Matendo 12 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 12:1-25

Yakobo Auawa, Petro Atiwa Gerezani

112:1 Mt 14:1Wakati huo huo Mfalme Herode Agripa aliwakamata baadhi ya watu wa kanisa. 212:2 Mt 4:21; Mk 10:39Akaamuru Yakobo, ndugu yake Yohana, auawe kwa upanga. 312:3 Mdo 24:27; 25:9; Kut 12:15; 23:15; Mdo 20:6Alipoona jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamkamata pia Petro. Hii ilitokea wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. 412:4 Yn 11:15Baada ya kumkamata alimtia gerezani, chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari, vyenye askari wanne kila kimoja. Herode alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka mbele ya watu baada ya Pasaka.

512:5 Mdo 1:14; Efe 6:18Kwa hiyo Petro akawekwa gerezani, lakini kanisa lilikuwa likimwombea kwa Mungu kwa bidii.

612:6 Mdo 21:33Usiku ule kabla ya siku ambayo Herode Agripa alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili, akiwa amefungwa kwa minyororo miwili. Nao walinzi wa zamu walikuwa wakilinda penye lango la gereza. 712:7 Mdo 5:19; Za 107:14; Mdo 16:26Ghafula malaika wa Bwana akatokea na nuru ikamulika mle ndani ya gereza. Yule malaika akampiga Petro ubavuni na kumwamsha, akisema, “Ondoka upesi!” Mara ile minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro.

8Yule malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Kisha akamwambia, “Jifunge vazi lako na unifuate.” 912:9 Mdo 9:10Petro akatoka mle gerezani akiwa amefuatana na yule malaika. Hakujua wakati huo kuwa yaliyokuwa yakitukia yalikuwa kweli. Alidhani kuwa anaona maono. 1012:10 Mdo 5:19; 16:26Wakapita lindo la kwanza na la pili, ndipo wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea mjini. Lango likawafungukia lenyewe, nao wakapita hapo wakatoka nje. Baada ya kutembea umbali wa mtaa mmoja, ghafula yule malaika akamwacha Petro.

1112:11 Lk 15:17; Za 34:7; Dan 3:28; 6:22; 2Kor 11:10; 2Pet 2:9Ndipo Petro akarudiwa na fahamu, akasema, “Sasa ninajua bila shaka yoyote kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kuniokoa kutoka makucha ya Herode Agripa na kutoka matazamio yote ya Wayahudi.”

1212:12 Mdo 12:25; 15:37; Kol 4:10; 2Tim 4:11; 1Pet 5:13Mara Petro alipotambua hili alikwenda nyumbani kwa Maria, mama yake Yohana aliyeitwa pia Marko, ambako watu wengi walikuwa wamekutana kwa maombi. 1312:13 Yn 18:16Petro alipobisha hodi kwenye lango la nje, mtumishi wa kike jina lake Roda, akaja kumfungulia. 1412:14 Lk 24:41Alipoitambua sauti ya Petro, alifurahi mno akarudi bila kufungua na kuwaeleza kwamba, “Petro yuko langoni!”

1512:15 Mt 18:10Wakamwambia yule mtumishi wa kike, “Umerukwa na akili.” Alipozidi kusisitiza kuwa ni kweli, wakasema, “Lazima awe ni malaika wake.”

16Lakini Petro aliendelea kugonga langoni, nao walipofungua lango na kumwona Petro, walistaajabu sana. 1712:17 Mdo 19:33; 21:40Yeye akawaashiria kwa mkono wake wanyamaze kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Naye akaongeza kusema, “Waelezeni Yakobo na ndugu wengine habari hizi.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.

1812:18 Mdo 5:21, 22Kulipokucha kukawa na fadhaa kubwa miongoni mwa wale askari kuhusu yaliyomtukia Petro. 1912:19 Mdo 8:1-4; 16:27; 8:40Baada ya Herode kuamuru atafutwe kila mahali na bila kumpata, aliwahoji wale askari walinzi kisha akatoa amri wauawe. Basi Herode Agripa akatoka Uyahudi akaenda Kaisaria, akakaa huko kwa muda.

Kifo Cha Herode Agripa

2012:20 Mt 11:21; 1Fal 5:9, 11; Eze 27:17Basi Herode Agripa alikuwa amekasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Hivyo watu wa miji hiyo miwili wakaungana pamoja wakatafuta kukutana naye. Wakiisha kuungwa mkono na Blasto, mtumishi maalum wa Mfalme Herode Agripa aliyeaminika, wakaomba mapatano ya amani maana nchi zao zilitegemea nchi ya huyo mfalme kwa mahitaji yao ya chakula.

