Mhubiri 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 4:1-16

Uonevu, Taabu, Uadui

14:1 Mao 1:16; Mhu 3:16; Za 12:5Nikatazama tena nikaona uonevu wote uliokuwa unafanyika chini ya jua:

Nikaona machozi ya walioonewa,

wala hawana wa kuwafariji;

uwezo ulikuwa upande wa wale wanaowaonea,

wala hawana wa kuwafariji.

24:2 Mhu 2:17; Yer 20:17-18; 22:10; Ay 3:17; 10Nami nikasema kwamba wafu,

waliokwisha kufa,

wana furaha kuliko watu walio hai,

ambao bado wanaishi.

34:3 Mhu 6:3; Mt 24:19; Ay 3:16-22Lakini aliye bora kuliko hao wawili

ni yule ambaye hajazaliwa bado,

ambaye hajaona ule uovu

unaofanyika chini ya jua.

4Tena nikaona kuwa kazi zote na mafanikio yote huchipuka kutokana na wivu wa mtu kwa jirani yake. Hili nalo ni ubatili, ni kukimbiza upepo.

54:5 Mit 6:10Mpumbavu hukunja mikono yake

na kujiangamiza mwenyewe.

64:6 Mit 15:16-17; 16:8Afadhali konzi moja pamoja

na utulivu kuliko konzi mbili pamoja na taabu

na kukimbiza upepo.

7Tena nikaona kitu kingine kilicho ubatili chini ya jua:

84:8 Mit 27:20; Hab 2:5-6; 1Yn 2:16Kulikuwepo mwanadamu aliye peke yake,

hakuwa na mwana wala ndugu.

Hapakuwa na mwisho wa kazi yake,

hata hivyo macho yake

hayakutosheka na utajiri wake.

Aliuliza, “Ninajitaabisha hivi kwa ajili ya nani,

nami kwa nini ninajinyima kufurahia?”

Hili pia ni ubatili,

ni shughuli yenye taabu!

9Wawili ni afadhali kuliko mmoja,

kwa sababu wana malipo mazuri kwa kazi yao:

10Kama mmoja akianguka,

mwenzake atamwinua.

Lakini ni jambo la kuhuzunisha

kwa mtu yule aangukaye

naye hana wa kumwinua!

11Pia, kama wawili wakilala pamoja

watapashana joto.

Lakini ni vipi mtu aweza

kujipasha joto mwenyewe?

12Ingawa mtu mmoja aweza kushindwa,

watu wawili wanaweza

kumkabili adui na kumshinda.

Kamba ya nyuzi tatu

haikatiki kwa urahisi.

Maendeleo Ni Ubatili

13Afadhali kijana maskini mwenye hekima kuliko mfalme mzee mpumbavu ambaye hajui tena kupokea maonyo. 14Kijana huyo angeweza kutokea gerezani akapata ufalme, au angeweza kuwa amezaliwa katika umaskini kwenye huo ufalme. 15Nikaona kwamba wote walioishi na kutembea chini ya jua walimfuata kijana, aliyepokea ufalme. 16Hapakuwa na kikomo cha watu wote aliowatawala. Lakini wale waliokuja baadaye hawakufurahia kazi ya yule aliyepokea ufalme. Hili nalo pia ni ubatili, ni kukimbiza upepo.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

傳道書 4:1-16

1於是,我又觀察日光之下的一切欺壓之事。我看見受欺壓的淚流滿面,無人安慰。因為欺壓者有權有勢,所以無人安慰他們。 2我為那已死的人慶幸,因為他們比活著的人幸福。 3不過,比以上兩種人更幸運的是那從未出生的人,他們從未見過日光之下各樣的惡行。 4我又看見人的一切勞碌和成就原是出於爭強好勝。這也是虛空,如同捕風。 5愚人遊手好閒,最後只能餓死。 6擁有不多,心裡安寧,勝過擁有很多,仍勞碌捕風。 7我又看見日光之下一件虛空的事: 8有一個人孤孤單單,沒有兒子也沒有兄弟,卻終身勞碌。他雖然家道豐裕,仍不滿足,從未想過「我不停地勞碌,放棄一切享受,究竟是為了誰?」這也是虛空,是一種悲哀。 9兩個人總比一個人好,因為二人勞碌同得美好的成果。 10一人跌倒,總有同伴相扶。但孤身一人、跌倒了無人相扶的真悲慘! 11還有,二人同睡會暖和,一人獨睡怎能暖和呢? 12遭遇攻擊,一人獨自不能抵擋,二人並肩就能對付。三股擰成的繩子不容易斷。 13貧窮但有智慧的青年,勝過年老、愚昧、不再納諫的君王。 14雖然這青年在本國出身貧寒,卻能從囚犯成為君王。 15我看見所有日光之下的人都起來擁護這位代替老君王的青年。 16擁護他的人不計其數,以後的世代卻對他不滿。這也是虛空,如同捕風。