Matendo 7 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 7:1-60

Hotuba Ya Stefano

1Ndipo kuhani mkuu akamuuliza Stefano, “Je, mashtaka haya ni ya kweli?”

27:2 Za 29:3; Mwa 11:31; 15:7; Mdo 22:1Stefano akajibu, “Ndugu zangu na baba zangu, nisikilizeni! Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Abrahamu, alipokuwa bado yuko Mesopotamia, kabla hajaishi Harani, 37:3 Mwa 12:1-5; 48:4akamwambia, ‘Ondoka kutoka nchi yako na kutoka kwa jamii yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.’

47:4 Mwa 12:5; Ebr 11:13“Hivyo aliondoka katika nchi ya Wakaldayo akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu akamtoa huko akamleta katika nchi hii ambayo mnaishi sasa. 57:5 Mwa 17:8; 26:3; 12:7; Ebr 11:13Mungu hakumpa urithi wowote katika nchi hii, hakumpa hata mahali pa kuweka wayo mmoja. Bali Mungu alimwahidi kuwa yeye na uzao wake baada yake wangeirithi hii nchi, ingawa wakati huo Abrahamu hakuwa na mtoto. 67:6 Kut 1:8-11; 12:40Mungu akasema naye hivi: ‘Wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.’ 77:7 Mwa 15:13-14; Kut 3:12Mungu akasema, ‘Lakini mimi nitaliadhibu taifa watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka katika nchi hiyo na wataniabudu mahali hapa.’ 87:8 Mwa 17:9-14; 21:2-4; 29:31-35; 35:16-18, 22-26Ndipo akampa Abrahamu Agano la tohara. Naye Abrahamu akamzaa Isaki na kumtahiri siku ya nane. Baadaye Isaki akamzaa Yakobo, naye Yakobo akawazaa wale wazee wetu kumi na wawili.

97:9 Mwa 37:4-11; 37:28; 39:2, 21-23; Hag 2:4“Kwa sababu wazee wetu walimwonea wivu Yosefu ndugu yao, walimuuza kama mtumwa huko Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye. 107:10 Mwa 41:37-41; Za 105:20-22Akamwokoa kutoka mateso yote yaliyompata, tena akampa kibali na hekima aliposimama mbele ya Farao, mfalme wa Misri, ambaye alimweka kuwa mtawala juu ya Misri na juu ya jumba lote la kifalme.

117:11 Mwa 41:54; 42:5“Basi kukawa na njaa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa, nao baba zetu wakawa hawana chakula. 127:12 Mwa 42:12Lakini Yakobo aliposikia kwamba kuna nafaka huko Misri, aliwatuma baba zetu, wakaenda huko kwa mara yao ya kwanza. 137:13 Mwa 45:1-4Walipokwenda mara ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, nao ndugu zake Yosefu wakajulishwa kwa Farao. 147:14 Mwa 45:9-10; Kut 1:5; Kum 10:22Ndipo Yosefu akawatuma kumleta Yakobo baba yake pamoja na jamaa yake yote, jumla yao walikuwa watu sabini na watano. 157:15 Mwa 49:33Hivyo Yakobo akaenda Misri ambako yeye na baba zetu walifia. 167:16 Mwa 50:13; Yos 24:32Miili yao ilirudishwa Shekemu na kuzikwa katika kaburi ambalo Abrahamu alinunua kutoka kwa wana wa Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.

177:17 Kut 1:6-7; Za 105:24“Lakini wakati ulipokuwa unakaribia wa kutimizwa kwa ile ahadi ambayo Mungu alikuwa amempa Abrahamu, watu wetu walizidi kuongezeka sana huko Misri. 187:18 Kut 1:8Ndipo mfalme mwingine ambaye hakujua lolote kuhusu Yosefu akatawala Misri. 197:19 Kut 1:8-22Huyu mfalme akawatendea watu wetu hila na kuwatesa baba zetu kwa kuwalazimisha wawatupe watoto wao wachanga ili wafe.

207:20 Kut 2:2; Ebr 11:23“Wakati huo Mose alizaliwa, naye hakuwa mtoto wa kawaida. Akalelewa nyumbani kwa baba yake kwa muda wa miezi mitatu. 217:21 Kut 2:3-10Waliposhindwa kumficha zaidi, wakamweka nje mtoni na binti Farao akamchukua akamtunza kama mtoto wake mwenyewe. 227:22 1Fal 4:30; Isa 19:11Mose akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa mtu hodari kwa maneno na matendo.

