Mathayo 20 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 20:1-34

Mfano Wa Wafanyakazi Katika Shamba La Mizabibu

120:1 Mt 13:24; 21:28, 33“Kwa maana Ufalme wa Mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba aliyetoka alfajiri ili kwenda kuajiri vibarua kufanya kazi katika shamba lake la mizabibu. 2Baada ya kukubaliana na hao vibarua kuwalipa ujira wa dinari20:2 Dinari moja ilikuwa kama mshahara wa kibarua wa siku moja. moja kwa siku, akawapeleka kwenye shamba lake la mizabibu.

3“Mnamo saa tatu akatoka tena, akawakuta wengine wamesimama sokoni bila kazi. 4Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu, nami nitawalipa chochote kilicho haki yenu.’ 5Kwa hiyo wakaenda.

“Akatoka tena mnamo saa sita na pia saa tisa akafanya vivyo hivyo. 6Mnamo saa kumi na moja akatoka tena akawakuta wengine bado wamesimama bila kazi. Akawauliza, ‘Kwa nini mmesimama hapa kutwa nzima pasipo kufanya kazi?’

7“Wakamjibu, ‘Ni kwa sababu hakuna yeyote aliyetuajiri.’

“Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu.’

820:8 Law 19:13; Kum 24:15“Ilipofika jioni, yule mwenye shamba la mizabibu akamwambia msimamizi, ‘Waite hao vibarua na uwalipe ujira wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho na kuishia na wale walioajiriwa kwanza.’

9“Wale vibarua walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakaja na kila mmoja wao akapokea dinari moja. 10Hivyo wale walioajiriwa kwanza walipofika, walidhani watalipwa zaidi. Lakini kila mmoja wao pia alipokea dinari moja. 1120:11 Yn 4:1Walipoipokea, wakaanza kulalamika dhidi ya yule mwenye shamba, 1220:12 Yn 4:8; Yak 1:11wakisema, ‘Hawa watu walioajiriwa mwisho wamefanya kazi kwa muda wa saa moja tu, nawe umewafanya sawa na sisi ambao tumestahimili taabu na joto lote la mchana kutwa?’

1320:13 Mt 22:12; 26:50“Yule mwenye shamba akamjibu mmoja wao, ‘Rafiki, sijakudhulumu. Je, hukukubaliana nami kwa ujira wa kawaida wa dinari moja? 14Chukua ujira wako na uende. Mimi nimeamua kumlipa huyu mtu aliyeajiriwa mwisho kama nilivyokupa wewe. 1520:15 Kum 15:9; Mk 7:22Je, sina haki yangu kufanya kile nitakacho na mali yangu mwenyewe? Au unaona wivu kwa kuwa nimekuwa mkarimu?’

1620:16 Mt 19:30“Vivyo hivyo, wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”

Yesu Atabiri Tena Kuhusu Kifo Chake

(Marko 10:32-34; Luka 18:31-34)

1720:17 Mk 10:32; Lk 18:31; Yn 12:12Basi Yesu alipokuwa anapanda kwenda Yerusalemu, aliwachukua kando wale wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia, 1820:18 Lk 9:51; Mt 8:20; 16:21; 27:1-2“Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Nao watamhukumu kifo 1920:19 Mdo 2:23; Mt 16:21na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa ili wamdhihaki na kumpiga mijeledi na kumsulubisha msalabani. Naye atafufuliwa siku ya tatu!”

Ombi La Mama Yake Yakobo Na Yohana

(Marko 10:35-45)

2020:20 Mt 4:21; 8:2Kisha mama yao wana wa Zebedayo akamjia Yesu pamoja na wanawe, naye akapiga magoti mbele yake, akamwomba Yesu amfanyie jambo fulani.

2120:21 Mt 19:28Yesu akamuuliza, “Unataka nini?” Akajibu, “Tafadhali, wajalie wanangu hawa ili mmoja aketi upande wako wa kuume, na mwingine upande wako wa kushoto katika Ufalme wako.”

2220:22 Yer 49:12; Yn 18:11Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe nitakachonywea mimi?”

Wakajibu, “Tunaweza.”

2320:23 Mdo 12:2; Ufu 1:9Yesu akawaambia, “Kwa kweli kikombe changu mtakinywea, lakini kuketi upande wangu wa kuume au wa kushoto si langu mimi kuwapa. Nafasi hizo ni za wale ambao wameandaliwa na Baba yangu.”

