Mhubiri 2 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 2:1-26

Anasa Ni Ubatili

12:1 Za 10:6; Lk 12:19; Mhu 7:4; 8:15Nikafikiri moyoni mwangu, “Haya basi, nitakujaribu kwa anasa nione ni lipi lililo jema.” Lakini hilo nalo likaonekana ni ubatili. 22:2 Mit 14:13; Isa 22:12-13; Mhu 7:6Nikasema, “Kicheko nacho ni upumbavu. Nayo matokeo ya anasa ni nini?” 32:3 Amu 9:13; Rut 3:3; Amo 6:3-6; Mhu 3:12-13; 5:18; 8:15Nikajaribu kujifurahisha kwa mvinyo na kukumbatia upumbavu, huku bado akili yangu inaniongoza kwa hekima. Nilitaka kuona ni lipi bora watu wafanye kwa siku chache wanazoishi chini ya mbingu.

42:4 1Fal 7:1-12; Wim 8:11; 2Nya 2:1Nikafanya miradi mikubwa: Nikajijengea majumba na kulima mashamba ya mizabibu. 5Nikatengeneza bustani na viwanja vya starehe nikaotesha huko kila aina ya miti ya matunda. 6Nikajenga mabwawa ya kukusanya maji ya kunyweshea hii miti iliyokuwa inastawi vizuri. 7Nikanunua watumwa wa kiume na wa kike na watumwa wengine walizaliwa nyumbani mwangu. Pia nilikuwa na makundi ya ngʼombe, kondoo na mbuzi kuliko mtu yeyote aliyewahi kuishi Yerusalemu kabla yangu. 82:8 1Fal 9:28; 10:10-21; 2Sam 19:35; Amu 3:15Nikajikusanyia fedha na dhahabu, hazina za wafalme na za majimbo. Nikajipatia waimbaji wanaume na wanawake, nazo nyumba za masuria: vitu ambavyo moyo wa mwanadamu hufurahia. 92:9 1Nya 29:25; Mhu 1:12-16Nikawa maarufu sana kuliko mtu mwingine yeyote aliyepata kuishi Yerusalemu kabla yangu. Katika haya yote bado nikawa nina hekima.

10Sikujinyima kitu chochote ambacho macho yangu yalikitamani,

hakuna anasa ambayo niliunyima moyo wangu.

Moyo wangu ulifurahia kazi zangu zote,

hii ilikuwa thawabu ya kazi zangu zote.

11Hata hivyo nilipokuja kuangalia yote ambayo

mikono yangu ilikuwa imefanya

na yale niliyotaabika kukamilisha,

kila kitu kilikuwa ni ubatili, ni kukimbiza upepo;

hapakuwa na faida yoyote chini ya jua.

Hekima Na Upumbavu Ni Ubatili

12Kisha nikageuza mawazo yangu kufikiria hekima,

wazimu na upumbavu.

Ni nini zaidi mtu anayetawala baada ya mfalme

anachoweza kufanya ambacho hakijafanywa?

132:13 Mhu 7:11-12, 19; 9:18Nikaona kuwa hekima ni bora kuliko upumbavu,

kama vile nuru ilivyo bora kuliko giza.

142:14 Za 49:10; Mit 17:24; Mhu 8:1; 3:19; 7:2; 9:3, 11-12Mtu mwenye hekima ana macho katika kichwa chake,

lakini mpumbavu anatembea gizani;

lakini nikaja kuona kwamba

wote wawili hatima yao inafanana.

152:15 Mhu 6:8Kisha nikafikiri moyoni mwangu,

“Hatima ya mpumbavu itanipata mimi pia.

Nitafaidi nini basi kwa kuwa na hekima?”

Nikasema moyoni mwangu,

“Hili nalo ni ubatili.”

162:16 Za 49:10; 112:6; Mhu 1:11Kwa maana kwa mtu mwenye hekima,

kama ilivyo kwa mpumbavu,

hatakumbukwa kwa muda mrefu,

katika siku zijazo wote watasahaulika.

Kama vile ilivyo kwa mpumbavu,

mtu mwenye hekima pia lazima atakufa!

Kutaabika Ni Ubatili

17Kwa hiyo nikachukia maisha, kwa sababu kazi inayofanyika chini ya jua ilikuwa masikitiko kwangu. Yote hayo ni ubatili, ni kukimbiza upepo. 182:18 Za 39:6; 49:10; 1Fal 12:13Nikachukia kila kitu nilichokuwa nimetaabikia chini ya jua, kwa sababu ni lazima nimwachie yule ajaye baada yangu. 19Nani ajuaye kama atakuwa ni mtu mwenye hekima au mpumbavu? Lakini hata hivyo yeye ndiye atakayetawala kazi zote ambazo nimemiminia juhudi na ustadi chini ya jua. Hili nalo ni ubatili. 20Kwa hiyo moyo wangu ukaanza kukata tamaa juu ya kazi yangu yote niliyoifanya kwa taabu chini ya jua. 21Kwa kuwa mtu anaweza kufanya kazi yake kwa hekima, maarifa na ustadi, kisha analazimika kuacha vyote alivyo navyo kwa mtu mwingine ambaye hajavifanyia kazi. Hili nalo pia ni ubatili tena ni balaa kubwa. 222:22 Mhu 3:9; 1:3Mtu atapata nini kwa taabu yote na kuhangaika kwa bidii katika kazi anayotaabikia chini ya jua? 232:23 Ay 5:7; 7:2; 14:1; Mhu 1:18; Mwa 3:17Siku zake zote kazi yake ni maumivu na masikitiko, hata usiku akili yake haipati mapumziko. Hili nalo pia ni ubatili.