237:23 Kut 2:11; 2:12“Mose alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kuwatembelea ndugu zake Waisraeli. 24Aliona mmoja wao akidhulumiwa na Mmisri, akamtetea yule aliyeonewa, akampiga yule Mmisri akamuua kulipiza kisasi. 25Mose alidhani kuwa ndugu zake wangetambua kwamba Mungu anamtumia ili kuwaokoa, lakini wao hawakuelewa. 267:26 Kut 2:13Siku iliyofuata Mose aliwakuta Waisraeli wawili wakigombana, akajaribu kuwapatanisha kwa kuwaambia, ‘Enyi watu, ninyi ni ndugu, mbona mnataka kudhulumiana?’

277:27 Lk 12:14; Mdo 4:7; Mwa 19:9; Hes 16; 13; Kut 2:14“Lakini yule mtu aliyekuwa akimdhulumu mwenzake akamsukuma Mose kando, akamuuliza, ‘Ni nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi juu yetu? 28Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?’ 297:29 Kut 2:11-15Mose aliposikia maneno haya, alikimbilia huko Midiani alikokaa kama mgeni, naye akapata watoto wawili wa kiume.

307:30 Kut 3:2; 2:15, 22; 18:3, 4“Basi baada ya miaka arobaini kupita, malaika wa Mungu akamtokea Mose jangwani karibu na Mlima Sinai katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto. 317:31 Kut 3:1-5Alipoona mambo haya, alishangaa yale maono. Aliposogea ili aangalie kwa karibu, akaisikia sauti ya Bwana, ikisema: 327:32 Mt 22:32; Ebr 11:16; Mdo 3:13; Kut 3:6‘Mimi ndimi Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo.’ Mose alitetemeka kwa hofu na hakuthubutu kutazama.

337:33 Kut 3:5-6; Yos 5:15“Ndipo Bwana akamwambia, ‘Vua viatu vyako kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu. 347:34 Kut 3:7-10Hakika nimeona mateso ya watu wangu huko Misri. Nimesikia kilio chao cha uchungu, nami nimeshuka ili niwaokoe. Basi sasa njoo, nami nitakutuma Misri.’

357:35 Mdo 7:27; Kut 2:14“Huyu ndiye Mose yule waliyemkataa wakisema, ‘Ni nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi juu yetu?’ Alikuwa ametumwa na Mungu mwenyewe kuwa mtawala na mkombozi wao, kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kile kichaka. 367:36 Kut 12:41; 33; 1; 14:21Aliwaongoza wana wa Israeli kutoka Misri, baada ya kufanya ishara na maajabu mengi huko Misri, katika Bahari ya Shamu,7:36 Yaani Bahari ya Mafunjo. na katika jangwa kwa muda wa miaka arobaini.

377:37 Kum 18:15, 18; Mdo 3:22; Mt 15:5“Huyu ndiye yule Mose aliyewaambia Waisraeli, ‘Mungu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe.’ 387:38 Kut 19:17; Law 27:34; Ebr 4:12; Rum 3:2Huyu ndiye yule Mose aliyekuwa katika kusanyiko huko jangwani, ambaye malaika alisema naye pamoja na baba zetu kwenye Mlima Sinai, naye akapokea maneno yaliyo hai ili atupatie.

397:39 Hes 14:3-4“Lakini baba zetu walikataa kumtii Mose, badala yake wakamkataa na kuielekeza mioyo yao Misri tena. 407:40 Kut 32:1-23Wakamwambia Aroni, ‘Tufanyie miungu watakaotuongoza, kwa maana mtu huyu Mose aliyetutoa nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.’ 417:41 Za 106:19-20; Ufu 9:20Huu ni ule wakati walitengeneza sanamu katika umbo la ndama, wakailetea sadaka kufanya maadhimisho kwa ajili ya kile kitu walichokitengeneza kwa mikono yao wenyewe. 427:42 Yos 24:20; Isa 63:19; Yer 19:13Ndipo Mungu akageuka, akawaacha waabudu jeshi lote la mbinguni, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Manabii:

“ ‘Je, mliniletea dhabihu na sadaka

kwa miaka arobaini kule jangwani,

ee nyumba ya Israeli?

437:43 Amo 5:25-27La, ninyi mliinua madhabahu ya Moleki,

na nyota ya mungu wenu Refani,

vinyago mlivyotengeneza ili kuviabudu.

Kwa hiyo nitawapeleka mbali’ kuliko Babeli.

447:44 Kut 38:21; Hes 17:7; Kut 25:8“Baba zetu walikuwa na lile Hema la Ushuhuda huko jangwani. Lilikuwa limetengenezwa kama Mungu alivyokuwa amemwelekeza Mose, kulingana na kielelezo alichoona. 457:45 Yos 23:9; Za 132:1-5Baba zetu wakiisha kulipokea hema kwa kupokezana wakiongozwa na Yoshua katika milki ya nchi kutoka kwa yale mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao, nalo likadumu katika nchi mpaka wakati wa Daudi, 467:46 1Fal 8:17; Za 44:2ambaye alipata kibali kwa Mungu, naye akaomba kwamba ampatie Mungu wa Yakobo maskani. 477:47 1Fal 6:1-38; 1Nya 17:12; 2Nya 3:1Lakini alikuwa Solomoni ndiye alimjengea Mungu nyumba.