2420:24 Lk 22:24-25Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, waliwakasirikia hao ndugu wawili. 25Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao. 2620:26 Mt 22:11; Mk 9:35Isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu, 2720:27 Mt 18:4; Mk 9:35naye anayetaka kuwa wa kwanza miongoni mwenu hana budi kuwa mtumwa wenu: 2820:28 Mt 8:20; Isa 42:1; Flp 2:8; Kut 30:2; Ebr 9:28kama vile ambavyo Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”

Yesu Awaponya Vipofu Wawili

(Marko 10:46-52; Luka 18:35-43)

2920:29 Mk 10:46; Lk 18:35Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu ulimfuata. 3020:30 Mt 9:27; 15:22Vipofu wawili walikuwa wameketi kando ya barabara. Waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie!”

31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie.”

32Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”

33Wakamjibu, “Bwana, tunataka kuona.”

34Yesu akawahurumia na kuwagusa macho yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao wakamfuata.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

馬太福音 20:1-34

葡萄園工人的比喻

1耶穌接著說:「因為天國就像一個園主清早去外面請工人到他的葡萄園做工。 2他跟工人講好一天的工錢是一個銀幣,然後派他們去葡萄園。

3「大約上午九點鐘,園主出去看見一些人站在街市上無所事事, 4就對他們說,『你們到我的葡萄園來工作吧,我會給你們合理的工錢。』

5「他們便去了。正午和下午三點鐘,他又出去繼續請人到葡萄園做工。 6到了下午五點鐘的時候,他再次出去,看見還有人閒站在那裡,就問他們,『為什麼你們整天站在這裡無所事事呢?』 7他們回答說,『因為沒有人僱用我們。』園主說,『你們也到我的葡萄園來吧!』

8「到了傍晚,園主對工頭說,『叫工人來領工錢吧,最晚來的先領,最先來的後領。』

9「下午五點來的工人每人得了一個銀幣。 10最早來的工人來領的時候,以為必定可以多得一點工錢,誰知也各得一個銀幣。

11「他們拿著工錢滿腹牢騷地對園主說, 12『那些最晚來的人只工作了一小時,而我們在烈日之下辛苦了一整天,怎麼會領同樣的工錢呢?』

13「園主對他們當中的一個人說,『朋友,我並沒有欠你呀!我們不是講好付你一個銀幣嗎? 14拿著你的工錢走吧。我給那後來的和你一樣的工錢,是我願意。 15難道我不可隨意使用自己的錢嗎?因為我慷慨,你就眼紅嗎?』 16因此,為首的將要殿後,殿後的將要為首。」

耶穌第三次預言自己受難

17在去耶路撒冷的途中,耶穌把十二個門徒帶到一邊,對他們說: 18「你們要留意,我們現在前往耶路撒冷,人子將被交給祭司長和律法教師。他們要判祂死刑, 19把祂交給外族人,受嘲弄、鞭打,被釘在十字架上。但第三天祂必復活。」

一個母親的請求

20當時,西庇太的妻子帶著兩個兒子上前,跪在耶穌面前,有事要求祂。

21耶穌問她:「你要什麼呢?」

她說:「在你的國度,請讓我這兩個兒子一個坐在你右邊,一個坐在你左邊。」

22耶穌回答說:「你們不知道自己在求什麼。我要喝的那一杯,你們能喝嗎?」

他們說:「我們能。」

23耶穌對他們說:「我要喝的那一杯,你們也要喝。不過誰坐在我的左右不是我來定,而是我父為誰預備的,就讓誰坐。」

24其他十個門徒聽見這事,都對他們兄弟二人十分惱火。 25於是,耶穌把他們叫來,說:「外族人有君王統治他們,有大臣管理他們。但你們不可這樣。 26你們中間,誰要當首領,誰就要做大家的僕人; 27誰要居首位,誰就要做大家的奴僕。 28正如人子不是來受人服侍,而是來服侍人,並且犧牲性命,作許多人的贖價。」

治好兩個瞎子

29耶穌和祂的門徒離開耶利哥時,有一大群人跟著祂。 30有兩個瞎子正坐在路旁,聽說耶穌經過,就高聲喊叫:「主啊,大衛的後裔啊,可憐我們吧!」 31眾人責備他們,叫他們不要出聲,他們卻喊得更大聲了:「主啊,大衛的後裔啊,可憐我們吧!」

32耶穌停下腳步,叫了他們來,問他們:「你們要我為你們做什麼?」 33他們說:「主啊,我們想能夠看見。」 34耶穌就動了慈心,摸他們的眼睛,他們立刻得見光明,並跟從了耶穌。