Matendo 9 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 9:1-43

Kuokoka Kwa Sauli

(Matendo 22:6-16; 26:12-18)

19:1 Mdo 8:3Wakati ule ule, Sauli alikuwa bado anazidisha vitisho vya kuua wanafunzi wa Bwana, akamwendea kuhani mkuu, 29:2 Mdo 22:4; 24:14, 22naye akamwomba kuhani mkuu ampe barua za kwenda kwenye masinagogi huko Dameski, ili akimkuta mtu yeyote wa Njia Ile, akiwa mwanaume au mwanamke, aweze kuwafunga na kuwaleta Yerusalemu. 39:3 1Kor 15:8Basi akiwa katika safari yake, alipokaribia Dameski, ghafula nuru kutoka mbinguni ikamwangaza kotekote. 49:4 Isa 6:8; Mt 25:40Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, “Sauli, Sauli, mbona unanitesa?”

59:5 Mdo 9:16Sauli akajibu, “U nani wewe, Bwana?”

Ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu unayemtesa. 69:6 Eze 3:22Sasa inuka uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”

79:7 Yn 12:29; Dan 10:7; Mdo 22:9Watu waliokuwa wakisafiri pamoja na Sauli wakasimama bila kuwa na la kusema, kwa sababu walisikia sauti lakini hawakumwona aliyekuwa akizungumza. 89:8 Mdo 9:18Sauli akainuka kutoka pale chini na alipojaribu kufungua macho yake hakuweza kuona kitu chochote. Basi wakamshika mkono wakamwongoza mpaka Dameski. 9Naye kwa muda wa siku tatu alikuwa kipofu naye hakula wala kunywa chochote.

109:10 Mdo 12:9; 18:9Huko Dameski alikuwepo mwanafunzi mmoja jina lake Anania. Bwana alimwita katika maono, “Anania!”

Akajibu, “Mimi hapa Bwana.”

119:11 Mdo 11:25; 21:39Bwana akamwambia, “Ondoka uende katika barabara iitwayo Nyofu ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu kutoka Tarso, jina lake Sauli, kwa maana wakati huu anaomba, 129:12 Mk 5:23katika maono amemwona mtu aitwaye Anania akija na kuweka mikono juu yake ili apate kuona tena.”

139:13 Flp 1:1; Mdo 8:3Anania akajibu, “Bwana, nimesikia kutoka kwa watu wengi habari nyingi kuhusu mtu huyu na madhara yote aliyowatendea watakatifu wako huko Yerusalemu. 149:14 Mdo 2:21; 9:2, 21Naye amekuja hapa Dameski akiwa na mamlaka kutoka kwa viongozi wa makuhani ili awakamate wote wanaotaja jina lako.”

159:15 Gal 1:15-16; 1Tim 1:12; Efe 3:7-8; Mdo 25:22-23; 26:1Lakini Bwana akamwambia Anania, “Nenda! Mtu huyu ni chombo changu kiteule nilichokichagua, apate kulichukua Jina langu kwa watu wa Mataifa na wafalme wao na mbele ya watu wa Israeli. 169:16 2Kor 11:23-27; 2Tim 1:8Nami nitamwonyesha jinsi impasavyo kuteseka kwa ajili ya Jina langu.”

179:17 Mdo 6:6Kisha Anania akaenda kwenye ile nyumba, akaingia ndani. Akaweka mikono yake juu ya Sauli akasema, “Ndugu Sauli, Bwana Yesu aliyekutokea njiani amenituma kwako ili upate kuona tena na ujazwe Roho Mtakatifu.” 189:18 Mdo 2:38Ghafula vitu kama magamba vikaanguka chini, kutoka machoni mwa Sauli, akapata kuona tena. Akasimama, akabatizwa. 199:19 Mdo 11:26; 26:20Baada ya kula chakula, akapata nguvu tena. Sauli akakaa siku kadhaa pamoja na wanafunzi huko Dameski.

