Mathayo 23 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 23:1-39

Yesu Awashutumu Walimu Wa Sheria Na Mafarisayo

(Marko 12:38-40; Luka 11:39-52; 20:45-47)

123:1 Mk 12:38-40Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake: 223:2 Ezr 7:6, 25; Neh 8:4“Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose, 323:3 Mal 2:7, 8hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri. 423:4 Mdo 15:10; Gal 6:13Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.

523:5 Mt 6:1-5, 16; Kut 13:6-9; Hes 15:38; Kum 22:12“Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao. 623:6 Lk 14:7; 20:46Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi. 723:7 Mk 9:5; Yn 20:16Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’23:7 Rabi maana yake Bwana, Mwalimu.

823:8 Yak 3:1; 2Kor 1:24; 1Pet 5:3“Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi,’ kwa sababu mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu. 923:9 Mal 1:6; Mt 9:6Nanyi msimwite mtu yeyote ‘Baba,’ hapa duniani, kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni. 10Wala msiitwe ‘Mwalimu,’ kwa maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.23:10 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 1123:11 Mt 20:26; Mk 9:35Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu. 1223:12 Za 18:27; Lk 1:52Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.

1323:13 Mt 23:25-29; Lk 11:52“Lakini ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Kwa maana mnawafungia watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka kuingia mnawazuia. [ 1423:14 Mk 12:40; Lk 20:47; 2Tim 3:6; Tit 1:11Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo hukumu yenu itakuwa kuu zaidi.]

1523:15 Mdo 6:5; 13:43; Mt 5:22“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi!

1623:16 Isa 9; 16; Mt 15:14; 5:33-35“Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi mwasema, ‘Mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’ 1723:17 Kut 30:29Ninyi vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi: ni ile dhahabu, au ni lile Hekalu linaloifanya hiyo dhahabu kuwa takatifu? 18Pia mnasema, ‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, amefungwa kwa kiapo chake’ 1923:19 Kut 29:37Ninyi vipofu! Ni kipi kikuu zaidi: ni sadaka, au ni madhabahu yanayoifanya hiyo sadaka kuwa takatifu? 20Kwa hiyo, mtu aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hayo madhabahu na vitu vyote vilivyo juu yake. 2123:21 1Fal 8:13; Za 26:8Naye mtu aapaye kwa Hekalu, huapa kwa hilo Hekalu na kwa huyo akaaye ndani yake. 2223:22 Za 11:4; Mt 5:34Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketiye juu ya kiti hicho.

2323:23 Law 27:30; Mik 6:8; Lk 11:42“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo. 2423:24 Mt 23:16Ninyi viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini mnameza ngamia!

2523:25 Mk 7:4; Lk 11:39“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na kutokuwa na kiasi. 2623:26 Tit 1:15; Yn 9:40Ewe Farisayo kipofu! Safisha ndani ya kikombe na sahani kwanza, ndipo nje itakuwa safi pia.

2723:27 Lk 11:44; Mdo 23:3“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo yanapendeza kwa nje, lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu. 2823:28 Lk 16:15Vivyo hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.

2923:29 Lk 11:47-48“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki. 30Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’ 3123:31 Mt 5:12; Mdo 7:51-52Hivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii. 3223:32 1The 2:16; Eze 20:4Haya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!

3323:33 Mt 3:7; 12:34; 5:22“Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? 3423:34 2Nya 36:15-16; Lk 11:49; Mt 10:17; 10:23Kwa sababu hii, tazameni, natuma kwenu manabii na wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha, na wengine wao mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwafuatia kutoka mji mmoja hadi mji mwingine. 3523:35 Mwa 4:8; Ebr 11:4; 2Nya 24:21Hivyo ile damu ya wenye haki wote iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mliyemuua kati ya patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu. 3623:36 Mt 24:34; Lk 11:50-51Amin, nawaambia, haya yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