242:24 1Kor 15:32; Mhu 3:12-13, 22; 7:7-10; 8:15; 5:17-19; 9:7-10; 11:7-10; Ay 2:10Hakuna kitu bora anachoweza kufanya mtu zaidi ya kula na kunywa na kuridhika katika kazi yake. Hili nalo pia, ninaona, latokana na mkono wa Mungu, 25kwa sababu pasipo yeye, ni nani awezaye kula na kufurahi? 262:26 Ay 27:17; 9:4; Mit 13:22Kwa yule mtu anayempendeza Mungu, Mungu humpa hekima, maarifa na furaha, bali kwa mwenye dhambi Mungu humpa kazi ya kukusanya na kuhifadhi utajiri ili Mungu ampe yule anayempenda. Hili nalo pia ni ubatili, ni kukimbiza upepo.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Eclesiastés 2:1-26

1Me dije entonces: «Vamos, pues, haré la prueba con los placeres y me daré la gran vida». ¡Pero aun esto resultó un absurdo! 2A la risa la considero una locura; en cuanto a los placeres, ¿para qué sirven?

3Quise luego hacer la prueba de entregarme al vino —si bien mi mente estaba bajo el control de la sabiduría—, y de aferrarme a la necedad, hasta ver qué ventaja le encuentra el hombre a lo que hace bajo el cielo durante los contados días de su vida.

4Realicé grandes obras: me construí casas, me planté viñedos, 5cultivé mis propios huertos y jardines, y en ellos planté toda clase de árboles frutales. 6También me construí aljibes para regar los muchos árboles que allí crecían. 7Me hice con esclavos y esclavas; y tuve criados, y mucho más ganado vacuno y lanar que todos los que me precedieron en Jerusalén. 8Amontoné oro y plata, y tesoros que fueron de reyes y provincias. Me hice con cantores y cantoras, y disfruté de los deleites de los hombres: ¡formé mi propio harén!2:8 ¡formé mi propio harén! Frase de difícil traducción.

9Me engrandecí en gran manera, más que todos los que me precedieron en Jerusalén; además, la sabiduría permanecía conmigo. 10No les negué a mis ojos ningún deseo, ni privé a mi corazón de placer alguno. Mi corazón disfrutó de todos mis afanes. ¡Solo eso saqué de tanto afanarme!

11Consideré luego todas mis obras y el trabajo que me había costado realizarlas, y vi que todo era absurdo, un correr tras el viento, y que ningún provecho se saca en esta vida.

Todos paran en lo mismo

12Consideré entonces la sabiduría, la necedad y la insensatez —¿qué más puede hacer el sucesor del rey, aparte de lo ya hecho?—, 13y pude observar que hay más provecho en la sabiduría que en la insensatez, así como hay más provecho en la luz que en las tinieblas.

14El sabio tiene los ojos bien puestos,

pero el necio anda a oscuras.

Pero también me di cuenta de que un mismo final les espera a todos. 15Me dije entonces: «Si al fin voy a acabar igual que el necio, ¿de qué me sirve ser tan sabio?» Y concluí que también esto es absurdo, 16pues nadie se acuerda jamás del sabio ni del necio; con el paso del tiempo todo cae en el olvido, y lo mismo mueren los sabios que los necios.

17Aborrecí entonces la vida, pues todo cuanto se hace en ella me resultaba repugnante. Realmente, todo es absurdo; ¡es correr tras el viento!

18Aborrecí también el haberme afanado tanto en esta vida, pues el fruto de tanto afán tendría que dejárselo a mi sucesor, 19y ¿quién sabe si este sería sabio o necio? Sin embargo, se adueñaría de lo que con tantos afanes y sabiduría logré hacer en esta vida. ¡Y también esto es absurdo!

20Volví a sentirme descorazonado de haberme afanado tanto en esta vida, 21pues hay quienes ponen a trabajar su sabiduría y sus conocimientos y experiencia, para luego entregarle todos sus bienes a quien jamás movió un dedo. ¡Y también esto es absurdo, y un mal enorme! 22Pues, ¿qué gana el hombre con todos sus esfuerzos y con tanto preocuparse y afanarse bajo el sol? 23Todos sus días están plagados de sufrimientos y tareas frustrantes, y ni siquiera de noche descansa su mente. ¡Y también esto es absurdo!

24Nada hay mejor para el hombre que comer y beber, y llegar a disfrutar de sus afanes. He visto que también esto proviene de Dios, 25porque ¿quién puede comer y alegrarse, si no es por Dios?2:25 por Dios (véanse mss. hebreos, LXX y Siríaca); por mí (TM). 26En realidad, Dios da sabiduría, conocimientos y alegría a quien es de su agrado; en cambio, al pecador le impone la tarea de acumular más y más, para luego dárselo todo a quien es de su agrado. Y también esto es absurdo; ¡es correr tras el viento!