Mathayo 14 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 14:1-36

Yohana Mbatizaji Akatwa Kichwa

(Marko 6:14-29; Luka 9:7-9)

114:1 Lk 13:31; 9:7-9; Mdo 12:1Wakati huo, Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za Yesu, 214:2 Mt 3:1akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji; amefufuka kutoka kwa wafu! Hii ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”

314:3 Mt 4:12; 11:2; Lk 3:19-20Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake, 414:4 Law 18:16; 20:21kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode: “Si halali kwako kuwa na huyo mwanamke.” 514:5 Mt 11:19; 21:26; Lk 20:26Herode alitaka sana kumuua Yohana, lakini akaogopa watu, kwa maana walimtambua kuwa ni nabii.

6Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode, 7kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba. 8Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.” 9Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake. 1014:10 Mt 17:12Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani. 11Kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake. 1214:12 Mt 8:2Wanafunzi wa Yohana wakaja na kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha wakaenda wakamwambia Yesu.

Yesu Alisha Wanaume 5,000

(Marko 6:30-44; Luka 9:10-17; Yohana 6:1-14)

1314:13 Mk 6:31-44; Mt 10:23; Mk 6:32; Lk 9:19; Yn 6:13Yesu aliposikia yaliyokuwa yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu kutoka miji. 1414:14 Mt 9:36; 4:23Yesu alipofika kando ya bahari, aliona makutano makubwa ya watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.

1514:15 Mk 6:35; Lk 9:12; Yn 6:5Ilipofika jioni, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na muda sasa umekwisha. Waage makutano ili waende zao vijijini wakajinunulie chakula.”

16Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.”

1714:17 Mt 16:9; 1Sam 9:13; 1Kor 10:16Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”

18Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.” 1914:19 Mt 15:36; 1Sam 9:13; Mt 26:26; Mk 8:6; Lk 9:16; 24:30; Mdo 2:42; 20:7Yesu akaagiza makutano wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia makutano. 2014:20 2Fal 4:44Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili. 21Idadi ya watu waliokula walikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.

Yesu Atembea Juu Ya Maji

(Marko 6:45-52; Yohana 6:15-21)

2214:22 Mk 6:45-46Mara Yesu akawaambia wanafunzi wake waingie kwenye mashua watangulie kwenda ngʼambo ya bahari, wakati yeye alikuwa akiwaaga wale makutano. 2314:23 Lk 3:21; 6:12; 9:18Baada ya kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke yake. 24Wakati huo ile mashua ilikuwa mbali kutoka nchi kavu ikisukwasukwa na mawimbi, kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.

25Wakati wa zamu ya nne ya usiku,14:25 Zamu ya nne ya usiku ni kati ya saa tisa na saa kumi na mbili asubuhi. Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji. 2614:26 Lk 24:37; Ay 9:8Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu, wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga yowe kwa kuogopa.

2714:27 Mt 9:2; Mdo 23:11; Dan 10:12; Mdo 18:9Lakini mara Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”

28Petro akamjibu, “Bwana, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.”

29Yesu akamwambia, “Njoo.”

Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu. 30Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”

3114:31 Mt 6:30Mara Yesu akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”

32Nao walipoingia ndani ya mashua, upepo ukakoma. 3314:33 Za 2:7; Mt 4:3Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Yesu, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”

Yesu Awaponya Wagonjwa Genesareti

(Marko 6:53-56)

34Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti. 35Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. Watu wakamletea wagonjwa wao wote, 3614:36 Mt 9:20-21wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake, nao wote waliomgusa, wakaponywa.

New International Reader’s Version

Matthew 14:1-36

John the Baptist’s Head Is Cut Off

1At that time Herod, the ruler of Galilee and Perea, heard reports about Jesus. 2He said to his attendants, “This is John the Baptist. He has risen from the dead! That is why he has the power to do miracles.”

3Herod had arrested John. He had tied him up and put him in prison because of Herodias. She was the wife of Herod’s brother Philip. 4John had been saying to Herod, “It is against the Law for you to have her as your wife.” 5Herod wanted to kill John. But he was afraid of the people, because they thought John was a prophet.

6On Herod’s birthday the daughter of Herodias danced for Herod and his guests. She pleased Herod very much. 7So he promised to give her anything she asked for. 8Her mother told her what to say. So the girl said to Herod, “Give me the head of John the Baptist on a big plate.” 9The king was very upset. But he thought of his promise and his dinner guests. So he told one of his men to give her what she asked for. 10Herod had John’s head cut off in the prison. 11His head was brought in on a big plate and given to the girl. She then carried it to her mother. 12John’s disciples came and took his body and buried it. Then they went and told Jesus.

Jesus Feeds Five Thousand

13Jesus heard what had happened to John. He wanted to be alone. So he went in a boat to a quiet place. The crowds heard about this. They followed him on foot from the towns. 14When Jesus came ashore, he saw a large crowd. He felt deep concern for them. He healed their sick people.

15When it was almost evening, the disciples came to him. “There is nothing here,” they said. “It’s already getting late. Send the crowds away. They can go and buy some food in the villages.”

16Jesus replied, “They don’t need to go away. You give them something to eat.”

17“We have only five loaves of bread and two fish,” they answered.

18“Bring them here to me,” he said. 19Then Jesus directed the people to sit down on the grass. He took the five loaves and the two fish. He looked up to heaven and gave thanks. He broke the loaves into pieces. Then he gave them to the disciples. And the disciples gave them to the people. 20All of them ate and were satisfied. The disciples picked up 12 baskets of leftover pieces. 21The number of men who ate was about 5,000. Women and children also ate.

Jesus Walks on the Water

22Right away Jesus made the disciples get into the boat. He had them go on ahead of him to the other side of the Sea of Galilee. Then he sent the crowd away. 23After he had sent them away, he went up on a mountainside by himself to pray. Later that night, he was there alone. 24The boat was already a long way from land. It was being pounded by the waves because the wind was blowing against it.

25Shortly before dawn, Jesus went out to the disciples. He walked on the lake. 26They saw him walking on the lake and were terrified. “It’s a ghost!” they said. And they cried out in fear.

27Right away Jesus called out to them, “Be brave! It is I. Don’t be afraid.”

28“Lord, is it you?” Peter asked. “If it is, tell me to come to you on the water.”

29“Come,” Jesus said.

So Peter got out of the boat. He walked on the water toward Jesus. 30But when Peter saw the wind, he was afraid. He began to sink. He cried out, “Lord! Save me!”

31Right away Jesus reached out his hand and caught him. “Your faith is so small!” he said. “Why did you doubt me?”

32When they climbed into the boat, the wind died down. 33Then those in the boat worshiped Jesus. They said, “You really are the Son of God!”

34They crossed over the lake and landed at Gennesaret. 35The men who lived there recognized Jesus. So they sent a message all over the nearby countryside. People brought all those who were sick to Jesus. 36They begged him to let those who were sick just touch the edge of his clothes. And all who touched his clothes were healed.