Mathayo 11 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 11:1-30

Yesu Na Yohana Mbatizaji

(Luka 7:18-35)

111:1 Mt 7:28; 26:1Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.

211:2 Mt 14:3Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo11:2 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake 311:3 Za 118:26; Ebr 10:37ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”

4Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona: 511:5 Lk 4:18-19; Isa 61:1-2Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. 611:6 Mt 13:21; 26:31Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”

711:7 Mt 3:1-5Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo? 8Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme. 911:9 Lk 1:76; 7:26Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii. 1011:10 Mal 3:1; Lk 7:27Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa:

“ ‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako,

atakayetengeneza njia mbele yako.’

1111:11 Mt 13:17Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana. 1211:12 Lk 16:16; 13:24Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka. 1311:13 Lk 16:16Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana. 1411:14 Mal 4:5; Yn 1:21Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja. 1511:15 Lk 14:35; Ufu 2:7Yeye aliye na masikio, na asikie.

1611:16 Lk 7:31“Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,

1711:17 Mit 29:9“ ‘Tuliwapigia filimbi,

lakini hamkucheza;

tuliwaimbia nyimbo za maombolezo,

lakini hamkuomboleza.’

1811:18 Mt 3:4; Lk 1:15Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’ 1911:19 Mt 9:11Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.” ’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”

Onyo Kwa Miji Isiyotubu

(Luka 10:13-15)

2011:20 Lk 10:11Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu. 2111:21 Mk 8:22; Yn 1:44; Yoe 3:4; Mk 3:8; Yn 3:5-9“Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu. 2211:22 Mt 11:24; 10:15Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi. 2311:23 Mt 4:13; Isa 14:13-15Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.11:23 Kuzimu ni Mahali pa wafu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. 2411:24 Mt 10:15Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”

Hakuna Amjuaye Baba Ila Mwana

(Luka 10:21-22)

2511:25 Lk 23:34; Yn 12:27-28; Mt 13:11; 1Kor 1:26-29Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. 26Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.

2711:27 Mt 28:18; Yn 3:35; 10:15; 17:25-26“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.

Yesu Awaita Waliolemewa Na Mizigo

2811:28 Yn 7:37“Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 2911:29 Flp 2:5; 1Yn 2:6; Za 116:7; Yer 6:16Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. 3011:30 1Yn 5:3Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”

Knijga O Kristu

Matej 11:1-30

Isus i Ivan Krstitelj

(Lk 7:18-30)

1Kad je završio s uputama dvanaestorici učenika, Isus ode poučavati i propovijedati po gradovima.

2Ivan Krstitelj je u tamnici čuo o Kristovim čudesnim djelima, pa pošalje svoje učenike da upitaju Isusa: 3“Jesi li ti zaista onaj koji treba doći ili da čekamo drugoga?”

4Zatim odgovori Ivanovim učenicima: “Idite Ivanu i ispričajte što čujete i vidite: 5slijepcima se vraća vid, hromi hodaju, gubavci ozdravljaju, gluhi čuju, mrtvi ustaju i Radosna vijest se propovijeda siromasima. 6Recite mu i ovo: ‘Blago onome tko se zbog mene ne sablazni!’”

7Kad su otišli, Isus počne govoriti mnoštvu o Ivanu. “Kad ste izišli u pustinju, što ste išli gledati? Samo trsku kako se povija na vjetru? 8Ili ste išli vidjeti raskošno odjevena čovjeka? Ali takvi žive u kraljevskim palačama. 9Ili ste išli vidjeti Božjeg proroka? Da, on je i više od proroka. 10Jer Ivan je čovjek o kojemu u Svetome pismu piše:

‘Gledajte, šaljem pred vas svojega glasnika

i on će vam pripraviti put.’11:10 Malahija 3:1.

11Zaista vam kažem: Od svih ljudi koji su ikada rođeni nije bilo većega od Ivana Krstitelja. Pa ipak, i najmanji u kraljevstvu nebeskomu veći je od njega! 12A od vremena kad je Ivan Krstitelj počeo propovijedati i krstiti pa sve do sada, navala je na kraljevstvo nebesko i siloviti ga prisvajaju. 13Jer svi su proroci i Zakon proricali o Ivanu. 14I, ako ste mi to spremni povjerovati, on je taj drugi Ilija koji je trebao doći.11:14 Vidjeti: Malahija 3:23. 15Slušajte, kad već imate uši!

Isusov sud o suvremenicima

16A s kime da usporedim ovaj naraštaj? On je poput djece koja sjede i igraju se na gradskome trgu, pa jedna drugoj dovikuju:

17‘Veselo smo vam zasvirali,

ali niste htjeli zaplesati.

Onda smo vam zapjevali tužaljke,

ali ni plakati niste htjeli.’

18Jer, došao je Ivan koji je postio i nije pio vino, a oni kažu: ‘Ima zloduha.’ 19Onda sam došao ja, Sin Čovječji. Jedem i pijem, pa sada govore: ‘Izjelica je i pijanac, prijatelj je ubiračima poreza i drugim grešnicima!’ Ali Božja će se mudrost opravdati svojim djelima.”

Sud za nevjernike

(Lk 7:31-35; 10:13-15)

20Tada počne koriti gradove u kojima se zbilo najviše njegovih čudesnih djela zato što se nisu obratili Bogu. 21“Teško tebi, Korozaine! Teško tebi, Betsaido! Jer da su se čudesa koja su se kod vas dogodila zbila u pokvarenima Tiru i Sidonu, oni bi se već odavno obratili u kostrijeti i pepelu. 22Kažem vam da će Tiru i Sidonu na Sudnji dan biti lakše nego vama! 23A ti, Kafarnaume, zar ćeš se do neba uzdignuti? Strovalit ćeš se u pakao. Da su se čudesa koja su se u tebi zbila dogodila u Sodomi, ona bi zaista ostala do danas. 24Kažem vam da će Sodomi biti lakše na Sudnji dan nego vama!”

Isusova molitva zahvale

(Lk 10:21-22)

25Tada Isus reče: “Oče, gospodaru neba i zemlje, slavim te što si to skrio od mudrih i umnih, a objavio malenima. 26Da, Oče, tebi se to svidjelo tako učiniti.

27Moj mi je Otac sve predao. Nitko ne poznaje Sina nego Otac i nitko ne poznaje Oca nego Sin i oni kojima se Sin hoće objaviti.

28Dođite k meni svi koji ste umorni i opterećeni i ja ću vas odmoriti. 29Uzmite na sebe moj jaram i učite od mene jer sam krotka i ponizna srca. Tako ćete naći spokoj svojim dušama. 30Moj je jaram sladak, a moje breme lako.”