Mathayo 3 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 3:1-17

Yohana Mbatizaji Atayarisha Njia

(Marko 1:1-8; Luka 3:1-18; Yohana 1:19-28)

13:1 Lk 3:2-19Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema, 23:2 Dan 7:14; Lk 17:20“Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.” 33:3 Mal 3:1; Yn 1:23Huyu ndiye yule aliyenenwa habari zake na nabii Isaya aliposema:

“Sauti ya mtu aliaye huko nyikani,

‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana,

yanyoosheni mapito yake.’ ”

43:4 1Fal 1:8Basi Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia, akiwa na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu. 53:5 Mk 1:5; Lk 3:7Watu walikuwa wakimwendea kutoka Yerusalemu, Uyahudi yote na nchi zote za kandokando ya Mto Yordani. 63:6 Mdo 19:4, 18; Mk 1:4Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.

73:7 Mt 12:34; 23:33; Rum 1:18; 1The 1:10Lakini alipowaona Mafarisayo na Masadukayo wengi wakija ili kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja? 83:8 Mdo 26:20Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. 93:9 Rum 2:28-29Wala msidhani mnaweza kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwa mawe haya. 103:10 Lk 3:9; Yn 15:2-6Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti, basi kila mti usiozaa matunda mazuri, hukatwa na kutupwa motoni.

113:11 Mk 1:18; Isa 4:4; Mdo 2:3-4“Mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini nyuma yangu anakuja yeye aliye na uwezo kuliko mimi, ambaye sistahili hata kuvichukua viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu3:11 …kwa Roho Mtakatifu hapa ina maana ya katika Roho Mtakatifu. na kwa moto. 123:12 Mt 13:30; 25:41Pepeto lake liko mkononi mwake, naye atasafisha sakafu yake ya kupuria, na kuikusanya ngano ghalani na kuyateketeza makapi kwa moto usiozimika.”

Yesu Abatizwa

(Marko 1:9-11; Luka 3:21-22)

133:13 Mt 3:1; Mk 1:4; Yn 1:31-34Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Mto Yordani ili Yohana ambatize. 14Lakini Yohana akajitahidi kumzuia, akimwambia, “Mimi ninahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu nikubatize?”

15Lakini Yesu akamjibu, “Kubali hivi sasa, kwa maana ndivyo itupasavyo kwa njia hii kuitimiza haki yote.” Hivyo Yohana akakubali.

163:16 Isa 11:2; 42:1; Mk 1:10; Lk 3:22; Yn 1:32-33Naye Yesu alipokwisha kubatizwa, mara alipotoka ndani ya maji, ghafula mbingu zikafunguka, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua na kutulia juu yake. 173:17 Kum 4:12; Yn 12:28; Za 2:7; 2:7; Mdo 13:33; Isa 42:1; 2Pet 1:17Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ambaye ninapendezwa sana naye.”

King James Version

Matthew 3:1-17

1In those days came John the Baptist, preaching in the wilderness of Judaea, 2And saying, Repent ye: for the kingdom of heaven is at hand. 3For this is he that was spoken of by the prophet Esaias, saying, The voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, make his paths straight. 4And the same John had his raiment of camel’s hair, and a leathern girdle about his loins; and his meat was locusts and wild honey. 5Then went out to him Jerusalem, and all Judaea, and all the region round about Jordan, 6And were baptized of him in Jordan, confessing their sins.

7¶ But when he saw many of the Pharisees and Sadducees come to his baptism, he said unto them, O generation of vipers, who hath warned you to flee from the wrath to come? 8Bring forth therefore fruits meet for repentance: 9And think not to say within yourselves, We have Abraham to our father: for I say unto you, that God is able of these stones to raise up children unto Abraham. 10And now also the axe is laid unto the root of the trees: therefore every tree which bringeth not forth good fruit is hewn down, and cast into the fire. 11I indeed baptize you with water unto repentance: but he that cometh after me is mightier than I, whose shoes I am not worthy to bear: he shall baptize you with the Holy Ghost, and with fire: 12Whose fan is in his hand, and he will throughly purge his floor, and gather his wheat into the garner; but he will burn up the chaff with unquenchable fire.

13¶ Then cometh Jesus from Galilee to Jordan unto John, to be baptized of him. 14But John forbad him, saying, I have need to be baptized of thee, and comest thou to me? 15And Jesus answering said unto him, Suffer it to be so now: for thus it becometh us to fulfil all righteousness. Then he suffered him. 16And Jesus, when he was baptized, went up straightway out of the water: and, lo, the heavens were opened unto him, and he saw the Spirit of God descending like a dove, and lighting upon him: 17And lo a voice from heaven, saying, This is my beloved Son, in whom I am well pleased.