Mhubiri 10 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 10:1-20

110:1 Mit 13:16; 18:2Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato,

ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.

2Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume,

lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.

3Hata anapotembea barabarani,

mpumbavu hukosa ufahamu

na kudhihirisha kwa kila mmoja

jinsi alivyo mpumbavu.

410:4 Mit 16:14; 25:15; Mhu 8:3Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako,

usiache mahali pako,

utulivu huweza kuzuia makosa mengi.

5Kuna ubaya niliouona chini ya jua,

aina ya kosa litokalo kwa mtawala:

610:6 Mit 29:2Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu,

wakati matajiri hushika nafasi za chini.

710:7 Mit 19:10Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi,

wakati wakuu wakitembea

kwa miguu kama watumwa.

810:8 Es 2:23; Amo 5:19; Mit 26:27; Za 57:6; 9:16Yeye achimbaye shimo

aweza kutumbukia ndani yake,

yeyote abomoaye ukuta

anaweza kuumwa na nyoka.

910:9 Mit 26:27Yeyote apasuaye mawe

inawezekana yakamuumiza,

yeyote apasuaye magogo

inawezekana yakamuumiza.

10Kama shoka ni butu

na halikunolewa,

nguvu nyingi zinahitajika,

lakini ustadi utaleta mafanikio.

1110:11 Yer 8:17; Za 58:5; Isa 3:3Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi,

mwaguzi hatahitajika tena.

1210:12 Mit 10:14, 32; 14:3; 15:2; 18:7Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima

yana neema,

bali mpumbavu huangamizwa

na midomo yake mwenyewe.

13Mwanzoni maneno yake ni upumbavu,

mwishoni ni wazimu mbaya,

1410:14 Yak 4:14; Mit 15:2; Mhu 8:7; 5:3; 9:1naye mpumbavu huzidisha maneno.

Hakuna yeyote ajuaye linalokuja,

ni nani awezaye kueleza ni jambo gani

litakalotokea baada yake?

15Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe,

hajui njia iendayo mjini.

1610:16 Isa 3:4-12Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa

na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.

1710:17 Mit 31:4; Kum 14:26; 1Sam 25:36Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika

na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa:

ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.

1810:18 Mit 20:4; 24:30-34Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama,

kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.

1910:19 Mwa 14:18; Amu 9:13Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko,

nao mvinyo hufurahisha maisha,

lakini fedha ni jawabu la mambo yote.

2010:20 Kut 22:28Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako,

au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala,

kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako,

naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.

Korean Living Bible

전도서 10:1-20

1죽은 파리가 향수도 악취가 나게 하듯이 작은 어리석음이 지혜와 영 예를 무색하게 한다.

2지혜로운 사람의 마음은 옳은 일을 하는 쪽으로 기울어지고 어리석은 사람의 마음은 악을 행하는 쪽으로 기울어진다.

3어리석은 사람은 지혜가 없으므로 길을 갈 때에도 모든 사람에게 자기 어리석음을 드러낸다.

410:4 또는 ‘주권자가 네게 분을 일으키거든 너는 네 자리를 떠나지 말라’윗사람이 너에게 화를 내어도 너는 사표를 제출하지 말아라. 아무 말 없이 가만히 있으면 큰 잘못도 용서받을 수 있다.

5나는 통치자들에게서 한 가지 잘못된 점을 보았는데

6그것은 어리석은 자들에게 높은 지위를 주고 반면에 부자들은 낮은 자리에 앉히는 것이다.

7내가 또 보니 종들은 말을 타고 귀족들은 종처럼 걸어다닌다.

8함정을 파는 자는 바로 그 함정에 빠질 것이며 담을 허는 자는 뱀에게 물릴 것이다.

9채석장에서 일하는 자는 돌에 다칠 것이며 나무를 쪼개는 자는 그 나무 때문에 위험을 당할 것이다.

10도끼를 갈지 않아 날이 무디면 그만큼 힘이 더 든다. 그러므로 도끼 날을 가는 것이 지혜로운 방법이다.

11마술을 걸기 전에 뱀에게 물리면 마술사는 아무 소용이 없다.

12지혜로운 사람의 말은 은혜를 끼치지만 어리석은 사람의 말은 자신을 망친다.

13미련한 자는 처음에 어리석은 말로 시작했다가 나중에는 미치광이처럼 말한다.

14그래서 미련한 자는 말이 많은 법이다. 앞으로 무슨 일이 일어날지 아는 사람은 아무도 없다. 그런데 그가 죽은 다음의 일을 누가 그에게 말해 줄 수 있겠는가?

15바보는 작은 일에도 쉽게 싫증을 느끼며 자기 집을 찾아가는 길도 모른다.

16왕이 어리고 지도자들이 아침부터 술타령을 하는 나라는 망할 것이다.

17그러나 왕이 고결한 인품을 가졌고 지도자들은 취하기 위해서가 아니라 일하는 데 필요한 힘을 얻기 위해서 때와 장소를 가려 먹고 마시는 나라는 번영을 누릴 것이다.

18게으르면 서까래가 썩어서 내려앉고 손을 놀리지 않고 가만히 있으면 집에 물이 새는 법이다.

19잔치는 즐기기 위한 것이며 포도주는 흥을 돋우기 위한 것이지만 돈은 모든 것을 해결해 준다.

20마음으로도 왕을 저주하지 말며 은밀한 침실에서도 부자를 저주하지 말아라. 10:20 원문에는 ‘공중의 새가 그 소리를 전하고 날짐승이 그 일을 전 파할 것이니라’낮 말은 새가 듣고 밤 말은 쥐가 듣는다.