21Katika siku iliyochaguliwa Herode Agripa akavaa mavazi yake ya kifalme, akaketi kwenye kiti chake cha enzi na kuwahutubia watu. 2212:22 Eze 28:2Watu waliokuwa wamekusanyika wakapiga kelele, wakisema, “Hii si sauti ya mwanadamu, bali ni ya Mungu.” 2312:23 Mdo 5:19; 1Sam 25:38; 2Sam 24:16; 2Fal 19:35Ghafula, kwa kuwa Herode hakumpa Mungu utukufu, malaika wa Bwana akampiga, naye akaliwa na chango, akafa.

2412:24 Ebr 4:12; Mdo 6:7; 19:20Lakini neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea, nao wengi wakaambatana nalo.

2512:25 Mdo 4:36; 11:30; 12:12Barnaba na Sauli walipomaliza ile huduma yao iliyowapeleka, wakarudi Yerusalemu wakiwa pamoja na Yohana aitwaye Marko.

Knijga O Kristu

Djela Apostolska 12:1-25

Jakovljevo smaknuće i Pavlovo utamničenje

1Tada kralj Herod Agripa12:1 U grčkome: kralj Herod. Nećak Heroda Antipe i unuk Heroda Velikoga. počne zlostavljati neke vjernike iz Crkve. 2Ivanova brata Jakova pogubi mačem. 3Kad je vidio da je to drago židovskim vođama, uhiti i Petra za Blagdana beskvasnih kruhova.12:3 Za vrijeme Pashe. 4Uhiti ga i baci u tamnicu te zapovjedi da ga čuvaju četiri vojničke straže. Kanio ga je poslije Pashe izvesti pred narod da mu sude. 5Dok je Petar bio u tamnici, Crkva se žarko molila Bogu za njega.

6Noć prije nego što ga je Herod kanio izvesti pred sud Petar je spavao okovan između dvojice vojnika, a pred vratima su stražarili vojnici.

Petrovo čudesno izbavljenje iz tamnice

7Ali odjednom ćeliju obasja svjetlost: pojavi se anđeo Gospodnji. Udari Petra po rebrima i reče “Brzo ustani!” I lanci mu spadnu s ruku. 8Zatim mu anđeo reče: “Opaši se i obuj sandale.” Petar posluša. “Obuci sada ogrtač i pođi za mnom!” zapovjedi anđeo.

9Petar iziđe i pođe za njim, ali nije znao da se to zaista događa. Mislio je da ima viđenje. 10Prošli su pokraj prve i druge straže te došli do željeznih vrata na izlazu iz zatvora. Ona se sama otvore te iziđu na ulicu. Kad su prošli jednu ulicu, anđeo odjednom ode od njega.

11Petar napokon shvati što se dogodilo: “Gospodin je zaista poslao anđela da me izbavi od Heroda i od onoga što su mi Židovi htjeli učiniti!” reče on.

12Kad je to shvatio, uputi se domu Marije, majke Ivana zvanoga Marko. Ondje su mnogi bili okupljeni na molitvi. 13Zakuca na dvorišna vrata. Sluškinja imenom Ruža dođe poslušati tko kuca. 14Kad je prepoznala Petrov glas, od veselja zaboravi otvoriti vrata. Utrči u kuću i javi im da je pred vratima Petar.

15“Poludjela si”, odgovore joj, ali ona je to i dalje uporno tvrdila. “Vjerojatno je to njegov anđeo”, zaključe zatim.

16Petar je i dalje kucao. Kad su na koncu otvorili i ugledali ga, zaprepaste se. 17On im rukom pokaže da šute te ispriča kako ga je sam Gospodin izveo iz tamnice. “Javite Jakovu i drugoj braći što se dogodilo!” reče. Zatim ode na drugo mjesto.

18Kad se razdanilo, među vojnicima nastane uzbuna zbog Petrova nestanka. 19Herod Agripa pošalje potragu za njim, a kad ga ne nađu, sasluša stražare i zapovjedi da se smaknu. Ode zatim iz Judeje u Cezareju te ondje ostane neko vrijeme.

Herodova smrt

20Herod je bio u žestoku sukobu sa žiteljima Tira i Sidona. Pošalju mu stoga izaslanike da s pomoću kraljevskoga komornika Blasta, kojega su pridobili, zaiskaju mir jer su hranu nabavljali iz Herodove zemlje. 21Na dan sastanka Herod obuče kraljevsko ruho te sjedne na prijestolje i počne im govoriti. 22Narod je vikao: “Božji je to glas, a ne ljudski!”

23Ali zato što je prihvatio da mu se ljudi klanjaju i što nije dao slavu Bogu, udari ga anđeo Gospodnji te ga izjedu crvi i umre.

24Ali Božja riječ brzo se širila i stjecala nove vjernike.

25Kad su Barnaba i Savao završili sa služenjem u Jeruzalemu, vrate se u Antiohiju i povedu sa sobom Ivana zvanog Marko.