Mathayo 24 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 24:1-51

Kubomolewa Kwa Hekalu Kwatabiriwa

(Marko 13:1-2; Luka 21:5-6)

124:1 Mk 13:1; Lk 21:5Yesu akatoka Hekaluni na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya Hekalu. 224:2 Lk 19:44; 1Fal 9:7; Yer 26:18; Mik 3:12Ndipo Yesu akawauliza, “Je, mnayaona haya yote? Amin, nawaambia, hakuna hata jiwe moja hapa litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”

Ishara Za Nyakati Za Mwisho

(Marko 13:3-23; Luka 21:7-24)

324:3 Mt 21:1Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani, wakamuuliza, “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, nayo dalili ya kuja kwako na ya mwisho wa dunia ni gani?”

424:4 Efe 5:6; Kol 2:8, 18; 2The 2:3; 1Yn 4:1Yesu akawajibu, “Jihadharini, mtu yeyote asiwadanganye. 524:5 Mt 24:11, 23-24; 1Yn 2:18Kwa maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye Kristo,’24:5 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. nao watawadanganya wengi. 624:6 Dan 2:26Mtasikia habari za vita na matetesi ya vita. Angalieni msitishike, kwa maana haya hayana budi kutukia. Lakini ule mwisho bado. 724:7 Isa 19:2; Mdo 11:28Taifa litainuka dhidi ya taifa, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali. 8Haya yote yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

924:9 Mt 10:17; Yn 16:2“Ndipo mtasalitiwa, ili mteswe na kuuawa, nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa ajili yangu. 1024:10 Dan 11:41Wakati huo, wengi wataacha imani yao, nao watasalitiana kila mmoja na mwenzake na kuchukiana. 1124:11 Mt 7; 15Watatokea manabii wengi wa uongo, nao watawadanganya watu wengi. 12Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo wa watu wengi utapoa, 1324:13 Mt 10:22lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa. 1424:14 Mt 4:23; Rum 10:18; Ufu 3:10Injili ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni kote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utakapokuja.

1524:15 Mdo 6:13; Dan 11:31; 12:11“Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu), 16basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. 1724:17 1Sam 9:25; Lk 12:3Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba. 18Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 1924:19 Lk 23:29Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! 2024:20 Mdo 1:12Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato. 2124:21 Eze 5:9; Dan 12:1Kwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe. 2224:22 Isa 65:8, 9Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angeokoka. Lakini kwa ajili ya wateule, siku hizo zitafupizwa. 2324:23 Lk 17:23; 21:8Wakati huo kama mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo huyu hapa!’ Au, ‘Kristo yuko kule,’ msisadiki. 2424:24 Kut 7:11, 22; Ufu 16:14Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara kubwa na maajabu mengi ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule hasa. 25Angalieni, nimekwisha kuwaambia mapema.

26“Kwa hiyo mtu yeyote akiwaambia, ‘Yule kule nyikani,’ msiende huko. Au akisema, ‘Yuko kwenye chumba,’ msisadiki. 2724:27 Lk 17:24; Mt 8:20Kwa maana kama vile umeme utokeavyo mashariki na kuonekana hata magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. 2824:28 Lk 17:37Kwa maana popote ulipo mzoga, huko ndiko wakusanyikapo tai.

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

(Marko 13:24-31; Luka 21:25-33)

2924:29 Sef 1:15; Ufu 8:12“Mara baada ya dhiki ya siku zile,

“ ‘jua litatiwa giza,

nao mwezi hautatoa nuru yake;

nazo nyota zitaanguka kutoka angani,

na nguvu za anga zitatikisika.’

3024:30 Dan 7:13; Ufu 1:7“Ndipo itakapotokea ishara ya Mwana wa Adamu angani, na makabila yote ya dunia yataomboleza. Nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu. 3124:31 Mt 13:41; Zek 9:14; 1The 4:16Naye atawatuma malaika zake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.

3224:32 Lk 21:29“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 3324:33 Yak 5:9Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yote, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 3424:34 Mt 16:28; 23:36Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 3524:35 Mt 5:18Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

(Marko 13:32-37; Luka 17:26-30, 34-36)

3624:36 Mdo 1:7“Kwa habari ya siku ile na saa, hakuna ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake. 3724:37 Mwa 6:5; 7:6-23Kama ilivyokuwa wakati wa Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. 3824:38 Mt 22:30Kwa maana siku zile kabla ya gharika, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. 3924:39 Lk 15Nao hawakujua lolote mpaka gharika ilipokuja ikawakumba wote. Hivyo ndivyo itakavyokuwa atakapokuja Mwana wa Adamu. 4024:40 Lk 17:34-35Watu wawili watakuwa shambani, naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. 4124:41 Lk 17:30Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja, naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.

4224:42 Mt 25:13; Lk 12:40“Basi kesheni, kwa sababu hamjui ni siku gani atakapokuja Bwana wenu. 4324:43 Lk 12:39Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua ni wakati gani wa usiku ambao mwizi atakuja, angekesha na hangekubali nyumba yake kuvunjwa. 4424:44 1The 5:6Kwa hiyo ninyi pia hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.

