Matendo 15 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 15:1-41

Baraza La Yerusalemu

115:1 Gal 2:12; 5:2, 3; Mdo 6:14Baadhi ya watu wakashuka Antiokia kutoka Uyahudi, nao wakawa wanawafundisha wandugu: “Msipotahiriwa kufuatana na desturi aliyofundisha Mose, hamwezi kuokoka.” 215:2 Gal 2:2; Mdo 11:30Baada ya Paulo na Barnaba kutokubaliana nao kukawa na mabishano makali, Paulo na Barnaba na baadhi ya wengine miongoni mwao wakachaguliwa kwenda Yerusalemu ili kujadiliana jambo hili na mitume na wazee. 315:3 Mdo 14:27Hivyo wakasafirishwa na kanisa, wakiwa njiani wakapitia nchi ya Foinike na Samaria, wakawaeleza jinsi watu wa Mataifa walivyookoka. Habari hizi zikaleta furaha kubwa kwa ndugu wote. 415:4 Mdo 21:19Walipofika Yerusalemu, walipokelewa na kanisa na mitume pamoja na wazee, ndipo Paulo na Barnaba wakawaarifu kila kitu Mungu alichokuwa amefanya kupitia kwao.

515:5 Mdo 5:17; Mt 3:7; Mdo 15:1Ndipo baadhi ya walioamini wa madhehebu ya Mafarisayo wakasimama na kusema, “Hao watu wa Mataifa lazima watahiriwe na waagizwe kutii sheria ya Mose.”

6Mitume na wazee wakakutana pamoja ili kufikiri jambo hili. 715:7 Mdo 10:20; 11:12; 10:1-48Baada ya majadiliano mengi, Petro akasimama na kusema, “Ndugu zangu, mnajua kwamba siku za kwanza Mungu alinichagua ili kwa midomo yangu watu wa Mataifa wapate kusikia ujumbe wa Injili na kuamini. 815:8 Mdo 1:24; Ufu 2:23; Mdo 10:44, 47Mungu, yeye ajuaye mioyo, alionyesha kwamba anawakubali kwa kuwapa Roho Mtakatifu kama vile alivyotupa sisi. 915:9 Mdo 10:28, 34; 11:12; 10:43Mungu hakutofautisha kati yetu na wao, bali alitakasa mioyo yao kwa imani. 1015:10 Mt 23:4; Gal 5:1Sasa basi, mbona mnataka kumjaribu Mungu kwa kuweka kongwa shingoni mwa wanafunzi ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulibeba? 1115:11 Gal 2:16; Efe 2:5-8Lakini sisi tunaamini ya kuwa tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu Kristo, kama wao wanavyookolewa.”

1215:12 Yn 4:48; Mdo 14:27; 21:19Kusanyiko lote likakaa kimya, wakawasikiliza Paulo na Barnaba wakieleza jinsi Mungu alivyowatumia kutenda ishara na maajabu kwa watu wa Mataifa. 1315:13 1Kor 15:7; Gal 1:19Walipomaliza kunena, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni. 1415:14 2Pet 1:1; Mdo 15:7; Lk 1:68Simoni amekwisha kutueleza jinsi Mungu, kwa mara ya kwanza alivyoonyesha kuhusika kwa kujichagulia watu kutoka watu wa Mataifa kwa ajili ya Jina lake. 1515:15 Amo 9:11-12Maneno ya manabii yanakubaliana na jambo hili, kama ilivyoandikwa:

1615:16 Amo 9:11-12“ ‘Baada ya mambo haya nitarudi,

nami nitajenga upya

nyumba ya Daudi iliyoanguka.

Nitajenga tena magofu yake

na kuisimamisha,

1715:17 Amo 9:11, 12ili wanadamu wengine wote

wapate kumtafuta Bwana,

hata wale watu wa Mataifa wote

ambao wanaitwa kwa Jina langu,

asema Bwana, afanyaye mambo haya’

1815:18 Isa 45:21ambayo yamejulikana tangu zamani.

1915:19 Mdo 15:28; 1The 1:9“Kwa hivyo uamuzi wangu ni kwamba, tusiwataabishe watu wa Mataifa wanaomgeukia Mungu. 2015:20 1Kor 8:7-13; Ufu 2:14, 20; 1Kor 10:7-8; Ufu 2:14; 20; Mwa 9:4; Law 7:26Badala yake, tuwaandikie kwamba wajiepushe na vyakula vilivyonajisiwa kwa kutolewa sanamu, wajiepushe na uasherati, au kula mnyama aliyenyongwa, na damu. 2115:21 Mdo 13:15; 2Kor 3:14-15Kwa maana katika kila mji kwa vizazi vilivyopita, Mose amekuwa na wale wanaotangaza sheria yake kwa kuwa imekuwa ikisomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila Sabato.”