Yesu Aililia Yerusalemu

(Luka 13:34-35)

3723:37 2Nya 24:21; Mt 5:12“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka! 3823:38 1Fal 9:7-8; Yer 22:5Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. 3923:39 Za 118:26; Mt 21:9Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’ ”

La Bible du Semeur

Matthieu 23:1-39

La condamnation des chefs religieux

(Mc 12.38-40 ; Lc 11.39-52 ; 20.45-47)

1Alors Jésus, s’adressant à la foule et à ses disciples, dit : 2Les spécialistes de la Loi et les pharisiens sont chargés d’enseigner la Loi de Moïse. 3Faites donc tout ce qu’ils vous disent, et réglez votre conduite sur leur enseignement. Mais gardez-vous de prendre modèle sur leurs actes, car ils parlent d’une manière et agissent d’une autre.

4Ils lient de pesants fardeaux et les placent sur les épaules des hommes ; mais ils ne bougeraient même pas le petit doigt pour les déplacer. 5Dans tout ce qu’ils font, ils agissent pour être vus des hommes. Ainsi, les petits coffrets à versets qu’ils portent pendant la prière sont plus grands que ceux des autres, et les franges de leurs manteaux plus longues23.5 Pour la prière, les Juifs portaient des tephillins ou phylactères. Il s’agissait de deux petites boîtes fixées à des lanières que l’on attachait, l’une sur le front, l’autre sur le bras gauche, et qui contenaient des bandes de parchemins sur lesquels étaient inscrits des versets de la Loi. Cette coutume était vue comme obéissant à l’injonction de Dt 6.8. Les Juifs pieux ornaient aussi leurs vêtements de franges, qui devaient leur rappeler les commandements de la Loi, selon ce qui était demandé en Dt 22.12. Certains devaient avoir des franges particulièrement longues, pour faire étalage de leur piété.. 6Ils affectionnent les meilleures places dans les banquets et les sièges d’honneur dans les synagogues. 7Ils aiment qu’on les salue sur les places publiques et qu’on les appelle « Maître ».

8Mais vous, ne vous faites pas appeler « Maître », car pour vous, il n’y a qu’un seul Maître, et vous êtes tous frères. 9Ne donnez pas non plus à quelqu’un, ici-bas, le titre de « Père », car pour vous, il n’y a qu’un seul Père : le Père céleste. 10Ne vous faites pas non plus appeler chefs23.10 Matthieu emploie un mot unique dans le Nouveau Testament qui peut désigner aussi l’enseignant, le directeur, le guide., car un seul est votre Chef : Christ.

11Le plus grand parmi vous sera votre serviteur. 12Car celui qui s’élève sera abaissé ; et celui qui s’abaisse sera élevé.

13Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites ! Parce que vous barrez aux autres l’accès au royaume des cieux. Non seulement vous n’y entrez pas vous-mêmes, mais vous empêchez d’entrer ceux qui voudraient le faire !

14[Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites, car vous dépouillez les veuves de leurs biens, tout en faisant de longues prières pour l’apparence. C’est pourquoi votre condamnation n’en sera que plus sévère23.14 Ce verset est absent de plusieurs manuscrits. Voir Mc 12.40..]

15Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites ! Vous parcourez terre et mer pour amener ne fût-ce qu’un seul païen à votre religion, et quand vous l’avez gagné, vous lui faites mériter l’enfer deux fois plus que vous.

