Matendo 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 3:1-26

Petro Amponya Mlemavu Kwa Jina La Yesu

13:1 Lk 22:8; Mdo 2:46; Za 55:17; Mdo 10:30Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri. 23:2 Mdo 14:8; Lk 16:20; Yn 9:8Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni. 3Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka. 43:4 Mdo 14:9Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.” 5Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.

63:6 Mk 1:24; Mdo 14:10Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!” 7Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu. 83:8 Isa 35:6; Mdo 14:10Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu. 93:9 Mdo 4:16, 21Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu, 103:10 Mdo 3:2; Yn 9:8wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.

Petro Anashuhudia Kuwa Yesu Anaponya

113:11 Lk 22:8; Yn 10:23; Mdo 5:12Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni. 12Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea? 133:13 Mdo 7:32; 22:14; Mt 27; 2; Lk 23:4Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake. 143:14 Mdo 4:27; 7:52; Mk 15:11; Lk 23:18-25Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji. 153:15 Mdo 2:24; 2:32Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya. 163:16 Mt 9:22; Mdo 4:10; 14:9Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.

173:17 Lk 23:34; Mdo 13:27“Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu. 183:18 Mdo 17:2-3; Lk 24:27; Mdo 26:22-27Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo3:18 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. atateswa. 193:19 Za 5:11; Mdo 2:38Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana, 203:20 Lk 2:11naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu. 213:21 Mdo 1:11; Mt 17:11; Lk 1:70Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. 223:22 Kum 18:15-18; Mdo 7:37Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia. 233:23 Kum 18:19; Law 23:29Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’

243:24 Lk 24:27“Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi. 253:25 Mdo 2:39; Rum 9:4-5; Mwa 22:18; 28:14Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’ 263:26 Mdo 2:24; 13:46; Rum 1:16Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”

New International Version – UK

Acts 3:1-26

Peter heals a lame beggar

1One day Peter and John were going up to the temple at the time of prayer – at three in the afternoon. 2Now a man who was lame from birth was being carried to the temple gate called Beautiful, where he was put every day to beg from those going into the temple courts. 3When he saw Peter and John about to enter, he asked them for money. 4Peter looked straight at him, as did John. Then Peter said, ‘Look at us!’ 5So the man gave them his attention, expecting to get something from them.

6Then Peter said, ‘Silver or gold I do not have, but what I do have I give you. In the name of Jesus Christ of Nazareth, walk.’ 7Taking him by the right hand, he helped him up, and instantly the man’s feet and ankles became strong. 8He jumped to his feet and began to walk. Then he went with them into the temple courts, walking and jumping, and praising God. 9When all the people saw him walking and praising God, 10they recognised him as the same man who used to sit begging at the temple gate called Beautiful, and they were filled with wonder and amazement at what had happened to him.

Peter speaks to the onlookers

11While the man held on to Peter and John, all the people were astonished and came running to them in the place called Solomon’s Colonnade. 12When Peter saw this, he said to them: ‘Fellow Israelites, why does this surprise you? Why do you stare at us as if by our own power or godliness we had made this man walk? 13The God of Abraham, Isaac and Jacob, the God of our fathers, has glorified his servant Jesus. You handed him over to be killed, and you disowned him before Pilate, though he had decided to let him go. 14You disowned the Holy and Righteous One and asked that a murderer be released to you. 15You killed the author of life, but God raised him from the dead. We are witnesses of this. 16By faith in the name of Jesus, this man whom you see and know was made strong. It is Jesus’ name and the faith that comes through him that has completely healed him, as you can all see.

17‘Now, fellow Israelites, I know that you acted in ignorance, as did your leaders. 18But this is how God fulfilled what he had foretold through all the prophets, saying that his Messiah would suffer. 19Repent, then, and turn to God, so that your sins may be wiped out, that times of refreshing may come from the Lord, 20and that he may send the Messiah, who has been appointed for you – even Jesus. 21Heaven must receive him until the time comes for God to restore everything, as he promised long ago through his holy prophets. 22For Moses said, “The Lord your God will raise up for you a prophet like me from among your own people; you must listen to everything he tells you. 23Anyone who does not listen to him will be completely cut off from their people.”3:23 Deut. 18:15,18,19

24‘Indeed, beginning with Samuel, all the prophets who have spoken have foretold these days. 25And you are heirs of the prophets and of the covenant God made with your fathers. He said to Abraham, “Through your offspring all peoples on earth will be blessed.”3:25 Gen. 22:18; 26:4 26When God raised up his servant, he sent him first to you to bless you by turning each of you from your wicked ways.’