Matendo 20 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 20:1-38

Paulo Apita Makedonia Na Uyunani

120:1 Mdo 11:26; 16:9Baada ya zile ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawatia moyo, akawaaga, akaanza safari kwenda Makedonia. 2Alipita katika sehemu zile, akinena na watu maneno mengi ya kuwatia moyo. Ndipo hatimaye akawasili Uyunani, 320:3 2Kor 11:26; 1The 2:15-16; Mdo 16:9ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa anakaribia kuanza safari kwa njia ya bahari kwenda Shamu, kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yake, aliamua kurudi kupitia njia ya Makedonia. 420:4 Mdo 19:29; 17:19-29; 16:1; Efe 6:21; 2Tim 4:12; Mdo 21:29; 2Tim 4:20Paulo alikuwa amefuatana na Sopatro mwana wa Piro, Mberoya, Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike na Gayo, mtu wa Derbe, Timotheo pamoja na Tikiko na Trofimo kutoka sehemu ya Asia. 520:5 Mdo 16:10; 16:8Hawa watu walitutangulia wakaenda kutungojea Troa. 620:6 Mdo 16:2; 18:8Lakini sisi tukasafiri kwa njia ya bahari kwa siku tano kutoka Filipi baada ya siku za Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, nasi tukaungana na wengine huko Troa, ambako tulikaa kwa siku saba.

Eutiko Afufuliwa Huko Troa

720:7 1Kor 16:2; Ufu 1:10Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. Paulo akaongea na watu, naye kwa kuwa alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliendelea kuongea mpaka usiku wa manane. 820:8 Mdo 1:13Kwenye chumba cha ghorofani walimokuwa wamekutania kulikuwa na taa nyingi. 9Kijana mmoja jina lake Eutiko, alikuwa amekaa dirishani, wakati Paulo alipokuwa akihubiri kwa muda mrefu, alipatwa na usingizi mzito, akaanguka kutoka ghorofa ya tatu, wakamwinua akiwa amekufa. 1020:10 1Fal 17:21; 2Fal 4:34; Mt 9:23; 24Paulo akashuka chini, akajitupa juu yake na kumkumbatia, akasema, “Msishtuke, uzima wake bado umo ndani yake.” 1120:11 Mdo 20:7; Mt 14:19Kisha Paulo akapanda tena ghorofani, akamega mkate na kula. Baada ya kuongea mpaka mapambazuko, akaondoka. 12Watu wakamrudisha yule kijana nyumbani akiwa hai nao wakafarijika sana.

Paulo Awaaga Wazee Wa Efeso

13Tukatangulia melini tukasafiri mpaka Aso ambako tungempakia Paulo. Alikuwa amepanga hivyo kwa maana alitaka kufika kwa miguu. 14Alipotukuta huko Aso, tulimpakia melini, tukasafiri wote mpaka Mitilene. 1520:15 2Tim 4:20Kutoka huko tuliendelea kwa njia ya bahari, na kesho yake tukafika mahali panapokabili Kio. Siku iliyofuata tukavuka kwenda Samo, na kesho yake tukawasili Mileto. 1620:16 Mdo 18:19; 19:21; 2:1; 1Kor 16:8Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi huko sehemu za Asia, kwa sababu alikuwa anatamani kama ikiwezekana kufika Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.

1720:17 Mdo 11:30Paulo akiwa Mileto, alituma mjumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa waje wakutane naye. 1820:18 Mdo 18:19, 21; 19:1-4Walipofika akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua jinsi nilivyoishi katikati yenu muda wote tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia. 19Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi nikivumilia taabu na mapingamizi yaliyonipata kutokana na hila za Wayahudi. 2020:20 Za 40:10Mnajua kwamba sikusita kuhubiri jambo lolote ambalo lingekuwa la kuwafaa ninyi, lakini nilifundisha hadharani na nyumba kwa nyumba. 2120:21 Mdo 18:5; 2:38; Efe 1:15; Kol 2:5Nimewashuhudia Wayahudi na Wayunani kwamba inawapasa kumgeukia Mungu kwa kutubu dhambi na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.

2220:22 Mdo 19:21“Nami sasa nimesukumwa na Roho, ninakwenda Yerusalemu wala sijui ni nini kitakachonipata huko. 2320:23 Mdo 21:4; 9:16Ila ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu amenionya kuwa vifungo na mateso vinaningoja. 2420:24 Mdo 21:13; 2Kor 4:1; Gal 1:1; Tit 1:3Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, kama kuyamaliza mashindano na kukamilisha ile kazi Bwana Yesu aliyonipa, yaani, kazi ya kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.

2520:25 Mt 4:23; Mdo 20:38; Rum 15:23“Nami sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja miongoni mwenu ambaye nimemhubiria Ufalme wa Mungu katika kwenda kwangu huku na huko, atakayeniona uso tena. 2620:26 Mdo 18:6Kwa hiyo nawatangazia leo, sina hatia ya damu ya mtu awaye yote. 27Kwa kuwa sikusita kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu. 2820:28 1Pet 5:2Jilindeni nafsi zenu na mlilinde lile kundi lote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi wake. Lichungeni kanisa lake Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe. 2920:29 Mt 7:15Najua kwamba baada yangu kuondoka, mbwa mwitu wakali watakuja katikati yenu ambao hawatalihurumia kundi. 3020:30 Mdo 11:26Hata kutoka miongoni mwenu watainuka watu na kuupotosha ukweli ili wawavute wanafunzi wawafuate. 3120:31 Mdo 19:10Hivyo jilindeni! Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuacha kamwe kuwaonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana.

