Mhubiri 10 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 10:1-20

110:1 Mit 13:16; 18:2Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato,

ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.

2Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume,

lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.

3Hata anapotembea barabarani,

mpumbavu hukosa ufahamu

na kudhihirisha kwa kila mmoja

jinsi alivyo mpumbavu.

410:4 Mit 16:14; 25:15; Mhu 8:3Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako,

usiache mahali pako,

utulivu huweza kuzuia makosa mengi.

5Kuna ubaya niliouona chini ya jua,

aina ya kosa litokalo kwa mtawala:

610:6 Mit 29:2Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu,

wakati matajiri hushika nafasi za chini.

710:7 Mit 19:10Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi,

wakati wakuu wakitembea

kwa miguu kama watumwa.

810:8 Es 2:23; Amo 5:19; Mit 26:27; Za 57:6; 9:16Yeye achimbaye shimo

aweza kutumbukia ndani yake,

yeyote abomoaye ukuta

anaweza kuumwa na nyoka.

910:9 Mit 26:27Yeyote apasuaye mawe

inawezekana yakamuumiza,

yeyote apasuaye magogo

inawezekana yakamuumiza.

10Kama shoka ni butu

na halikunolewa,

nguvu nyingi zinahitajika,

lakini ustadi utaleta mafanikio.

1110:11 Yer 8:17; Za 58:5; Isa 3:3Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi,

mwaguzi hatahitajika tena.

1210:12 Mit 10:14, 32; 14:3; 15:2; 18:7Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima

yana neema,

bali mpumbavu huangamizwa

na midomo yake mwenyewe.

13Mwanzoni maneno yake ni upumbavu,

mwishoni ni wazimu mbaya,

1410:14 Yak 4:14; Mit 15:2; Mhu 8:7; 5:3; 9:1naye mpumbavu huzidisha maneno.

Hakuna yeyote ajuaye linalokuja,

ni nani awezaye kueleza ni jambo gani

litakalotokea baada yake?

15Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe,

hajui njia iendayo mjini.

1610:16 Isa 3:4-12Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa

na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.

1710:17 Mit 31:4; Kum 14:26; 1Sam 25:36Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika

na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa:

ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.

1810:18 Mit 20:4; 24:30-34Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama,

kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.

1910:19 Mwa 14:18; Amu 9:13Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko,

nao mvinyo hufurahisha maisha,

lakini fedha ni jawabu la mambo yote.

2010:20 Kut 22:28Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako,

au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala,

kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako,

naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

傳道書 10:1-20

1死蒼蠅會使芬芳的膏油發臭,

同樣,一點點愚昧足以毀掉智慧和尊榮。

2智者的心引導他走正路,

愚人的心帶領他入歧途。10·2 這一節希伯來文是「智者的心在右,愚人的心在左。」

3愚人走路時也無知,

並向眾人顯出他的愚昧。

4如果當權的人向你大發雷霆,

不要因此就離開崗位,

因為平心靜氣能避免大錯。

5我發現日光之下有一件可悲的事,

似乎是掌權者所犯的錯誤:

6愚人身居許多高位,

富人卻屈居在下。

7我曾看見奴僕騎在馬上,

王子卻像奴僕一樣步行。

8挖掘陷阱的,自己必掉在其中;

拆圍牆的,必被蛇咬;

9開鑿石頭的,必被砸傷;

劈木頭的,必有危險。

10斧頭鈍了若不磨利,

用起來必多費力氣,

但智慧能助人成功。

11弄蛇人行法術之前,

若先被蛇咬,

行法術還有什麼用呢?

12智者口出恩言,

愚人的話毀滅自己。

13愚人開口是愚昧,

閉口是邪惡狂妄。

14愚人高談闊論,

其實無人知道將來的事,

人死後,誰能告訴他世間的事呢?

15愚人因勞碌而精疲力盡,

連進城的路也認不出來。

16一國之君若年幼無知,

他的臣宰從早到晚只顧宴樂,

那國就有禍了!

17一國之君若英明尊貴,

他的臣宰為了強身健體而節制飲食,

不酗酒宴樂,那國就有福了!

18屋頂因人懶惰而坍塌,

房間因人遊手好閒而漏雨。

19宴席帶來歡笑,

酒使人開懷,

錢使人萬事亨通。

20不可咒詛君王,

連這樣的意念都不可有,

也不可在臥室裡咒詛富豪,

因為天空的飛鳥會通風報信,

有翅膀的會把事情四處傳開。