Mathayo 19 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 19:1-30

Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

(Marko 10:1-12)

119:1 Mt 7:28Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ngʼambo ya Mto Yordani. 219:2 Mt 4:23Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.

319:3 Mt 5:31Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”

419:4 Mwa 1:27; 5:2Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke, 519:5 Mwa 2:24; Efe 5:31naye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’? 619:6 1Kor 7:10, 11Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

719:7 Kum 24:1-4; Mt 5:31-32Wakamuuliza, “Kwa nini basi Mose aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?”

8Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo. 919:9 Lk 16:18Mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati naye akaoa mke mwingine, anazini. Naye amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia anazini.”

1019:10 Mit 21:19Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali mtu asioe!”

1119:11 Mit 13:11; 1Kor 7:7-9, 17Yesu akawaambia, “Si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu. 1219:12 1Kor 7:12, 14; 9:5, 15Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”

Yesu Awabariki Watoto Wadogo

(Marko 10:13-16; Luka 18:15-17)

1319:13 Mk 5:23Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wale waliowaleta.

1419:14 Mt 23:34; 18:3; 1Pet 2:2Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio kama hawa.” 15Naye akaweka mikono yake juu yao, na akaondoka huko.

Kijana Tajiri

(Marko 10:17-31; Luka 18:18-30)

1619:16 Mt 25:46; Lk 10:25Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?”

1719:17 Law 18:5Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza habari ya mema? Aliye mwema ni Mmoja tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”

1819:18 Yak 2:11Yule mtu akamuuliza, “Amri zipi?”

Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, 1919:19 Kut 20:12-16; Kum 5:16-20; Law 19:18; Mt 5:43waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.”

20Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?”

2119:21 Mt 5:48; Lk 12:33; Mdo 4:34-35; Mt 6:20Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”

2219:22 Za 62:10Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

Hatari Za Utajiri

2319:23 Mt 13:22; 1Tim 6:9-10Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Amin, nawaambia, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni. 24Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

25Wanafunzi wake waliposikia haya, walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”

2619:26 Zek 8:6; Rum 4:21; Lk 18:28; Kum 33:9; Mt 4:20; Lk 5:11Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”

2719:27 Mt 4:19Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata! Tutapata nini basi?”

2819:28 Mt 20:21; 25:31; Lk 22:28-30; Ufu 3:21; Lk 22:28, 29, 30; 1Kor 6:2, 3; Ufu 2:26Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, wakati wa kufanywa upya vitu vyote, Mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake kitukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli. 2919:29 Mt 6:33; 25:46; Mk 10:29, 30; Lk 18:29, 30Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. 3019:30 Mk 10:33; Lk 10:30Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.

King James Version

Matthew 19:1-30

1And it came to pass, that when Jesus had finished these sayings, he departed from Galilee, and came into the coasts of Judaea beyond Jordan; 2And great multitudes followed him; and he healed them there.

3¶ The Pharisees also came unto him, tempting him, and saying unto him, Is it lawful for a man to put away his wife for every cause? 4And he answered and said unto them, Have ye not read, that he which made them at the beginning made them male and female, 5And said, For this cause shall a man leave father and mother, and shall cleave to his wife: and they twain shall be one flesh? 6Wherefore they are no more twain, but one flesh. What therefore God hath joined together, let not man put asunder. 7They say unto him, Why did Moses then command to give a writing of divorcement, and to put her away? 8He saith unto them, Moses because of the hardness of your hearts suffered you to put away your wives: but from the beginning it was not so. 9And I say unto you, Whosoever shall put away his wife, except it be for fornication, and shall marry another, committeth adultery: and whoso marrieth her which is put away doth commit adultery.

10¶ His disciples say unto him, If the case of the man be so with his wife, it is not good to marry. 11But he said unto them, All men cannot receive this saying, save they to whom it is given. 12For there are some eunuchs, which were so born from their mother’s womb: and there are some eunuchs, which were made eunuchs of men: and there be eunuchs, which have made themselves eunuchs for the kingdom of heaven’s sake. He that is able to receive it, let him receive it.

13¶ Then were there brought unto him little children, that he should put his hands on them, and pray: and the disciples rebuked them. 14But Jesus said, Suffer little children, and forbid them not, to come unto me: for of such is the kingdom of heaven. 15And he laid his hands on them, and departed thence.

16¶ And, behold, one came and said unto him, Good Master, what good thing shall I do, that I may have eternal life? 17And he said unto him, Why callest thou me good? there is none good but one, that is, God: but if thou wilt enter into life, keep the commandments. 18He saith unto him, Which? Jesus said, Thou shalt do no murder, Thou shalt not commit adultery, Thou shalt not steal, Thou shalt not bear false witness, 19Honour thy father and thy mother: and, Thou shalt love thy neighbour as thyself. 20The young man saith unto him, All these things have I kept from my youth up: what lack I yet? 21Jesus said unto him, If thou wilt be perfect, go and sell that thou hast, and give to the poor, and thou shalt have treasure in heaven: and come and follow me. 22But when the young man heard that saying, he went away sorrowful: for he had great possessions.

23¶ Then said Jesus unto his disciples, Verily I say unto you, That a rich man shall hardly enter into the kingdom of heaven. 24And again I say unto you, It is easier for a camel to go through the eye of a needle, than for a rich man to enter into the kingdom of God. 25When his disciples heard it, they were exceedingly amazed, saying, Who then can be saved? 26But Jesus beheld them, and said unto them, With men this is impossible; but with God all things are possible.

27¶ Then answered Peter and said unto him, Behold, we have forsaken all, and followed thee; what shall we have therefore? 28And Jesus said unto them, Verily I say unto you, That ye which have followed me, in the regeneration when the Son of man shall sit in the throne of his glory, ye also shall sit upon twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel. 29And every one that hath forsaken houses, or brethren, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or lands, for my name’s sake, shall receive an hundredfold, and shall inherit everlasting life. 30But many that are first shall be last; and the last shall be first.