Matendo 5 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 5:1-42

Anania Na Safira

1Lakini mtu mmoja jina lake Anania pamoja na mkewe Safira waliuza kiwanja. 25:2 Mdo 4:35-37Huku mkewe akijua kikamilifu, Anania alificha sehemu ya fedha alizopata, akaleta kiasi kilichobaki na kukiweka miguuni pa mitume.

35:3 Mt 4:10; Yn 13:2, 27Petro akamuuliza, “Anania, mbona Shetani ameujaza moyo wako ili kumwambia uongo Roho Mtakatifu, ukaficha sehemu ya fedha ulizopata kutokana na kiwanja? 45:4 Kum 23:22; Law 6:2Je, kabla hujauza hicho kiwanja si kilikuwa mali yako? Hata baada ya kukiuza, fedha ulizopata si zilikuwa kwenye uwezo wako? Kwa nini basi umewaza hila hii moyoni mwako kufanya jambo kama hili? Wewe hukumwambia uongo mwanadamu bali Mungu.”

55:5 Za 5:6; Mdo 5:10Anania aliposikia maneno haya akaanguka chini na kufa. Hofu kuu ikawapata wote waliosikia jambo lililokuwa limetukia. 65:6 Yn 19:40Vijana wakaja, wakaufunga mwili wake sanda, wakamchukua nje kumzika.

7Saa tatu baadaye mkewe Anania akaingia, naye hana habari ya mambo yaliyotukia. 85:8 Mdo 5:2Petro akamuuliza, “Niambie, je, mliuza kiwanja kwa thamani hii?” Akajibu, “Ndiyo, tuliuza kwa thamani hiyo.”

95:9 Mdo 5:3; Mt 4:7Ndipo Petro akamwambia, “Imekuwaje mkakubaliana kumjaribu Roho wa Bwana? Tazama! Nyayo za vijana waliomzika mumeo ziko mlangoni, wewe nawe watakuchukua nje.”

105:10 Mdo 5:5, 6Saa ile ile akaanguka chini miguuni mwake na kufa. Nao wale vijana wakaingia, wakamkuta amekufa, wakamchukua wakamzika kando ya mumewe. 115:11 Mdo 19:7Hofu kuu ikalipata kanisa lote pamoja na watu wote waliosikia juu ya matukio haya.

Mitume Waponya Wengi

125:12 Yn 4:48; Mdo 2:43; 4:32; Yn 10:23Mitume wakafanya ishara nyingi na miujiza miongoni mwa watu. Walioamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Solomoni. 135:13 Mdo 2:47; 4:21; Yn 9:22; 12:42; 19; 18Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kuambatana nao ijapokuwa waliheshimiwa sana na watu. 145:14 Mdo 2:41, 47; 6; 7; 21:20Hata hivyo, waliomwamini Bwana wakazidi kuongezeka, wanaume na wanawake. 155:15 Mdo 19; 12Hata wakawa wanawaleta wagonjwa na kuwalaza kwenye magodoro na kwenye vitanda barabarani ili yamkini Petro akipita kivuli chake kiwaguse baadhi yao. 165:16 Mt 8:16; Mk 16:17Pia watu wakakusanyika kutoka miji iliyokuwa karibu na Yerusalemu, wakileta wagonjwa na watu walioteswa na pepo wachafu. Hao wote wakaponywa.

Mitume Washtakiwa

175:17 Mdo 15:5; 4:1Kisha kuhani mkuu na wenzake wote waliokuwa pamoja naye, waliokuwa wa kundi la Masadukayo, wakajawa na wivu. 18Wakawakamata mitume na kuwatia gerezani. 195:19 Kut 3:2; Mt 28:2; Mdo 16:26Lakini wakati wa usiku, malaika wa Bwana akaja, akafungua milango ya gereza na akawatoa nje. Akawaambia, 205:20 Yn 6:63-68; 17:3; 1Yn 5:11“Nendeni, mkasimame Hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya uzima huu mpya.”

215:21 Mdo 4:5-6; Mt 5:22Waliposikia haya wakaenda Hekaluni alfajiri wakaendelea kufundisha watu.

Kuhani mkuu na wale waliokuwa pamoja nao walipowasili, alikusanya baraza na wazee wote wa Israeli wakatuma wale mitume waletwe kutoka gerezani. 225:22 Mdo 12:18, 19Lakini wale walinzi wa Hekalu walipokwenda gerezani hawakuwakuta mitume mle. Kwa hiyo wakarudi na kutoa habari. 23Wakasema, “Tumekuta milango ya gereza imefungwa sawasawa na askari wa gereza wamesimama nje ya mlango, lakini tulipofungua milango hakuwepo mtu yeyote ndani.” 245:24 Lk 22:4; Mdo 4:1Basi mkuu wa walinzi wa Hekalu na viongozi wa makuhani waliposikia haya, wakafadhaika na kushangaa sana kwa ajili yao kwamba jambo hili litakuwaje.