Sauli Ahubiri Dameski

209:20 Mdo 18:4, 19; 19:8; Mt 4:3Papo hapo akaanza kuhubiri kwenye masinagogi kwamba “Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu” 219:21 Mdo 8:3; Gal 1:13, 23Watu wote waliomsikia Sauli walishangaa na kuuliza, “Huyu si yule mtu aliyesababisha maangamizi makuu huko Yerusalemu miongoni mwa watu waliolitaja jina hili? Naye si amekuja hapa kwa kusudi la kuwakamata na kuwapeleka wakiwa wafungwa mbele ya viongozi wa makuhani?” 229:22 Lk 2:11; Mdo 17:3Sauli akazidi kuwa hodari na kuwashangaza Wayahudi walioishi Dameski kwa kuthibitisha kuwa Yesu ndiye Kristo.9:22 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.

239:23 Mdo 20:3; 23:12; 25:3Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi wakafanya shauri kumuua Sauli. 249:24 Mdo 20:3, 19; 23:16, 30Lakini shauri lao likajulikana kwa Sauli. Wayahudi wakawa wanalinda malango yote ya mji, usiku na mchana ili wapate kumuua. 259:25 1Sam 19:12; 2Kor 11:22-33Lakini wafuasi wake wakamchukua usiku wakamshusha akiwa ndani ya kapu kupitia mahali penye nafasi ukutani.

Sauli Huko Yerusalemu

269:26 Mdo 26:20; Gal 1:17-18Sauli alipofika Yerusalemu akajaribu kujiunga na wanafunzi lakini wote walimwogopa, kwa maana hawakuamini kwamba kweli naye alikuwa mwanafunzi. 279:27 Mdo 4:36; 13:2Lakini Barnaba akamchukua, akampeleka kwa wale mitume. Akawaeleza jinsi Sauli akiwa njiani alivyomwona Bwana, jinsi Bwana alivyosema naye na jinsi alivyohubiri kwa ujasiri kwa jina la Yesu huko Dameski. 289:28 Gal 1:18Kwa hiyo Sauli akakaa nao akitembea kwa uhuru kila mahali huko Yerusalemu, akihubiri kwa ujasiri katika jina la Bwana. 299:29 Mdo 6:1; 2Kor 11:26Alinena na kuhojiana na Wayahudi wenye asili ya Kiyunani lakini wao walijaribu kumuua. 309:30 Mdo 1:16; 8:40Wale ndugu walipopata habari wakampeleka hadi Kaisaria, wakamsafirisha kwenda Tarso.

319:31 Mdo 8:1Ndipo kanisa katika Uyahudi wote, Galilaya na Samaria likafurahia wakati wa amani. Likatiwa nguvu, na kwa faraja ya Roho Mtakatifu, idadi yake ikazidi kuongezeka, na likaendelea kudumu katika kumcha Bwana.

Matendo Ya Petro

(9:32–12:25)

Kuponywa Kwa Ainea

329:32 Mdo 9:13; 8:14Petro alipokuwa akisafiri sehemu mbalimbali, alikwenda kuwatembelea watakatifu walioishi huko Lida. 33Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Ainea, ambaye alikuwa amepooza na kwa muda wa miaka minane alikuwa hajaondoka kitandani. 349:34 Mdo 3:6, 16; 4:10Petro akamwambia, “Ainea, Yesu Kristo anakuponya, inuka utandike kitanda chako.” Mara Ainea akainuka. 359:35 Wim 2:1; Isa 65:10; Mdo 2:41; 11:21Watu wote wa Lida na Sharoni walipomwona Ainea akitembea wakamgeukia Bwana.

Petro Amfufua Dorkasi

369:36 Yn 1:3; Mdo 10:5; 1Tim 2:10; Tit 3:8Huko Yafa palikuwa na mwanafunzi jina lake Tabitha (ambalo kwa Kiyunani ni Dorkasi9:36 Tabitha kwa Kiaramu na Dorkasi kwa Kiaramu yote yamaanisha Paa.). Huyu alikuwa mkarimu sana, akitenda mema na kuwasaidia maskini. 379:37 Mdo 1:13; 20:8Wakati huo akaugua, akafa na wakiisha kuuosha mwili wake wakauweka katika chumba cha ghorofani. 389:38 Mdo 11:26Kwa kuwa Yafa hapakuwa mbali sana na Lida, wanafunzi waliposikia kwamba Petro yuko huko waliwatuma watu wawili kwake ili kumwomba, “Tafadhali njoo huku pasipo kukawia.”