3220:32 Mdo 14:23; Mt 25:34; Ebr 9:15; Mdo 26:18“Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa. 3320:33 1Sam 12:3; 1The 2:5Sikutamani fedha wala dhahabu wala vazi la mtu yeyote. 3420:34 Mdo 18:3Ninyi wenyewe mnajua kwamba mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami. 3520:35 Rum 15:1; 1Kor 9:12; 2Kor 11:9, 12; 12:13; Efe 4:28; 1The 4:11; 2The 3:8Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa njia hii ya kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wadhaifu, mkikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe jinsi alivyosema, ‘Ni heri kutoa kuliko kupokea.’ ”

3620:36 Lk 22:41; Mdo 9:40Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba. 3720:37 Lk 15:20Wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kumbusu, 38Kilichowahuzunisha zaidi ni kwa sababu ya yale maneno aliyosema kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Wakaenda naye mpaka kwenye meli.

New International Reader’s Version

Acts 20:1-38

Paul Travels Through Macedonia and Greece

1All the trouble came to an end. Then Paul sent for the believers. After encouraging them, he said goodbye. He then left for Macedonia. 2He traveled through that area, speaking many words of hope to the people. Finally he arrived in Greece. 3There he stayed for three months. He was just about to sail for Syria. But some Jews were making plans against him. So he decided to go back through Macedonia. 4Sopater, son of Pyrrhus, from Berea went with him. Aristarchus and Secundus from Thessalonica, Gaius from Derbe, and Timothy went too. Tychicus and Trophimus from Asia Minor also went with him. 5These men went on ahead. They waited for us at Troas. 6But we sailed from Philippi after the Feast of Unleavened Bread. Five days later we joined the others at Troas. We stayed there for seven days.

Eutychus Is Raised From the Dead at Troas

7On the first day of the week we met to break bread and eat together. Paul spoke to the people. He kept on talking until midnight because he planned to leave the next day. 8There were many lamps in the room upstairs where we were meeting. 9A young man named Eutychus was sitting in a window. He sank into a deep sleep as Paul talked on and on. Sound asleep, Eutychus fell from the third floor. When they picked him up from the ground, he was dead. 10Paul went down and threw himself on the young man. He put his arms around him. “Don’t be alarmed,” he told them. “He’s alive!” 11Then Paul went upstairs again. He broke bread and ate with them. He kept on talking until daylight. Then he left. 12The people took the young man home. They were greatly comforted because he was alive.

Paul Says Goodbye to the Ephesian Elders

13We went on ahead to the ship. We sailed for Assos. There we were going to take Paul on board. He had planned it this way because he wanted to go to Assos by land. 14So he met us there. We took him on board and went on to Mitylene. 15The next day we sailed from there. We arrived near Chios. The day after that we crossed over to Samos. We arrived at Miletus the next day. 16Paul had decided to sail past Ephesus. He didn’t want to spend time in Asia Minor. He was in a hurry to get to Jerusalem. If he could, he wanted to be there by the day of Pentecost.

17From Miletus, Paul sent for the elders of the church at Ephesus. 18When they arrived, he spoke to them. “You know how I lived the whole time I was with you,” he said. “From the first day I came into Asia Minor, 19I served the Lord with tears and without pride. I served him when I was greatly tested. I was tested by the evil plans of the Jews who disagreed with me. 20You know that nothing has kept me from preaching whatever would help you. I have taught you in public and from house to house. 21I have told both Jews and Greeks that they must turn away from their sins to God. They must have faith in our Lord Jesus.

22“Now I am going to Jerusalem. The Holy Spirit compels me. I don’t know what will happen to me there. 23I only know that in every city the Spirit warns me. He tells me that I will face prison and suffering. 24But my life means nothing to me. My only goal is to finish the race. I want to complete the work the Lord Jesus has given me. He wants me to tell others about the good news of God’s grace.

25“I have spent time with you preaching about the kingdom. I know that none of you will ever see me again. 26So I tell you today that I am not guilty if any of you don’t believe. 27I haven’t let anyone keep me from telling you everything God wants you to do. 28Keep watch over yourselves. Keep watch over all the believers. The Holy Spirit has made you leaders over them. Be shepherds of God’s church. He bought it with his own blood. 29I know that after I leave, wild wolves will come in among you. They won’t spare any of the sheep. 30Even men from your own people will rise up and twist the truth. They want to get the believers to follow them. 31So be on your guard! Remember that for three years I never stopped warning you. Night and day I warned each of you with tears.

32“Now I trust God to take care of you. I commit you to the message about his grace. It can build you up. Then you will share in what God plans to give all his people. 33I haven’t longed for anyone’s silver or gold or clothing. 34You yourselves know that I have used my own hands to meet my needs. I have also met the needs of my companions. 35In everything I did, I showed you that we must work hard and help the weak. We must remember the words of the Lord Jesus. He said, ‘It is more blessed to give than to receive.’ ”

36Paul finished speaking. Then he got down on his knees with all of them and prayed. 37They all wept as they hugged and kissed him. 38Paul had said that they would never see him again. That’s what hurt them the most. Then they went with him to the ship.