487:48 1Fal 8:27; 2Nya 2:6“Hata hivyo, Yeye Aliye Juu Sana hakai kwenye nyumba zilizojengwa kwa mikono ya wanadamu. Kama nabii alivyosema:

497:49 Mt 5:32-35; Isa 66:1, 2; Mt 23:22“ ‘Mbingu ni kiti changu cha enzi,

nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu.

Mtanijengea nyumba ya namna gani?

asema Bwana.

Au mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?

507:50 Isa 66:1-2; Lk 23:34Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote?’

517:51 Kut 32:9; 33:3-5; Law 26:41; Yer 9:26“Enyi watu wenye shingo ngumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, daima hamwachi kumpinga Roho Mtakatifu, kama walivyofanya baba zenu. 527:52 2Nya 36:16; Mt 5:12; Mdo 3:14; 1The 2:15Je, kuna nabii gani ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki. Nanyi sasa mmekuwa wasaliti wake na wauaji. 537:53 Gal 3:19; Ebr 2:2Ninyi ndio mlipokea sheria zilizoletwa kwenu na malaika, lakini hamkuzitii.”

Stefano Apigwa Mawe

547:54 Mt 5:33; Mdo 5:33Waliposikia haya wakaghadhibika, wakamsagia meno. 557:55 Mk 16:19; Mdo 6:5; Lk 22:69Lakini yeye Stefano, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alikaza macho mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, na Yesu akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu. 567:56 Mt 3:16; 8:20; Eze 1:1; Mdo 10:11; Dan 7:13Akasema, “Tazameni! Naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama upande wa kuume wa Mungu.”

57Lakini wao wakapiga kelele kwa sauti kubwa, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja. 587:58 Lk 4:29; Law 24:14-16; Kum 13; 9; Mdo 22:20; 8:1Wakamtupa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka mavazi yao miguuni mwa kijana mmoja ambaye jina lake aliitwa Sauli.

597:59 Za 31:5; Lk 23:46Walipokuwa wakimpiga mawe, Stefano aliomba, “Bwana Yesu, pokea roho yangu.” 607:60 Lk 22:41; Mdo 9:40; Mt 5:44Kisha akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa akasema, “Bwana usiwahesabie dhambi hii.” Baada ya kusema hayo, akalala.

New International Version

Acts 7:1-60

Stephen’s Speech to the Sanhedrin

1Then the high priest asked Stephen, “Are these charges true?”

2To this he replied: “Brothers and fathers, listen to me! The God of glory appeared to our father Abraham while he was still in Mesopotamia, before he lived in Harran. 3‘Leave your country and your people,’ God said, ‘and go to the land I will show you.’7:3 Gen. 12:1

4“So he left the land of the Chaldeans and settled in Harran. After the death of his father, God sent him to this land where you are now living. 5He gave him no inheritance here, not even enough ground to set his foot on. But God promised him that he and his descendants after him would possess the land, even though at that time Abraham had no child. 6God spoke to him in this way: ‘For four hundred years your descendants will be strangers in a country not their own, and they will be enslaved and mistreated. 7But I will punish the nation they serve as slaves,’ God said, ‘and afterward they will come out of that country and worship me in this place.’7:7 Gen. 15:13,14 8Then he gave Abraham the covenant of circumcision. And Abraham became the father of Isaac and circumcised him eight days after his birth. Later Isaac became the father of Jacob, and Jacob became the father of the twelve patriarchs.

9“Because the patriarchs were jealous of Joseph, they sold him as a slave into Egypt. But God was with him 10and rescued him from all his troubles. He gave Joseph wisdom and enabled him to gain the goodwill of Pharaoh king of Egypt. So Pharaoh made him ruler over Egypt and all his palace.

11“Then a famine struck all Egypt and Canaan, bringing great suffering, and our ancestors could not find food. 12When Jacob heard that there was grain in Egypt, he sent our forefathers on their first visit. 13On their second visit, Joseph told his brothers who he was, and Pharaoh learned about Joseph’s family. 14After this, Joseph sent for his father Jacob and his whole family, seventy-five in all. 15Then Jacob went down to Egypt, where he and our ancestors died. 16Their bodies were brought back to Shechem and placed in the tomb that Abraham had bought from the sons of Hamor at Shechem for a certain sum of money.

17“As the time drew near for God to fulfill his promise to Abraham, the number of our people in Egypt had greatly increased. 18Then ‘a new king, to whom Joseph meant nothing, came to power in Egypt.’7:18 Exodus 1:8 19He dealt treacherously with our people and oppressed our ancestors by forcing them to throw out their newborn babies so that they would die.

