Mathayo 13 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 13:1-58

Mfano Wa Mpanzi

(Marko 4:1-9; Luka 8:4-8)

113:1 Mt 13:36; 9:28Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari. 213:2 Lk 5:3Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari. 313:3 Lk 8:5Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. 4Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila. 5Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba. 6Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina. 7Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea. 813:8 Mwa 26:12Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini. 913:9 Mt 11:15Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”

Sababu Ya Kufundisha Kwa Mifano

(Marko 4:10-12; Luka 8:9-10)

10Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”

1113:11 Kol 1:27; 1Yn 2:20, 27Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa. 1213:12 Mt 25:29; Lk 19:26Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa. 1313:13 Yer 5:21; Eze 12:2Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano:

“Ingawa wanatazama, hawaoni;

wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.

1413:14 Mt 1:22; 13:35; Eze 12:2; Isa 6:9; Mdo 28:26-28Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema:

“ ‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa;

na pia mtatazama lakini hamtaona.

1513:15 Isa 6:9-10; Rum 11:8Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu;

hawasikii kwa masikio yao,

na wamefumba macho yao.

Wasije wakaona kwa macho yao,

na wakasikiliza kwa masikio yao,

wakaelewa kwa mioyo yao,

na kugeuka nami nikawaponya.’

1613:16 Mt 16:17; Lk 10:23-24Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia. 1713:17 Ebr 11:13; 1Pet 1:10-12Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.

Maelezo Ya Mfano Wa Mbegu

(Marko 4:13-20; Luka 8:11-15)

1813:18 Mk 4:14; Lk 8:11“Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi: 1913:19 Mt 4:23; 5:37Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia. 2013:20 Isa 58:2; Eze 33:31, 32; Yn 5:35Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha. 2113:21 Mt 11:6; 26:31Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa. 2213:22 Mt 19:23; 1Tim 6:9-10, 17Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. 2313:23 Mt 13:8Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”

Mfano Wa Magugu

2413:24 Mt 25:1; Mk 4:26-39Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake. 25Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake. 26Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.

27“Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’

28“Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’

“Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’

29“Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo. 3013:30 Mt 3:12Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’ ”

Mfano Wa Mbegu Ya Haradali

(Marko 4:30-32; Luka 13:18-19)

3113:31 Mt 17:20; Lk 17:6Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake. 3213:32 Za 104:12; Dan 4:12Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”

Mfano Wa Chachu

(Luka 13:20-21)

3313:33 Mt 13:24; Mwa 18:6; Gal 5:9Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”

Sababu Ya Yesu Kutumia Mifano

(Marko 4:33-34)

3413:34 Mk 4:33-34Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano. 3513:35 Za 78:2; 1Kor 2:7Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema:

“Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano;

nitahubiri mambo yaliyofichika

tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”

Ufafanuzi Wa Mfano Wa Magugu

3613:36 Mt 15:15; 13:24-30Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”

3713:37 Mt 8:20Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu. 3813:38 Yn 8:44-45; 1Yn 3:10Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu. 3913:39 Yoe 3:13; Mt 24:3; 28:20; Ufu 14:15Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika.

4013:40 Yn 15:6“Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. 4113:41 Mt 8:20; 24:31Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote. 4213:42 Mt 13:50; 8:12Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno. 4313:43 Dan 12:3; Mt 11:15Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.

Mfano Wa Hazina Iliyofichwa Na Lulu

4413:44 Mt 13:24; Isa 55:1; Flp 3:7-8“Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”

4513:45 Mt 13:24“Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi. 4613:46 Mt 2:4; 3:14, 15; 8:10, 19Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”

Mfano Wa Wavu

4713:47 Mt 13:24; 22:9-10“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina. 48Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa. 4913:49 Mt 25:32Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. 5013:50 Mt 8:12Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”

51Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?”

Wakamjibu, “Ndiyo.”

5213:52 Wim 7:13Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”

Yesu Akataliwa Nazareti

(Marko 6:1-6; Luka 4:16-30)

5313:53 Mt 7:28Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka. 5413:54 Mt 4:23; 7:28Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?” 5513:55 Lk 3:23; Yn 6:42; Mt 12:46“Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 5613:56 Yn 7:15, 52Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?” 5713:57 Yn 6:61; Lk 4:24; Yn 4:44Wakachukizwa naye.

Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”

5813:58 Mk 6:5, 6Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.

New International Version

Matthew 13:1-58

The Parable of the Sower

1That same day Jesus went out of the house and sat by the lake. 2Such large crowds gathered around him that he got into a boat and sat in it, while all the people stood on the shore. 3Then he told them many things in parables, saying: “A farmer went out to sow his seed. 4As he was scattering the seed, some fell along the path, and the birds came and ate it up. 5Some fell on rocky places, where it did not have much soil. It sprang up quickly, because the soil was shallow. 6But when the sun came up, the plants were scorched, and they withered because they had no root. 7Other seed fell among thorns, which grew up and choked the plants. 8Still other seed fell on good soil, where it produced a crop—a hundred, sixty or thirty times what was sown. 9Whoever has ears, let them hear.”

10The disciples came to him and asked, “Why do you speak to the people in parables?”

