu 11:35; Ay 6:24; Mit 10:19; 20:25Usiwe mwepesi kuzungumza,

usiwe na haraka katika moyo wako

kuzungumza lolote mbele za Mungu.

Mungu yuko mbinguni

nawe uko duniani,

kwa hiyo maneno yako

na yawe machache.

35:3 Ay 20:8; Mhu 10:14Kama vile ndoto huja

wakati kuna shughuli nyingi,

ndivyo yalivyo mazungumzo ya mpumbavu

wakati kuna maneno mengi.

45:4 Mwa 28:20; Kum 23:21; Hes 30:2; Za 76:11; 119:60; Amu 11:35Wakati unapomwekea Mungu nadhiri, usikawie kuitimiza. Yeye hafurahii wapumbavu; timiza nadhiri yako. 55:5 Yon 2:9; Mdo 5:4; Hes 30:2-4Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuiweka na usiitimize. 6Usiruhusu kinywa chako kukuingiza dhambini. Tena usijitetee mbele ya huyo mjumbe wa hekaluni, ukisema, “Niliweka nadhiri kwa makosa.” Kwa nini Mungu akasirike kwa ajili ya yale unayosema na kuiharibu kazi ya mikono yako? 75:7 Kum 10:12; Mhu 3:14; 12:13Kuota ndoto kwingi na maneno mengi ni ubatili. Kwa hiyo simama katika kicho cha Mungu.

Utajiri Ni Ubatili

85:8 Mhu 3:16; 4:1; Za 12:5Kama ukiona maskini wanaonewa katika nchi, hukumu na haki vikipotoshwa, usishangazwe na mambo hayo, kwa maana afisa mmoja anaangaliwa na aliye juu yake zaidi na juu ya hao wawili kuna wengine walio juu zaidi yao. 9Mafanikio ya nchi ni kwa ajili ya wote, hata mfalme mwenyewe hufaidi kutoka mashambani.

10Yeyote apendaye fedha kamwe

hatosheki na fedha;

yeyote apendaye utajiri kamwe

hatosheki na kipato chake.

Hili nalo pia ni ubatili.

11Mali ikiongezeka, ndivyo walaji

wanavyoongezeka.

Hii nayo inamfaidia nini mwenye mali

isipokuwa ni kushibisha macho yake?

125:12 Ay 20:20Usingizi wa kibarua ni mtamu,

awe amekula kidogo au kingi,

lakini wingi wa mali

humnyima tajiri usingizi.

135:13 Mhu 6:1-2Nimeshaona uovu mzito chini ya jua:

Utajiri uliolimbikizwa kwa kujinyima

na kuleta madhara kwa mwenye mali,

14au utajiri uliopotea kwa bahati mbaya,

hivyo kwamba wakati akiwa na mwana

hakuna chochote kilichobaki kwa ajili yake.

155:15 Za 49:17; 1Tim 6:7; Ay 1:21; Mhu 1:3Mtu hutoka tumboni mwa mama yake uchi,

naye jinsi alivyokuja vivyo hivyo huondoka.

Hachukui chochote kutokana na kazi yake

ambacho anaweza kukibeba mkononi mwake.

165:16 Mit 11:29; Mhu 1:3Hili nalo ni baya la kusikitisha:

Kama vile mtu ajavyo, vivyo hivyo huondoka,

naye anapata faida gani,

maadamu hutaabika kwa ajili ya upepo?

17Siku zake zote hula gizani,

pamoja na fadhaa kubwa,

mateso na hasira.

185:18 Mhu 2:3, 10, 14, 24Ndipo nikatambua kwamba ni vyema na sahihi kwa mtu kula na kunywa na kutosheka katika kazi yake ngumu chini ya jua katika siku chache za maisha yake Mungu alizompa, kwa maana hili ndilo fungu lake. 195:19 1Nya 29:12; 2Nya 1:12; Ay 31:2; Mhu 2:24; 6:2Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu yeyote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu. 205:20 Kum 12:7, 18; Kut 23:25Mara chache mtu huzifikiri siku za maisha yake, kwa sababu Mungu humfanya ashikwe na furaha ya moyoni.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

傳道書 5:1-20

敬畏上帝

1你進入上帝的殿時要小心謹慎,近前傾聽勝過愚人獻祭,因為他們不知道自己是在作惡。 2在上帝面前不要冒失開口,不可急於發言,因為祂在天上,你在地上。所以,你要少言寡語。 3事務繁雜,夜裡多夢;多言多語,顯出愚昧。 4你向上帝許願,不可遲遲不還,因為祂不喜歡這樣的愚人。要還所許的願。 5與其許了願不還,倒不如不許。 6不要在言語上犯罪,也不要在祭司5·6 祭司」希伯來文是「使者」。面前說許錯了願。為什麼用言語惹上帝發怒,以致祂摧毀你手中的工作呢? 7多夢多言都是虛空。你只要敬畏上帝!

財富虛空

8若你在某地看見窮人受欺壓,公平正義被扭曲,不要震驚,因為官上有官,在眾官之上還有更高的官。 9況且,地的出產滋養萬物,就是君王也需要從田地得到供應。 10貪愛錢財的,金銀不能使他滿足;貪圖富裕的,再多的利益也不能叫他稱心。這也是虛空! 11財富增加,消費的人也增加,這對財富的主人有什麼益處呢?只是過眼雲煙罷了! 12勞力的人不管吃多吃少,總是睡得香甜;富人的萬貫家財卻害得他不能成眠。 13我看到日光之下有一件可悲的事:有人積攢財寶,反而害了自己。 14經營不善,便財富盡失,什麼也不能留給兒子。 15人怎樣從母腹空空而來,也必照樣空空而去;勞碌一生,什麼也不能帶走。 16這是多麼可悲啊!人怎樣來,也要怎樣去,為風勞碌有什麼益處呢? 17他一生活在黑暗中,飽受煩惱、病痛和憤怒的困擾。 18我認為人生最美最善的是,在上帝所賜的短暫歲月中盡情吃喝,享受自己在日光之下勞苦得來的成果。因為這是人當得的。 19上帝不單給人財富,也叫他能吃能喝,享用自己所當得的,並在勞碌中得到快樂,這都是上帝的恩賜。 20他不用擔憂自己壽命的長短,因為上帝使他心裡充滿喜樂。