Mathayo 1 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 1:1-25

Kumbukumbu Za Ukoo Wa Yesu Kristo

(Luka 3:23-38)

11:1 Rum 1:3; Mwa 22:18; Lk 3:23-38Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:

21:2 Mwa 21:3, 12; 25:26; 29:35; 49:10Abrahamu akamzaa Isaki,

Isaki akamzaa Yakobo,

Yakobo akawazaa Yuda na ndugu zake,

31:3 Mwa 38:27-30; 1Nya 2:5, 9; Rut 4:18-22; 1Nya 2:10-12Yuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari,

Peresi akamzaa Hesroni,

Hesroni akamzaa Aramu,

4Aramu akamzaa Aminadabu,

Aminadabu akamzaa Nashoni,

Nashoni akamzaa Salmoni,

51:5 Rut 4:13-17; Ebr 11:31Salmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu,

Boazi akamzaa Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruthu,

Obedi akamzaa Yese,

61:6 1Sam 16:1; 17:12; 2Sam 12:24Yese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme.

Daudi akamzaa Solomoni, ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria.

71:7 1Nya 3:10-14Solomoni akamzaa Rehoboamu,

Rehoboamu akamzaa Abiya,

Abiya akamzaa Asa,

8Asa akamzaa Yehoshafati,

Yehoshafati akamzaa Yoramu,1:8 Yoramu ndiye Yehoramu, maana yake ni Yehova yu juu.

Yoramu akamzaa Uzia,

9Uzia akamzaa Yothamu,

Yothamu akamzaa Ahazi,

Ahazi akamzaa Hezekia,

101:10 2Fal 20:21; 1Nya 3:13Hezekia akamzaa Manase,

Manase akamzaa Amoni,

Amoni akamzaa Yosia,

111:11 Dan 1:1-2; 2Fal 24:14-16; Yer 27:20; 40:1wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.

121:12 1Nya 3:17-19; Ezr 3:2Baada ya uhamisho wa Babeli:

Yekonia alimzaa Shealtieli,

Shealtieli akamzaa Zerubabeli,

13Zerubabeli akamzaa Abiudi,

Abiudi akamzaa Eliakimu,

Eliakimu akamzaa Azori,

14Azori akamzaa Sadoki,

Sadoki akamzaa Akimu,

Akimu akamzaa Eliudi,

15Eliudi akamzaa Eleazari,

Eleazari akamzaa Matani,

Matani akamzaa Yakobo,

161:16 Lk 1:27; Mt 27:17naye Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa mumewe Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.1:16 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.

17Hivyo, kulikuwepo na jumla ya vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli, na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli hadi Kristo.

Kuzaliwa Kwa Yesu Kristo

(Luka 2:1-7)

181:18 Lk 1:35Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana kuwa na mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 191:19 Kum 24:1Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.

201:20 Lk 1:35Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 211:21 Lk 1:31; Za 130:8; Tit 2:14Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu,1:21 Yesu ni Iesous kwa Kiyunani, na kwa Kiebrania ni Yoshua au Yeshua. Maana yake ni Yehova ni wokovu. kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.”

221:22 Mt 22:15; 17:23; 4:14; Lk 4:21; 21:22; Yn 13:18; 19:24Haya yote yalitukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema: 231:23 Isa 7:14; 8:8-10“Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli”: maana yake, “Mungu pamoja nasi.”

241:24 Mdo 5:19Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake. 251:25 Lk 1:31; 2:7; 2:1; 2:4-7; 1:5Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.

Knijga O Kristu

Matej 1:1-25

Isusovi preci

(Lk 3:23-38)

1Ovo je rodoslovlje Isusa Krista, potomka kralja Davida koji je bio Abrahamov potomak.

2Abrahamu se rodio Izak.

Izaku se rodio Jakov.

Jakovu su se rodili Juda i njegova braća.

3Judi je Tamara rodila Peresa i Zeraha.

Peresu se rodio Hesron,

a Hesronu Ram.

4Ramu se rodi Aminadab.

Aminadabu se rodi Nahšon,

a Nahšonu Salma.

5Salmi je Rahaba rodila Boaza.

Boazu je Ruta rodila Obeda.

Obedu se rodio Jišaj.

6Jišaju se rodio kralj David.

Davidu je bivša Urijina žena rodila Salomona.

7Salomonu se rodio Roboam.

Roboamu se rodio Abija.

Abiji se rodio Asa.

8Asi se rodio Jozafat.

Jozafatu se rodio Joram,

a Joramu Ahazja.

9Ahazji se rodio Jotam,

Jotamu Ahaz,

a Ahazu Ezekija.

10Ezekiji se rodio Manaše,

Manašeu Amon.

Amonu se rodio Jošija.

11Jošiji su se, u vrijeme progonstva u Babilon, rodili Jehonija i njegova braća.

12Poslije progonstva u Babilon

Jehoniji se rodio Šealtiel.

Šealtielu se rodio Zerubabel.

13Zerubabelu se rodio Abiud.

Abiudu se rodio Elijakim,

a Elijakimu Azor.

14Azoru se rodio Sadok.

Sadoku se rodio Akim,

a Akimu Elijud.

15Elijudu se rodio Eleazar.

Eleazaru Matan,

a Matanu Jakov.

16Jakovu se rodio Josip, muž Marije koja je rodila Isusa zvanoga Krist.

17To je, dakle, ukupno četrnaest naraštaja od Abrahama do kralja Davida, četrnaest naraštaja od kralja Davida do progonstva u Babilon i četrnaest naraštaja od progonstva do Krista.

Rođenje Isusa Krista

(Lk 1:26—2:20)

18Evo kako se zbilo rođenje Isusa Krista: Njegova majka Marija bila je zaručena s Josipom. Ali dok je još bila djevica, začela je po Svetome Duhu. 19Kako je njezin muž Josip bio pravedan čovjek i kako ju nije htio javno osramotiti, naumi ju potajice napustiti.

20Razmišljajući o tome, zaspao je te mu se u snu ukaže Božji glasnik. “Josipe, sine Davidov,” reče mu on, “ne oklijevaj uzeti Mariju za ženu! Jer dijete koje nosi začeto je po Svetome Duhu. 21Ona će roditi sina i nazvat ćeš ga Isus (što znači: ‘Gospodin spasava’) jer će spasiti svoj narod od njegovih grijeha.” 22Sve se to dogodilo da bi se obistinilo što je Gospodin rekao po proroku:

23“Slušajte! Djevica će zanijeti!

Rodit će sina koji će se zvati Emanuel”,

(što znači: “Bog je s nama”).

24Kad se Josip probudio, učini kako mu je Božji glasnik zapovjedio—dovede Mariju svojoj kući da mu bude žena. 25Nije joj prišao kao muškarac dok nije rodila sina. A onda mu nadjene ime Isus.