11He replied, “Because the knowledge of the secrets of the kingdom of heaven has been given to you, but not to them. 12Whoever has will be given more, and they will have an abundance. Whoever does not have, even what they have will be taken from them. 13This is why I speak to them in parables:

“Though seeing, they do not see;

though hearing, they do not hear or understand.

14In them is fulfilled the prophecy of Isaiah:

“ ‘You will be ever hearing but never understanding;

you will be ever seeing but never perceiving.

15For this people’s heart has become calloused;

they hardly hear with their ears,

and they have closed their eyes.

Otherwise they might see with their eyes,

hear with their ears,

understand with their hearts

and turn, and I would heal them.’13:15 Isaiah 6:9,10 (see Septuagint)

16But blessed are your eyes because they see, and your ears because they hear. 17For truly I tell you, many prophets and righteous people longed to see what you see but did not see it, and to hear what you hear but did not hear it.

18“Listen then to what the parable of the sower means: 19When anyone hears the message about the kingdom and does not understand it, the evil one comes and snatches away what was sown in their heart. This is the seed sown along the path. 20The seed falling on rocky ground refers to someone who hears the word and at once receives it with joy. 21But since they have no root, they last only a short time. When trouble or persecution comes because of the word, they quickly fall away. 22The seed falling among the thorns refers to someone who hears the word, but the worries of this life and the deceitfulness of wealth choke the word, making it unfruitful. 23But the seed falling on good soil refers to someone who hears the word and understands it. This is the one who produces a crop, yielding a hundred, sixty or thirty times what was sown.”

The Parable of the Weeds

24Jesus told them another parable: “The kingdom of heaven is like a man who sowed good seed in his field. 25But while everyone was sleeping, his enemy came and sowed weeds among the wheat, and went away. 26When the wheat sprouted and formed heads, then the weeds also appeared.

27“The owner’s servants came to him and said, ‘Sir, didn’t you sow good seed in your field? Where then did the weeds come from?’

28“ ‘An enemy did this,’ he replied.

“The servants asked him, ‘Do you want us to go and pull them up?’

29“ ‘No,’ he answered, ‘because while you are pulling the weeds, you may uproot the wheat with them. 30Let both grow together until the harvest. At that time I will tell the harvesters: First collect the weeds and tie them in bundles to be burned; then gather the wheat and bring it into my barn.’ ”

The Parables of the Mustard Seed and the Yeast

31He told them another parable: “The kingdom of heaven is like a mustard seed, which a man took and planted in his field. 32Though it is the smallest of all seeds, yet when it grows, it is the largest of garden plants and becomes a tree, so that the birds come and perch in its branches.”

33He told them still another parable: “The kingdom of heaven is like yeast that a woman took and mixed into about sixty pounds13:33 Or about 27 kilograms of flour until it worked all through the dough.”

34Jesus spoke all these things to the crowd in parables; he did not say anything to them without using a parable. 35So was fulfilled what was spoken through the prophet:

“I will open my mouth in parables,

I will utter things hidden since the creation of the world.”13:35 Psalm 78:2

The Parable of the Weeds Explained

36Then he left the crowd and went into the house. His disciples came to him and said, “Explain to us the parable of the weeds in the field.”

37He answered, “The one who sowed the good seed is the Son of Man. 38The field is the world, and the good seed stands for the people of the kingdom. The weeds are the people of the evil one, 39and the enemy who sows them is the devil. The harvest is the end of the age, and the harvesters are angels.

40“As the weeds are pulled up and burned in the fire, so it will be at the end of the age. 41The Son of Man will send out his angels, and they will weed out of his kingdom everything that causes sin and all who do evil. 42They will throw them into the blazing furnace, where there will be weeping and gnashing of teeth. 43Then the righteous will shine like the sun in the kingdom of their Father. Whoever has ears, let them hear.

The Parables of the Hidden Treasure and the Pearl

44“The kingdom of heaven is like treasure hidden in a field. When a man found it, he hid it again, and then in his joy went and sold all he had and bought that field.

45“Again, the kingdom of heaven is like a merchant looking for fine pearls. 46When he found one of great value, he went away and sold everything he had and bought it.

The Parable of the Net

47“Once again, the kingdom of heaven is like a net that was let down into the lake and caught all kinds of fish. 48When it was full, the fishermen pulled it up on the shore. Then they sat down and collected the good fish in baskets, but threw the bad away. 49This is how it will be at the end of the age. The angels will come and separate the wicked from the righteous 50and throw them into the blazing furnace, where there will be weeping and gnashing of teeth.

51“Have you understood all these things?” Jesus asked.

“Yes,” they replied.

52He said to them, “Therefore every teacher of the law who has become a disciple in the kingdom of heaven is like the owner of a house who brings out of his storeroom new treasures as well as old.”

A Prophet Without Honor

53When Jesus had finished these parables, he moved on from there. 54Coming to his hometown, he began teaching the people in their synagogue, and they were amazed. “Where did this man get this wisdom and these miraculous powers?” they asked. 55“Isn’t this the carpenter’s son? Isn’t his mother’s name Mary, and aren’t his brothers James, Joseph, Simon and Judas? 56Aren’t all his sisters with us? Where then did this man get all these things?” 57And they took offense at him.

But Jesus said to them, “A prophet is not without honor except in his own town and in his own home.”

58And he did not do many miracles there because of their lack of faith.