Matendo 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 2:1-47

Kushuka Kwa Roho Mtakatifu

12:1 Law 23:15-16; 1Kor 16:18; Mdo 1:14Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja. 22:2 Mdo 4:31Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi. 32:3 Mt 3:11Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao. 42:4 Mk 16:17; 1Kor 12:10Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.

52:5 Lk 2:25; Mdo 8:2Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu. 6Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 72:7 Mdo 1:11Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya? 8Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa? 92:9 Mdo 18:2; 1Pet 1:1; 2Kor 1:8; Ufu 1:4Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia, 102:10 Mdo 16:6; 18:23; 14:24; Mt 27:32Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi, 11Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.” 12Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”

132:13 1Kor 14:23; Efe 5:18Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”

Petro Ahutubia Umati

14Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize. 152:15 1The 5:7Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi! 162:16 Yoe 2:28-32La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:

172:17 Eze 39:29; Yn 7:37-39; Mdo 21:9“ ‘Katika siku za mwisho, asema Mungu,

nitamimina Roho wangu

juu ya wote wenye mwili.

Wana wenu na binti zenu watatabiri,

vijana wenu wataona maono,

na wazee wenu wataota ndoto.

182:18 Mdo 21:9-12; 1Kor 12:10, 28; 14:1Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake,

katika siku zile nitamimina Roho wangu,

nao watatabiri.

192:19 Yoe 2:30, 31; Lk 21:11Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni,

na ishara chini duniani:

damu, moto, na mawimbi ya moshi.

202:20 Mt 24:29Jua litakuwa giza

na mwezi utakuwa mwekundu kama damu,

kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana

iliyo tukufu.

212:21 Yoe 2:28-32; Rum 10:13Na kila mtu atakayeliitia

jina la Bwana, ataokolewa.’

222:22 Yn 4:48; Mdo 10:38; Yn 3:2“Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo. 232:23 Isa 53:10; Lk 22:22; 24:20; Mt 16:21Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani. 242:24 Rum 8:11; Ebr 13:20; Yn 20:9Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti. 252:25 Za 16:8Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye:

“ ‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima.

Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,

sitatikisika.

26Kwa hiyo moyo wangu unafurahia,

na ulimi wangu unashangilia;

mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.

272:27 Mdo 13:35Kwa maana hutaniacha kaburini,

wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.

282:28 Za 16:8-11Umenionyesha njia za uzima,

utanijaza na furaha mbele zako.’

292:29 Mdo 7:8-9; 1Fal 2:10; Neh 3:16“Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo. 302:30 2Sam 7:12; Mt 1:1; Za 132:11; Lk 1:32, 69; Rum 1:3; 2Tim 2:8Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi. 312:31 Za 16:10; Mdo 13:35Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo,2:31 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. 322:32 Mdo 1:8; 2:24; Lk 24:48Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo. 332:33 Flp 2:9; Mk 16:19; Yn 14:26; Mdo 10:45; Yn 15:26Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia. 342:34 Za 110:1; Mt 22:44; 1Kor 15:25; Efe 1:20; Ebr 1:13Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema,

“ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu:

“Keti mkono wangu wa kuume,

352:35 Za 110:1; Mt 22:44hadi nitakapowaweka adui zako

chini ya miguu yako.” ’

362:36 Lk 2:11; Mdo 5:31; Mt 28:18“Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”

Waumini Waongezeka

372:37 Lk 3:10-14; Mdo 16:30Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”

382:38 Mdo 22:16; Kol 2:12; Yer 36:3Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 392:39 Isa 44:3; 66:23; 57:19; Efe 2:13Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”

402:40 Kum 32:5; Flp 2:15Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.” 412:41 Mdo 2:47; 4:4; 5:14; 9:31, 35, 42; 11:21, 24; 14:1, 21Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.

Ushirika Wa Waumini

422:42 Mdo 1:14Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali. 432:43 Mdo 5:12Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume. 442:44 Mdo 4:32Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika. 452:45 Mt 19:21; Lk 12:33Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake. 462:46 Lk 24:53; Mdo 3:1; 20:7; Mt 14:19Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe, 472:47 Rum 14:18; Mdo 5:14wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

使徒行传 2:1-47

圣灵降临

1五旬节那天,门徒聚集在一起。 2忽然,天上发出一阵响声,好像狂风呼啸而过,充满了他们所在的房子, 3又有火焰般的舌头显现出来,分别落在各人的头上。 4大家都被圣灵充满,得到圣灵所赐的才能,说起别的语言来。

