Matendo 12 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 12:1-25

Yakobo Auawa, Petro Atiwa Gerezani

112:1 Mt 14:1Wakati huo huo Mfalme Herode Agripa aliwakamata baadhi ya watu wa kanisa. 212:2 Mt 4:21; Mk 10:39Akaamuru Yakobo, ndugu yake Yohana, auawe kwa upanga. 312:3 Mdo 24:27; 25:9; Kut 12:15; 23:15; Mdo 20:6Alipoona jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamkamata pia Petro. Hii ilitokea wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. 412:4 Yn 11:15Baada ya kumkamata alimtia gerezani, chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari, vyenye askari wanne kila kimoja. Herode alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka mbele ya watu baada ya Pasaka.

512:5 Mdo 1:14; Efe 6:18Kwa hiyo Petro akawekwa gerezani, lakini kanisa lilikuwa likimwombea kwa Mungu kwa bidii.

612:6 Mdo 21:33Usiku ule kabla ya siku ambayo Herode Agripa alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili, akiwa amefungwa kwa minyororo miwili. Nao walinzi wa zamu walikuwa wakilinda penye lango la gereza. 712:7 Mdo 5:19; Za 107:14; Mdo 16:26Ghafula malaika wa Bwana akatokea na nuru ikamulika mle ndani ya gereza. Yule malaika akampiga Petro ubavuni na kumwamsha, akisema, “Ondoka upesi!” Mara ile minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro.

8Yule malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Kisha akamwambia, “Jifunge vazi lako na unifuate.” 912:9 Mdo 9:10Petro akatoka mle gerezani akiwa amefuatana na yule malaika. Hakujua wakati huo kuwa yaliyokuwa yakitukia yalikuwa kweli. Alidhani kuwa anaona maono. 1012:10 Mdo 5:19; 16:26Wakapita lindo la kwanza na la pili, ndipo wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea mjini. Lango likawafungukia lenyewe, nao wakapita hapo wakatoka nje. Baada ya kutembea umbali wa mtaa mmoja, ghafula yule malaika akamwacha Petro.

1112:11 Lk 15:17; Za 34:7; Dan 3:28; 6:22; 2Kor 11:10; 2Pet 2:9Ndipo Petro akarudiwa na fahamu, akasema, “Sasa ninajua bila shaka yoyote kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kuniokoa kutoka makucha ya Herode Agripa na kutoka matazamio yote ya Wayahudi.”

1212:12 Mdo 12:25; 15:37; Kol 4:10; 2Tim 4:11; 1Pet 5:13Mara Petro alipotambua hili alikwenda nyumbani kwa Maria, mama yake Yohana aliyeitwa pia Marko, ambako watu wengi walikuwa wamekutana kwa maombi. 1312:13 Yn 18:16Petro alipobisha hodi kwenye lango la nje, mtumishi wa kike jina lake Roda, akaja kumfungulia. 1412:14 Lk 24:41Alipoitambua sauti ya Petro, alifurahi mno akarudi bila kufungua na kuwaeleza kwamba, “Petro yuko langoni!”

1512:15 Mt 18:10Wakamwambia yule mtumishi wa kike, “Umerukwa na akili.” Alipozidi kusisitiza kuwa ni kweli, wakasema, “Lazima awe ni malaika wake.”

16Lakini Petro aliendelea kugonga langoni, nao walipofungua lango na kumwona Petro, walistaajabu sana. 1712:17 Mdo 19:33; 21:40Yeye akawaashiria kwa mkono wake wanyamaze kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Naye akaongeza kusema, “Waelezeni Yakobo na ndugu wengine habari hizi.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.

1812:18 Mdo 5:21, 22Kulipokucha kukawa na fadhaa kubwa miongoni mwa wale askari kuhusu yaliyomtukia Petro. 1912:19 Mdo 8:1-4; 16:27; 8:40Baada ya Herode kuamuru atafutwe kila mahali na bila kumpata, aliwahoji wale askari walinzi kisha akatoa amri wauawe. Basi Herode Agripa akatoka Uyahudi akaenda Kaisaria, akakaa huko kwa muda.