16Malheur à vous, guides aveugles ! En effet, vous dites : Si quelqu’un jure « par le Temple », il n’est pas tenu par son serment, mais s’il jure « par l’or du Temple », il doit tenir son serment. 17Insensés et aveugles que vous êtes ! Qu’est-ce qui est plus important : l’or ou le Temple qui rend cet or sacré ? 18Ou bien vous dites : Si quelqu’un jure « par l’autel », il n’est pas tenu par son serment ; mais s’il jure « par l’offrande qui est sur l’autel », il doit tenir son serment. 19Aveugles que vous êtes ! Qu’est-ce qui est plus important : l’offrande ou l’autel qui rend cette offrande sacrée ? 20En fait, celui qui jure « par l’autel », jure à la fois par l’autel et par tout ce qui est dessus. 21Celui qui jure « par le Temple », jure à la fois par le Temple et par celui qui y habite. 22Celui qui jure « par le ciel », jure à la fois par le trône de Dieu et par celui qui y siège.

23Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites ! Vous vous acquittez de la dîme sur la menthe, l’anis et le cumin, mais vous laissez de côté ce qu’il y a de plus important dans la Loi, c’est-à-dire la justice, la compassion et la fidélité23.23 Autre traduction : foi.. Voilà ce qu’il fallait pratiquer, sans négliger le reste.

24Guides aveugles que vous êtes ! Vous filtrez vos boissons pour éliminer le moindre moucheron, mais vous avalez le chameau tout entier.

25Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites ! Vous nettoyez soigneusement l’extérieur de vos coupes et de vos assiettes, mais vous les remplissez du produit de vos vols et de vos désirs incontrôlés. 26Pharisien aveugle, commence donc par purifier l’intérieur de la coupe et de l’assiette, alors l’extérieur sera pur.

27Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites ! Vous êtes comme ces tombeaux crépis de blanc23.27 Toucher un tombeau rendait rituellement impur. C’est pourquoi on les peignait en blanc (couleur de la pureté) afin qu’on ne les touche pas la nuit par inadvertance., qui sont beaux au-dehors. Mais à l’intérieur, il n’y a qu’ossements de cadavres et pourriture. 28Vous de même, à l’extérieur, vous avez l’air d’être justes aux yeux des hommes, mais, à l’intérieur, il n’y a qu’hypocrisie et désobéissance à Dieu.

29Malheur à vous, spécialistes de la Loi et pharisiens hypocrites ! Vous édifiez des tombeaux aux prophètes, vous couvrez d’ornements ceux des justes. 30Vous dites : Si nous avions vécu du temps de nos ancêtres, nous ne nous serions pas associés à eux pour tuer les prophètes. 31En disant cela, vous attestez vous-mêmes que vous êtes bien les descendants de ceux qui ont fait périr les prophètes. 32Eh bien, ce que vos pères ont commencé, portez-le à son comble !

33Serpents, race de vipères ! Comment pouvez-vous penser que vous éviterez le châtiment de l’enfer ? 34En effet, je vais vous envoyer des prophètes, des sages et des spécialistes de l’Ecriture : vous allez tuer ou crucifier les uns, fouetter les autres dans vos synagogues, et les persécuter d’une ville à l’autre, 35pour que retombe sur vous le châtiment qu’appelle le meurtre de tous les innocents, depuis celui d’Abel, le juste, jusqu’à celui de Zacharie, fils de Barachie, que vous avez assassiné entre le Temple et l’autel du sacrifice.

36Oui, vraiment, je vous l’assure : le châtiment mérité par tous ces meurtres retombera sur les hommes de cette génération.

Lamentation sur Jérusalem

(Lc 13.34-35)

37Ah, Jérusalem ! Jérusalem ! Toi qui fais mourir les prophètes et qui lapides ceux que Dieu t’envoie ! Combien de fois j’ai voulu rassembler tes habitants auprès de moi comme une poule rassemble ses poussins sous ses ailes ! Mais vous ne l’avez pas voulu ! 38Maintenant, votre maison va être abandonnée et restera déserte23.38 Certains manuscrits omettent déserte..

39En effet, je vous le déclare : Désormais, vous ne me verrez plus jusqu’à ce que vous disiez : Béni soit celui qui vient au nom du Seigneur23.39 Ps 118.26. Autre traduction : Béni soit, au nom du Seigneur, celui qui vient !!