399:39 Mdo 6:1; 1Tim 5:3Kwa hiyo Petro akainuka akaenda nao, naye alipowasili, wakampeleka hadi kwenye chumba cha ghorofani alipokuwa amelazwa. Wajane wengi walisimama karibu naye wakilia na kuonyesha majoho na nguo nyingine ambazo Dorkasi alikuwa amewashonea alipokuwa pamoja nao.

409:40 Mt 9:25; Lk 22:41; Mdo 7:60; Lk 7:14Petro akawatoa wote nje ya kile chumba, kisha akapiga magoti akaomba, akaugeukia ule mwili akasema, “Tabitha, inuka.” Akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi. 419:41 Mdo 9:32Petro akamshika mkono akamwinua, ndipo akawaita wale watakatifu na wajane akamkabidhi kwao akiwa hai. 429:42 Yn 11:45; 12:11Habari hizi zikajulikana sehemu zote za Yafa na watu wengi wakamwamini Bwana. 439:43 Mdo 10:6Petro akakaa Yafa kwa siku nyingi akiishi na Simoni mtengenezaji ngozi.

Slovo na cestu

Skutky 9:1-43

Bůh zkřížil plány Kristova nepřítele: Pavlovo obrácení na jeho cestě do Damašku

1Saul se však snažil Ježíšovy následovníky zastrašit a zlikvidovat. 2Vyžádal si od velekněze pověřující listiny pro židovské synagogy v Damašku. Chtěl tam pátrat po křesťanech, mužích i ženách, zatknout je a přivést do Jeruzaléma před soud. 3Vydal se tam se svým doprovodem a byl již před branami Damašku, když ho obklopilo zvláštní světlo z nebe. 4V úleku padl na zem a uslyšel hlas: „Saule, Saule, proč mne pronásleduješ?“ 5Zeptal se: „Ale kdo jsi, pane?“ Pán mu odpověděl: „Já jsem Ježíš a ty mne pronásleduješ v mých učednících. Je to stejné, jako bys chtěl hlavou rozbít zeď.“ Saul zlomený hrůzou řekl: „Pane, čekám na tvoje rozkazy.“

6A Pán k němu: „Vstaň, jdi do města a tam se dozvíš další.“ 7Muži ze Saulova doprovodu stáli v úžasu; něco slyšeli, ale nevěděli, s kým jejich velitel mluví. 8Saul se zvedl ze země, protíral si oči, ale neviděl nic; oslepl. Uchopili ho za ruce, a tak ho odvedli do Damašku. 9Tři dny trvala jeho slepota a po celou tu dobu nic nejedl ani nepil.

10V Damašku žil věřící muž jménem Ananiáš. Tomu se zjevil Pán Ježíš a oslovil ho jménem. Ananiáš se zeptal: „Pane, co si přeješ?“ 11Pán mu řekl: „Vstaň a jdi do Přímé ulice. Tam v Judově domě najdeš Saula, který pochází z Tarsu. 12Při modlitbě tě uviděl, jak k němu jdeš, kladeš na něj ruce a on znovu dostává zrak. Zjevil jsem mu i tvoje jméno.“ 13Ale Ananiáš namítl: „Pane, o tom muži kdekdo vypráví, jak mnoho zla způsobil mezi tvými věrnými v Jeruzalémě. 14I sem prý přišel s pověřením předních kněží, aby pozatýkal všechny, kdo vyznávají tvoje jméno.“ 15Pán mu však řekl: „Přesto jdi. Já jsem si ho vybral za svůj zvláštní nástroj, který bude šířit zvuk mého jména nejen mezi židy, ale i mezi pohany a donese ho až před panovníky. 16A ukáži mu, že pro moje jméno hodně vytrpí.“

17Ananiáš šel a v určeném domě nalezl Saula. Položil na něj ruce a řekl: „Saule, bratře, posílá mě k tobě Pán Ježíš, který se ti ukázal na cestě k nám. Máš zase prohlédnout a být naplněn svatým Duchem.“ 18A tu jako by se protrhla tma a Saul okamžitě prohlédl. Povstal a dal se pokřtít. 19Potom se posilnil jídlem.