25Ndipo mtu mmoja akaja akawaambia, “Tazameni watu mliowatia gerezani wako Hekaluni wakiwafundisha watu.” 265:26 Mdo 4:21Ndipo yule mkuu wa walinzi wa Hekalu wakaenda pamoja na askari wakawaleta wale mitume, lakini bila ghasia kwa sababu waliogopa kupigwa mawe na watu.

275:27 Mt 5:22Wakiisha kuwaleta mitume wakawaamuru kusimama mbele ya baraza ili kuhani mkuu awahoji. 285:28 Mdo 4:18; Mt 23:35; 27:25“Tuliwaonya kwa nguvu msifundishe kwa jina hili, lakini ninyi mmeijaza Yerusalemu yote mafundisho yenu na tena mmekusudia kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”

295:29 Kut 1:17; Mdo 4:19Petro na wale mitume wengine wakajibu, “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. 305:30 Mdo 3:13; 2:24; Gal 3:13; 1Pet 2:24Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu kutoka kwa wafu, ambaye ninyi mlimuua kwa kumtundika kwenye msalaba. 315:31 Mk 16:19; Lk 2:11; Mdo 2:23Mungu alimtukuza, akamweka mkono wake wa kuume kuwa Kiongozi na Mwokozi ili awape Israeli toba na msamaha wa dhambi. 325:32 Lk 24:48; Yn 15:26Nasi tu mashahidi wa mambo haya, vivyo hivyo na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii.”

335:33 Mdo 2:37; 7:54Wale wajumbe wa baraza la wazee waliposikia haya, walijawa na ghadhabu, wakataka kuwaua mitume. 345:34 Mdo 22:3; Lk 2:46; 5:17Lakini Farisayo mmoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, akasimama mbele ya baraza akaamuru mitume watolewe nje kwa muda. 35Ndipo alipowaambia wajumbe wa baraza, “Enyi watu wa Israeli, fikirini kwa uangalifu mnayotaka kuwatendea watu hawa. 365:36 Mdo 21:38Kwa maana wakati uliopita, aliinuka mtu mmoja jina lake Theuda, alijidai kuwa yeye ni mtu maarufu, akapata wafuasi wapatao 400 walioambatana naye. Lakini aliuawa, na wafuasi wake wote wakatawanyika, wakawa si kitu. 375:37 Lk 2:2Baada yake, alitokea Yuda Mgalilaya wakati wa kuorodhesha watu, naye akaongoza kundi la watu kuasi. Yeye pia aliuawa, nao wafuasi wake wakatawanyika. 385:38 Lk 15:13Kwa hiyo, kwa habari ya jambo hili nawashauri, jiepusheni na watu hawa. Waacheni waende zao! Kwa maana kama kusudi lao na shughuli yao imetokana na mwanadamu, haitafanikiwa. 395:39 2Nya 13:12; Mdo 11:17Lakini ikiwa imetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwazuia watu hawa. Badala yake mtajikuta mnapigana na Mungu.”

405:40 Mt 10:17Wakapokea ushauri wa Gamalieli. Wakawaita mitume ndani, wakaamuru wachapwe mijeledi, kisha wakawaagiza wasinene tena kwa jina la Yesu, wakawaachia waende zao.

415:41 Mt 5:12; Mk 15:21Nao mitume wakatoka nje ya baraza, wakiwa wamejaa furaha kwa sababu wamehesabiwa kustahili kupata aibu kwa ajili ya jina la Yesu. 425:42 Mdo 2:46; 4:20, 29; 9:22; 13:32Kila siku, Hekaluni na nyumba kwa nyumba, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema kwamba Yesu ndiye Kristo.5:42 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.

Slovo na cestu

Skutky 5:1-42

Soud nad Ananiášem a Zafirou

1Svůj pozemek prodal i jistý Ananiáš a jeho manželka Zafira. 2Ti se však domluvili, že část získaných peněz odnese Ananiáš apoštolům a bude je vydávat za celou částku. 3Ale Petr mu řekl: „Ananiáši, tento podvod ti poradil sám ďábel. Tím, že se nás snažíš obelstít a vydáváš částku za celek, obelháváš vlastně svatého Ducha. 4Vždyť to pole bylo tvoje a mohl sis je klidně nechat. I stržené peníze patřily tobě a nikdo z nás by ti nevyčítal, kdyby sis je byl všechny ponechal. Co tě to jen napadlo? Chtěl jsi podvést nejen lidi, ale samotného Boha.“

5Když to Ananiáš vyslechl, zhroutil se mrtev na zem. Všechny, kdo se to dověděli, naplnila hrůza. 6Několik mladých mužů vyneslo Ananiášovo tělo, aby ho pohřbili.

7Asi za tři hodiny přišla také Zafira, která netušila, co se mezitím odehrálo. 8Petr se jí zeptal: „Poslyš, Zafiro, prodali jste to pole za tolik a za tolik?“ Odpověděla: „Ano, jistě za tolik.“ 9Na to Petr: „Proč jste se tak smluvili? To jste chtěli podvést Božího Ducha? Právě se vracejí chlapci, kteří pohřbili tvého muže. A tebe stihne stejný trest jako Ananiáše.“ 10Zafira padla k Petrovým nohám a zemřela. Ti mládenci právě vešli do dveří a hned museli jít vykonat ještě druhý pohřeb do stejného hrobu. 11To se samozřejmě rychle rozkřiklo nejen mezi věřícími, ale i mezi ostatními lidmi a všemi to hluboce otřáslo.