Barua Kwa Waumini Wa Mataifa

2215:22 Mdo 11:30; 16:19, 25, 26; 2Kor 1:19; 1The 1:1; 1Pet 5:12Mitume na wazee pamoja na kanisa lote, wakaamua kuwachagua baadhi ya watu wao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Wakamchagua Yuda aitwaye Barsaba pamoja na Sila, watu wawili waliokuwa viongozi miongoni mwa ndugu. 2315:23 Mdo 20:23Wakatumwa na barua ifuatayo:

Sisi mitume na wazee, ndugu zenu,

Kwa ndugu Mataifa mlioamini mlioko Antiokia, Shamu na Kilikia:

Salamu.

2415:24 Mdo 15:1; Gal 1:7; 5:10Tumesikia kwamba kuna baadhi ya watu waliokuja huko kutoka kwetu bila ruhusa yetu na kuwasumbua, wakiyataabisha mawazo yenu. 25Hivyo tumekubaliana wote kuwachagua baadhi ya watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, 2615:26 Mdo 11:19; 11:23; 15:40; 13:13watu ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo. 2715:27 Mdo 15:22Kwa hiyo tunawatuma Yuda na Sila, kuthibitisha kwa maneno ya mdomo mambo haya tunayowaandikia. 2815:28 Mdo 5:32Kwa maana imempendeza Roho Mtakatifu na sisi tusiwatwike mzigo wowote mkubwa zaidi ya mambo haya yafuatayo ambayo ni ya lazima: 2915:29 Mdo 21:25Kwamba mjiepushe na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na mjiepushe na uasherati. Mkiyaepuka mambo haya, mtakuwa mmefanya vyema.

Kwaherini.

30Hivyo wakaagwa, wakashuka kwenda Antiokia. Baada ya kulikusanya kanisa pamoja, wakawapa ile barua. 31Nao hao watu wakiisha kuisoma, wakafurahishwa sana kwa ujumbe wake wa kutia moyo. 3215:32 Mdo 14:22; 18:23Yuda na Sila, ambao wenyewe walikuwa manabii, wakanena maneno mengi ya kuwatia moyo na kuwajenga katika imani wale ndugu walioamini. 3315:33 1Sam 1:17; Lk 7:50Baada ya kukaa huko Antiokia kwa muda, wakaagwa kwa amani na wale ndugu ili waende kwa wale waliowatuma. [ 3415:34 Mdo 4:36; 13:40Lakini Sila bado akaendelea kukaa huko.] 3515:35 Mdo 8:4Lakini Paulo na Barnaba walibaki Antiokia ambako wao pamoja na wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.

Safari Ya Pili Ya Paulo Kueneza Injili

(15:36–18:22)

Paulo Na Barnaba Wagawanyika

3615:36 Mdo 13:4, 13, 14, 51; 14:1, 6, 24; 25Baada ya muda, Paulo akamwambia Barnaba, “Turudi tukawatembelee ndugu katika miji yote tuliyohubiri neno la Bwana tuone jinsi wanavyoendelea.” 3715:37 Mdo 12:12Barnaba alitaka wamchukue Yohana aitwaye Marko waende naye. 3815:38 Mdo 13:13Lakini Paulo aliona si vyema kwa sababu aliwahi kuwaacha walipokuwa huko Pamfilia, hakutaka kuendelea kufanya kazi naye. 39Pakatokea ubishi mkali kati ya Paulo na Barnaba kuhusu jambo hili, hivyo wakagawanyika. Barnaba akamchukua Yohana Marko wakasafiri baharini kwenda Kipro. 4015:40 Mdo 11:23; 15:41; Lk 2:2; Mdo 6:9; 16:5Lakini Paulo akamchagua Sila na akaondoka baada ya ndugu kuwatakia neema ya Bwana. 41Akapitia Shamu na Kilikia, akiimarisha makanisa ya huko.