Mfano Wa Mtumishi Mwaminifu

(Luka 12:41-48)

4524:45 Mt 25:21-23“Ni nani basi aliye mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake amemweka kusimamia watumishi wengine katika nyumba yake, ili awape chakula chao kwa wakati unaofaa? 4624:46 Ufu 16:15Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo. 4724:47 Mt 25:21, 23; Lk 22:29Amin, nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote. 4824:48 Mhu 8:11Lakini kama huyo mtumishi ni mwovu, naye akasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu atakawia muda mrefu,’ 4924:49 Lk 21:34kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, na kula na kunywa pamoja na walevi. 50Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. 5124:51 Mt 8:12Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wanafiki, mahali ambako kutakuwa ni kulia na kusaga meno.

New International Version – UK

Matthew 24:1-51

The destruction of the temple and signs of the end times

1Jesus left the temple and was walking away when his disciples came up to him to call his attention to its buildings. 2‘Do you see all these things?’ he asked. ‘Truly I tell you, not one stone here will be left on another; every one will be thrown down.’

3As Jesus was sitting on the Mount of Olives, the disciples came to him privately. ‘Tell us,’ they said, ‘when will this happen, and what will be the sign of your coming and of the end of the age?’

4Jesus answered: ‘Watch out that no-one deceives you. 5For many will come in my name, claiming, “I am the Messiah,” and will deceive many. 6You will hear of wars and rumours of wars, but see to it that you are not alarmed. Such things must happen, but the end is still to come. 7Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom. There will be famines and earthquakes in various places. 8All these are the beginning of birth-pains.

9‘Then you will be handed over to be persecuted and put to death, and you will be hated by all nations because of me. 10At that time many will turn away from the faith and will betray and hate each other, 11and many false prophets will appear and deceive many people. 12Because of the increase of wickedness, the love of most will grow cold, 13but the one who stands firm to the end will be saved. 14And this gospel of the kingdom will be preached in the whole world as a testimony to all nations, and then the end will come.

15‘So when you see standing in the holy place “the abomination that causes desolation,”24:15 Daniel 9:27; 11:31; 12:11 spoken of through the prophet Daniel – let the reader understand – 16then let those who are in Judea flee to the mountains. 17Let no-one on the housetop go down to take anything out of the house. 18Let no-one in the field go back to get their cloak. 19How dreadful it will be in those days for pregnant women and nursing mothers! 20Pray that your flight will not take place in winter or on the Sabbath. 21For then there will be great distress, unequalled from the beginning of the world until now – and never to be equalled again.

22‘If those days had not been cut short, no-one would survive, but for the sake of the elect those days will be shortened. 23At that time if anyone says to you, “Look, here is the Messiah!” or, “There he is!” do not believe it. 24For false messiahs and false prophets will appear and perform great signs and wonders to deceive, if possible, even the elect. 25See, I have told you in advance.

26‘So if anyone tells you, “There he is, out in the desert,” do not go out; or, “Here he is, in the inner rooms,” do not believe it. 27For as lightning that comes from the east is visible even in the west, so will be the coming of the Son of Man. 28Wherever there is a carcass, there the vultures will gather.

29‘Immediately after the distress of those days

‘ “the sun will be darkened,

and the moon will not give its light;

the stars will fall from the sky,

and the heavenly bodies will be shaken.”24:29 Isaiah 13:10; 34:4

30‘Then will appear the sign of the Son of Man in heaven. And then all the peoples of the earth24:30 Or the tribes of the land will mourn when they see the Son of Man coming on the clouds of heaven, with power and great glory.24:30 See Daniel 7:13-14. 31And he will send his angels with a loud trumpet call, and they will gather his elect from the four winds, from one end of the heavens to the other.

32‘Now learn this lesson from the fig-tree: as soon as its twigs become tender and its leaves come out, you know that summer is near. 33Even so, when you see all these things, you know that it24:33 Or he is near, right at the door. 34Truly I tell you, this generation will certainly not pass away until all these things have happened. 35Heaven and earth will pass away, but my words will never pass away.

The day and hour unknown

36‘But about that day or hour no-one knows, not even the angels in heaven, nor the Son,24:36 Some manuscripts do not have nor the Son. but only the Father. 37As it was in the days of Noah, so it will be at the coming of the Son of Man. 38For in the days before the flood, people were eating and drinking, marrying and giving in marriage, up to the day Noah entered the ark; 39and they knew nothing about what would happen until the flood came and took them all away. That is how it will be at the coming of the Son of Man. 40Two men will be in the field; one will be taken and the other left. 41Two women will be grinding with a hand-mill; one will be taken and the other left.

42‘Therefore keep watch, because you do not know on what day your Lord will come. 43But understand this: if the owner of the house had known at what time of night the thief was coming, he would have kept watch and would not have let his house be broken into. 44So you also must be ready, because the Son of Man will come at an hour when you do not expect him.

45‘Who then is the faithful and wise servant, whom the master has put in charge of the servants in his household to give them their food at the proper time? 46It will be good for that servant whose master finds him doing so when he returns. 47Truly I tell you, he will put him in charge of all his possessions. 48But suppose that servant is wicked and says to himself, “My master is staying away a long time,” 49and he then begins to beat his fellow servants and to eat and drink with drunkards. 50The master of that servant will come on a day when he does not expect him and at an hour he is not aware of. 51He will cut him to pieces and assign him a place with the hypocrites, where there will be weeping and gnashing of teeth.