20“At that time Moses was born, and he was no ordinary child.7:20 Or was fair in the sight of God For three months he was cared for by his family. 21When he was placed outside, Pharaoh’s daughter took him and brought him up as her own son. 22Moses was educated in all the wisdom of the Egyptians and was powerful in speech and action.

23“When Moses was forty years old, he decided to visit his own people, the Israelites. 24He saw one of them being mistreated by an Egyptian, so he went to his defense and avenged him by killing the Egyptian. 25Moses thought that his own people would realize that God was using him to rescue them, but they did not. 26The next day Moses came upon two Israelites who were fighting. He tried to reconcile them by saying, ‘Men, you are brothers; why do you want to hurt each other?’

27“But the man who was mistreating the other pushed Moses aside and said, ‘Who made you ruler and judge over us? 28Are you thinking of killing me as you killed the Egyptian yesterday?’7:28 Exodus 2:14 29When Moses heard this, he fled to Midian, where he settled as a foreigner and had two sons.

30“After forty years had passed, an angel appeared to Moses in the flames of a burning bush in the desert near Mount Sinai. 31When he saw this, he was amazed at the sight. As he went over to get a closer look, he heard the Lord say: 32‘I am the God of your fathers, the God of Abraham, Isaac and Jacob.’7:32 Exodus 3:6 Moses trembled with fear and did not dare to look.

33“Then the Lord said to him, ‘Take off your sandals, for the place where you are standing is holy ground. 34I have indeed seen the oppression of my people in Egypt. I have heard their groaning and have come down to set them free. Now come, I will send you back to Egypt.’7:34 Exodus 3:5,7,8,10

35“This is the same Moses they had rejected with the words, ‘Who made you ruler and judge?’ He was sent to be their ruler and deliverer by God himself, through the angel who appeared to him in the bush. 36He led them out of Egypt and performed wonders and signs in Egypt, at the Red Sea and for forty years in the wilderness.

37“This is the Moses who told the Israelites, ‘God will raise up for you a prophet like me from your own people.’7:37 Deut. 18:15 38He was in the assembly in the wilderness, with the angel who spoke to him on Mount Sinai, and with our ancestors; and he received living words to pass on to us.

39“But our ancestors refused to obey him. Instead, they rejected him and in their hearts turned back to Egypt. 40They told Aaron, ‘Make us gods who will go before us. As for this fellow Moses who led us out of Egypt—we don’t know what has happened to him!’7:40 Exodus 32:1 41That was the time they made an idol in the form of a calf. They brought sacrifices to it and reveled in what their own hands had made. 42But God turned away from them and gave them over to the worship of the sun, moon and stars. This agrees with what is written in the book of the prophets:

“ ‘Did you bring me sacrifices and offerings

forty years in the wilderness, people of Israel?

43You have taken up the tabernacle of Molek

and the star of your god Rephan,

the idols you made to worship.

Therefore I will send you into exile’7:43 Amos 5:25-27 (see Septuagint) beyond Babylon.

44“Our ancestors had the tabernacle of the covenant law with them in the wilderness. It had been made as God directed Moses, according to the pattern he had seen. 45After receiving the tabernacle, our ancestors under Joshua brought it with them when they took the land from the nations God drove out before them. It remained in the land until the time of David, 46who enjoyed God’s favor and asked that he might provide a dwelling place for the God of Jacob.7:46 Some early manuscripts the house of Jacob 47But it was Solomon who built a house for him.

48“However, the Most High does not live in houses made by human hands. As the prophet says:

49“ ‘Heaven is my throne,

and the earth is my footstool.

What kind of house will you build for me?

says the Lord.

Or where will my resting place be?

50Has not my hand made all these things?’7:50 Isaiah 66:1,2

51“You stiff-necked people! Your hearts and ears are still uncircumcised. You are just like your ancestors: You always resist the Holy Spirit! 52Was there ever a prophet your ancestors did not persecute? They even killed those who predicted the coming of the Righteous One. And now you have betrayed and murdered him— 53you who have received the law that was given through angels but have not obeyed it.”

The Stoning of Stephen

54When the members of the Sanhedrin heard this, they were furious and gnashed their teeth at him. 55But Stephen, full of the Holy Spirit, looked up to heaven and saw the glory of God, and Jesus standing at the right hand of God. 56“Look,” he said, “I see heaven open and the Son of Man standing at the right hand of God.”

57At this they covered their ears and, yelling at the top of their voices, they all rushed at him, 58dragged him out of the city and began to stone him. Meanwhile, the witnesses laid their coats at the feet of a young man named Saul.

59While they were stoning him, Stephen prayed, “Lord Jesus, receive my spirit.” 60Then he fell on his knees and cried out, “Lord, do not hold this sin against them.” When he had said this, he fell asleep.