Apoštolové uzdravují mnoho nemocných

12Apoštolové se pravidelně scházeli v Šalomounově podloubí v chrámu, 13-14kde se je nikdo neodvážil rušit. Stali se totiž mezi jeruzalémským lidem velmi populárními pro divy a zázračná uzdravení, která se děla jejich prostřednictvím. 15Došlo to tak daleko, že když měl jít Petr do chrámu nebo zpět, lidé podél cesty připravovali nemocné na rohožích a nosítkách, aby na ně padl alespoň Petrův stín. 16Dokonce z širého okolí snášeli do Jeruzaléma nemocné a pomatené a všichni byli uzdraveni. A mnoho dalších mužů a žen uvěřilo Pánu a připojilo se k církvi.

Apoštolové čelí tvrdé opozici

17Toto hnutí vyvolalo žárlivost a strach především u nejvyššího kněze a jeho přívrženců – saducejů. Ti totiž učili, že se žádné zázraky – a natož vzkříšení z mrtvých – nedějí. 18Dali proto apoštoly zatknout a uvěznit, tentokrát do městské věznice. 19Boží anděl však v noci otevřel dveře žaláře, vyvedl apoštoly ven a povzbudil je: 20„Nebojte se, jděte zase do chrámu a říkejte lidem, jak mohou dosáhnout věčného života!“ 21Poslechli a už na úsvitě byli v chrámu a učili.

Mezitím velekněz a jeho stoupenci svolali zasedání velerady a přikázali, aby byli apoštolové předvedeni. 22Chrámoví strážci však našli vězení prázdné, vrátili se a podali hlášení: 23„Věznice je v naprostém pořádku, dveře zamčené, strážní u nich drželi řádně hlídku, ale když jsme odemkli, uvnitř nikdo nebyl.“ 24Velekněz, velitel a jeho chrámová stráž vyslechli tu zprávu a byli zmateni. Nevěděli, co si o tom mají myslet. 25Vtom někdo přiběhl a hlásil: „Ti muži, které jste včera uvěznili, jsou zase v chrámu a klidně mluví k lidem!“ 26Velitel tam spěchal se stráží, ale neodvážili se žádného násilí, protože lid by je ukamenoval. 27Apoštolové však s nimi šli dobrovolně před veleradu.

Velekněz je obvinil: 28„Copak jsme vám nezakázali Ježíšovo jméno veřejně vyslovit? Jak to, že jste naplnili celý Jeruzalém svými výklady o něm a nás označujete za jeho vrahy?“ 29Petr promluvil jménem ostatních apoštolů: „Boha přece musíme poslechnout víc než lidi. 30To Bůh našich praotců vzkřísil z mrtvých Ježíše, kterého jste vy zabili potupným způsobem na římském kříži. 31Bůh mu však svěřil veliký úkol Mesiáše a Vysvoboditele. Jenom on může Izraeli odpustit jeho hříchy, když se mu ovšem pokoříte. 32My jsme svědkové všeho, co říkáme. Jasným dokladem vám může být moc svatého Ducha, kterou Bůh dal těm, kdo si už dali říct a učinili pokání.“

33To ovšem veleradu rozzuřilo a ozvalo se volání, aby byli apoštolové popraveni. 34O slovo se však přihlásil známý farizejský učitel zákona Gamaliel, muž značné autority, a dal pokyn, aby na chvíli obžalované odvedli. 35Pak oslovil veleradu: „Izraelci, dobře si rozmyslete, co chcete udělat s těmito lidmi. 36Vzpomínáte na rozruch kolem Teuda? Ten ze sebe dělal velkou osobnost a shromáždil na čtyři sta přívrženců. Když však zemřel, jeho lidé se rozprchli a všechno utichlo. 37Nebo vzpomeňte na povstání Judy z Galileje za sčítání lidu. Měl hodně následovníků, ale i on zahynul a jeho tlupa se rozptýlila. 38A tak vám radím, nechte ty lidi prostě na pokoji. Jestli je to zase nějaké lidské hnutí, brzo se rozpadne. 39Stojí-li však za tím Bůh, nic proti tomu nezmůžete a vlastně byste se snažili bojovat s Bohem.“ Dali na jeho radu. 40Opět předvedli apoštoly, vyměřili jim obvyklý trest bičování a znovu jim přísně zakázali hlásat cokoliv o Ježíšovi a šířit jeho učení. Pak je propustili.

41Apoštolové šli ze soudu a radovali se, že byli vyznamenáni těžkostmi a utrpením pro jméno Pána Ježíše. 42Učili i nadále každý den o Ježíšovi a jak v soukromí, tak na veřejnosti ho prohlašovali za Božího Syna.