New International Reader’s Version

Acts 15:1-41

Church Leaders Meet in Jerusalem

1Certain people came down from Judea to Antioch. Here is what they were teaching the believers. “Moses commanded you to be circumcised,” they said. “If you aren’t, you can’t be saved.” 2But Paul and Barnabas didn’t agree with this. They argued strongly with them. So Paul and Barnabas were appointed to go up to Jerusalem. Some other believers were chosen to go with them. They were told to ask the apostles and elders about this question. 3The church sent them on their way. They traveled through Phoenicia and Samaria. There they told how the Gentiles had turned to God. This news made all the believers very glad. 4When they arrived in Jerusalem, the church welcomed them. The apostles and elders welcomed them too. Then Paul and Barnabas reported everything God had done through them.

5Some of the believers were Pharisees. They stood up and said, “The Gentiles must be circumcised. They must obey the law of Moses.”

6The apostles and elders met to consider this question. 7After they had talked it over, Peter got up and spoke to them. “Brothers,” he said, “you know that some time ago God chose me. He appointed me to take the good news to the Gentiles. He wanted them to hear the good news and believe. 8God knows the human heart. By giving the Holy Spirit to the Gentiles, he showed that he accepted them. He did the same for them as he had done for us. 9God showed that there is no difference between us and them. That’s because he made their hearts pure because of their faith. 10Now then, why are you trying to test God? You test him when you put a heavy load on the shoulders of Gentiles. Our people of long ago couldn’t carry that load. We can’t either. 11No! We believe we are saved through the grace of our Lord Jesus. The Gentiles are saved in the same way.”

12Everyone became quiet as they listened to Barnabas and Paul. They were telling about the signs and wonders God had done through them among the Gentiles. 13When they finished, James spoke up. “Brothers,” he said, “listen to me. 14Simon Peter has explained to us what God has now done. He has chosen some of the Gentiles to be among his very own people. 15The prophets’ words agree with that. They say,

16“ ‘After this I will return

and set up again David’s fallen tent.

I will rebuild what was destroyed.

I will make it what it used to be.

17Then everyone else can look to the Lord.

This includes all the Gentiles who belong to me, says the Lord.

The Lord is the one who does these things.’ (Amos 9:11,12)

18The Lord does things that have been known from long ago.

19“Now here is my decision. We should not make it hard for the Gentiles who are turning to God. 20Here is what we should write to them. They must not eat food that has been made impure by being offered to statues of gods. They must not commit sexual sins. They must not eat the meat of animals that have been choked to death. And they must not drink blood. 21These laws of Moses have been preached in every city from the earliest times. They are read out loud in the synagogues every Sabbath day.”

A Letter Is Written to Gentile Believers

22Then the apostles, the elders and the whole church decided what to do. They would choose some of their own men who were leaders among the believers. They would send them to Antioch with Paul and Barnabas. So they chose Judas Barsabbas and Silas. They were leaders among the believers. 23Here is the letter they sent with them.

The apostles and elders, your brothers, are writing this letter.

We are sending it to the Gentile believers in Antioch, Syria and Cilicia.

Greetings.

24We have heard that some of our people came to you and caused trouble. You were upset by what they said. But we had given them no authority to go. 25So we all agreed to send our dear friends Barnabas and Paul to you. We chose some other men to go with them. 26Barnabas and Paul have put their lives in danger. They did it for the name of our Lord Jesus Christ. 27So we are sending Judas and Silas with them. What they say will agree with this letter. 28Here is what seemed good to the Holy Spirit and to us. We will not give you a load that is too heavy. So here are a few basic rules. 29Don’t eat food that has been offered to statues of gods. Don’t drink blood. Don’t eat the meat of animals that have been choked to death. And don’t commit sexual sins. You will do well to keep away from these things.

Farewell.

30So the men were sent down to Antioch. There they gathered the church together. They gave the letter to them. 31The people read it. They were glad for its message of hope. 32Judas and Silas were prophets. They said many things to give strength and hope to the believers. 33-34Judas and Silas stayed there for some time. Then the believers sent them away with the blessing of peace. They sent them back to those who had sent them out. 35Paul and Barnabas remained in Antioch. There they and many others taught and preached the word of the Lord.

Paul and Barnabas Do Not Agree

36Some time later Paul spoke to Barnabas. “Let’s go back to all the towns where we preached the word of the Lord,” he said. “Let’s visit the believers and see how they are doing.” 37Barnabas wanted to take John Mark with them. 38But Paul didn’t think it was wise to take him. Mark had deserted them in Pamphylia. He hadn’t continued with them in their work. 39Barnabas and Paul strongly disagreed with each other. So they went their separate ways. Barnabas took Mark and sailed for Cyprus. 40But Paul chose Silas. The believers asked the Lord to give his grace to Paul and Silas as they went. 41Paul traveled through Syria and Cilicia. He gave strength to the churches there.