5当时耶路撒冷住着从各国回来的虔诚的犹太人。 6众人听见这阵响声便赶过来,听见门徒在说他们各自的语言,都十分纳闷, 7惊诧地说:“看啊!这些说话的不都是加利利人吗? 8怎么会说我们各自的语言呢? 9我们这里有帕提亚人、玛代人、以拦人,以及住在美索不达米亚犹太加帕多迦本都亚细亚10弗吕迦旁非利亚埃及和靠近古利奈利比亚的人,还有从罗马来的犹太人和改信犹太教的人、 11克里特人和阿拉伯人。我们都听见他们在用我们各自的语言诉说上帝的伟大!” 12他们都大感惊奇和困惑,彼此议论说:“这到底是怎么回事?”

13有些人就讥笑说:“他们不过是被新酒灌醉了!”

彼得讲道

14彼得和其他十一位使徒都站起来,他大声对众人说:“各位犹太同胞和住在耶路撒冷的人啊,请留心听!我告诉你们这是怎么回事。 15你们以为这些人是醉了,其实不是,因为现在才早上九点钟。 16你们眼前看见的正是先知约珥所说的,

17“‘上帝说,在末后的日子,

我要将我的灵浇灌所有的人,

你们的儿女要说预言,

青年要见异象,

老人要做异梦。

18那时,我要将我的灵浇灌我的奴仆和婢女,

他们都要说预言。

19在天上,我要显异兆;

在地上,我要行神迹,有血、有火、有浓烟。

20太阳要变得昏暗,

月亮要变得血红。

这都要发生在主伟大荣耀的日子来临以前。

21那时,凡求告主名的,都必得救。’

22“各位以色列人啊,请留心听。上帝借着拿撒勒人耶稣在你们中间行了异能、奇事和神迹,以证明拿撒勒人耶稣是祂派来的。这是你们都知道的。 23上帝照着自己的计划和预知把耶稣交在你们手里,你们借着邪恶之人的手把祂钉死在十字架上了。 24但上帝为祂解除了死亡的痛苦,使祂从死里复活,因为祂不可能被死亡拘禁。 25论到耶稣,大卫曾说,

“‘我看见主常在我面前,

祂在我右边,我必不动摇。

26因此我的心欢喜,我的口颂赞,

我的身体也要活在盼望中。

27因为你不会把我的灵魂撇在阴间,

也不会让你的圣者身体朽坏。

28你已把生命之路指示我,

叫我在你面前充满喜乐。’

29“弟兄们,我肯定地对你们说,先祖大卫死了,埋葬了,他的坟墓至今还在这里。 30大卫是先知,知道上帝曾起誓要从他的后裔中选立一人继承他的王位。 31他预先知道这事,讲到基督的复活,说,‘祂的灵魂不会被撇在阴间,祂的身体也不会朽坏’。 32上帝已经使这位耶稣复活了!我们都是这件事的见证人。 33现在祂升到上帝的右边,从天父领受了所应许的圣灵,并将圣灵浇灌下来,你们今天也耳闻目睹了。 34大卫并没有升到天上,但他曾说,

“‘主对我主说,

你坐在我的右边,

35等我使你的仇敌成为你的脚凳。’

36“所以,全体以色列人啊!你们应当确实地知道,上帝已经立这位被你们钉在十字架上的耶稣为主,为基督了。”

37他们听了彼得的话,觉得扎心,就对彼得和其他使徒说:“弟兄们,我们该怎么办呢?” 38彼得说:“你们每一个人都要悔改,奉耶稣基督的名受洗,使你们的罪得到赦免,你们就必领受上帝所赐的圣灵。 39因为这应许是给你们和你们的儿女,以及远方的人,就是所有被主——我们的上帝呼召的人。”

40然后,彼得还讲了许多话警戒、劝勉他们,说:“你们要保守自己脱离这邪恶的世代。”

41结果,那天约有三千人相信了他传的道,接受了洗礼。 42他们都一心遵守使徒的教导,一起团契、掰饼、祷告。

43大家都满心敬畏上帝。使徒又行了很多神迹奇事。 44信徒聚在一起,共用所有的东西。 45他们把田产家业变卖了,按照各人的需要把钱分给大家。 46他们天天同心合意地聚集在圣殿里敬拜上帝,又在各人家中掰饼聚会,以欢喜、慷慨的心分享食物, 47赞美上帝,受到众人的喜爱。主使得救的人数与日俱增。