Kifo Cha Herode Agripa

2012:20 Mt 11:21; 1Fal 5:9, 11; Eze 27:17Basi Herode Agripa alikuwa amekasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Hivyo watu wa miji hiyo miwili wakaungana pamoja wakatafuta kukutana naye. Wakiisha kuungwa mkono na Blasto, mtumishi maalum wa Mfalme Herode Agripa aliyeaminika, wakaomba mapatano ya amani maana nchi zao zilitegemea nchi ya huyo mfalme kwa mahitaji yao ya chakula.

21Katika siku iliyochaguliwa Herode Agripa akavaa mavazi yake ya kifalme, akaketi kwenye kiti chake cha enzi na kuwahutubia watu. 2212:22 Eze 28:2Watu waliokuwa wamekusanyika wakapiga kelele, wakisema, “Hii si sauti ya mwanadamu, bali ni ya Mungu.” 2312:23 Mdo 5:19; 1Sam 25:38; 2Sam 24:16; 2Fal 19:35Ghafula, kwa kuwa Herode hakumpa Mungu utukufu, malaika wa Bwana akampiga, naye akaliwa na chango, akafa.

2412:24 Ebr 4:12; Mdo 6:7; 19:20Lakini neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea, nao wengi wakaambatana nalo.

2512:25 Mdo 4:36; 11:30; 12:12Barnaba na Sauli walipomaliza ile huduma yao iliyowapeleka, wakarudi Yerusalemu wakiwa pamoja na Yohana aitwaye Marko.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

使徒行傳 12:1-25

希律王的暴行

1那時,希律王下手殘害教會的一些人, 2殺了約翰的哥哥雅各3他見這樣做能取悅猶太人,便又在除酵節期間拘捕了彼得4把他關在監裡,由四班衛兵,每班四人輪流看守,想等逾越節12·4 除酵節為期七天,逾越節是其中的第一天,參見出埃及記12章。過後當眾懲辦他。 5彼得被囚期間,教會都迫切地為他向上帝禱告。

彼得神奇出獄

6在被希律提審前一夜,彼得被兩條鐵鏈鎖著睡在兩個衛兵中間,門外警衛森嚴。 7忽然,有一位主的天使站在彼得身旁,監牢內一片光明,天使拍他的肋旁,把他叫醒,說:「趕快起來!」鐵鏈就從他手上脫落下來。 8天使對他說:「束上腰帶,穿好鞋子。」彼得一一照辦。天使又說:「披上外衣,跟我來!」 9他跟著天使走出牢房,不知道這一切都是真的,還以為自己看到了異象。 10他們一路穿過第一道和第二道守衛,來到通往城裡的鐵門,那門竟自動打開了。他們就出來,走過一條街之後,天使便離開了彼得

11彼得這才如夢初醒,說:「現在我確定,主派了天使來救我脫離希律的魔掌,不讓猶太人的期望得逞。」 12他清醒後,便到約翰·馬可的母親瑪麗亞家,很多人正聚集在那裡禱告。

13彼得在外面敲門,有一個叫羅大的婢女出來應門。 14她聽出是彼得的聲音,喜出望外,竟然沒有開門就跑進去告訴大家:「彼得在門外!」 15他們說:「你一定瘋了。」她堅持說:「是真的!」他們就說:「是他的天使吧!」

16彼得不住地敲門。他們開門看見他,都大吃一驚! 17彼得擺手示意他們安靜,然後把主怎樣領他出獄的經過告訴大家,又說:「把這事告訴雅各和其他弟兄姊妹。」交待完了,他便離開那裡,往其他地方去了。

18天亮後,監獄的守衛發現彼得不見了,頓時一片騷動。 19希律派人四處搜捕,一無所獲,於是親自審問看守彼得的衛兵,下令處決他們。後來希律離開猶太,下到凱撒利亞,並住在那裡。

希律的下場

20希律泰爾西頓的人非常惱火。於是,他們聯合起來去見他,先取得宮廷總管伯拉斯都的支持,然後向他求和,因為他們兩地需要從他的轄區獲得糧食。

21到了約定的日子,希律穿上王袍,坐在寶座上向眾人致詞。 22致詞完畢,眾人齊聲高呼:「這是神明在說話,不是凡人在說話!」 23希律沒有把榮耀歸給上帝,主的天使立刻懲罰他,他當場被蟲子咬死了。

24上帝的道日見興旺,越傳越廣。

25巴拿巴掃羅把款項送到以後,就帶著約翰·馬可耶路撒冷回去。