Kristův odpůrce se stává jeho zastáncem

Připojil se k damašským následovníkům Krista a byl s nimi několik dní. 20Brzy však začal chodit také do synagog a veřejně hlásal, že Ježíš je Boží Syn. 21Všichni posluchači se divili a říkali: „Cožpak to není ten, kdo tak tvrdě v Jeruzalémě pronásledoval Ježíšovy vyznavače? I sem přece přišel, aby je pochytal a předvedl před veleradu.“ 22Avšak Saula tím neumlčeli. Naopak on umlčoval damašské židy a dokazoval jim, že Ježíš je Mesiáš. 23Když už to trvalo dlouho, domluvili se někteří z nich, že ho zabijí. 24Saul se dozvěděl o těch úkladech, ale oni dali hlídat ve dne i v noci městské brány, aby jim neunikl. 25Tak ho křesťané nakonec spustili v koši přes hradby.

26Saul přišel zpět do Jeruzaléma a pokoušel se připojit k Ježíšovým následovníkům, ale všichni se ho báli; nevěřili, že by se mohl tak změnit. 27Tu se ho ujal Barnabáš, přivedl ho k apoštolům a všechno jim vyprávěl: Jak se Pán na cestě ukázal Saulovi a mluvil s ním a jak potom Saul v Damašku bez bázně hlásal Ježíše. 28A tak ho věřící v Jeruzalémě přijali mezi sebe a také zde směle mluvil o Pánu Ježíši. 29Zvláště rád diskutoval s řecky mluvícími židy. Ti mu nakonec také ukládali o život. 30Když se to dozvěděli bratři, odvedli ho tajně do Césareje a odtud ho poslali do rodného Tarsu.

31Saulovým obrácením nastala pro sbory v Judsku, Galileji i v Samařsku pokojná doba vnitřního budování a života v oddanosti Bohu. Duch svatý mezi nimi působil, takže rostly i počtem.

Petr uzdravil Eneáše a Tabitu

32Petr podnikl okružní cestu po všech sborech a přišel tak i k věřícím v Lyddě. 33Navštívil tam jakéhosi Eneáše, který byl už osm let ochrnutý upoután na lůžko. 34Petr mu řekl: „Eneáši, Ježíš Kristus tě uzdravuje. Vstaň a skliď si své lůžko!“ A on hned vstal. 35Když to viděli obyvatelé Lyddy a Sáronu, uvěřili v Pána Ježíše.

36Nedaleko Lyddy, v Joppe, žila věřící žena jménem Tabita, řecky Dorkas. Byla známá tím, jak z lásky podporovala chudé. 37Právě v těch dnech však onemocněla a zemřela. Připravili ji k pohřbu a zatím uložili do místnosti v patře. 38Věřící se doslechli, že Petr je v Lyddě, a poslali k němu s prosbou, aby k nim hned přišel. 39Petr šel s posly a ti ho vedli přímo nahoru do domu. Tam byl zástup plačících vdov, ty ho obklopily a ukazovaly mu šaty, které jim ušila jejich milá Dorkas. 40Petr požádal, aby všichni odešli, poklekl a modlil se. Po chvíli se obrátil k mrtvému tělu a řekl: „Tabito, vstaň!“ Ona otevřela oči, uviděla Petra a posadila se. 41Petr jí podal ruku a pomohl jí vstát. Pak zase zavolal všechny nahoru a odevzdal jim Tabitu živou. 42To se rychle rozkřiklo po celém Joppe a mnoho lidí uvěřilo v Pána Ježíše. 43Petr pak bydlel dlouho v Joppe v domě koželuha Šimona.