Matendo 1 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 1:1-26

Kanisa La Kwanza

(1:1–5:42)

Ahadi Ya Roho Mtakatifu

11:1 Lk 1:14; 3:23Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo, 21:2 Mk 16:19; 6:30; Mt 28:19-20; 10:1-4; Yn 13:18hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua. 31:3 1Kor 15:5-7; Mt 28:17; Lk 24:39-43Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu. 41:4 Lk 24:49; Yn 14:16; Mdo 2:33Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake. 51:5 Mk 1:4, 8; Mt 3:11; Mdo 11:16; 19:4; Yoe 3:18; Mdo 2:4; 11:15Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”

Yesu Apaa Mbinguni

(Marko 16:19-20; Luka 24:50-53)

61:6 Mt 17:11; Mdo 3:21; Lk 24:21; Isa 1:26; Dan 7:27; Amo 9:11Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”

71:7 Za 102:13; Mt 24:48Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. 81:8 Mdo 2:1-4; Lk 24:48Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”

91:9 Mk 16:19; Lk 24:51; Yn 6:62Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.

101:10 Lk 24:4; Yn 20:12; Mt 28:3; Mk 16:5; Mdo 10:3, 30Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao, 111:11 Mdo 2:7; Mt 16:27; Lk 21:27; 1Tim 3:16; Mdo 1:7wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”

Mathiya Achaguliwa Badala Ya Yuda

(Mathayo 27:3-10)

121:12 Lk 24:52; Mt 21:1Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato1:12 Mwendo wa Sabato hapa ina maana umbali wa mita 1,100. kutoka mjini. 131:13 Mdo 9:37; 20:8; Mt 10:2-4; Mk 3:16-19Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote1:13 Zelote hapa ina maana alikuwa mwanachama wa Wazelote, kikundi cha Kiyahudi cha kupinga jeuri ya Warumi. na Yuda mwana wa Yakobo. 141:14 Lk 18:1; 23:49-55; Mt 12:46Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.

151:15 Ufu 3:4Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema, 161:16 Mt 10:4; Yn 13:18“Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu. 171:17 Yn 6:70-71; Mt 10:4; Lk 6:16; Mdo 12:25; 20:24; 21:19Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”

181:18 Mt 26:14-15; 27:3-10(Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje. 191:19 Yn 5:2Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).

201:20 Za 69:25; 109:8“Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi,

“ ‘Mahali pake na pawe ukiwa,

wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’

na,

“ ‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’

211:21 Yn 15:27Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu, 221:22 Mk 1:4; Lk 24:48kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”

231:23 Mdo 15:22Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya. 241:24 Mdo 13:3; 14:23; 1Sam 16:7; Ufu 2:23Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua 251:25 Mdo 1:17ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.” 261:26 Mdo 2:14Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.

Knijga O Kristu

Djela Apostolska 1:1-26

Obećanje Svetoga Duha

1Dragi Teofile, u prvoj knjizi koju sam ti napisao iznio sam sve što je Isus počeo da djeluje i poučava 2do dana kad je uznesen na nebo, pošto je odabranim apostolima dao upute Svetoga Duha. 3Još četrdeset dana nakon raspeća ukazivao se apostolima i na mnoge im načine dokazao da je živ. Govorio im je o Božjemu kraljevstvu.

4Dok je tako s njima blagovao, reče im: “Ne idite iz Jeruzalema, nego ostanite ondje dok vam Otac ne pošalje što je obećao. Sjetite se, već sam vam o tomu govorio. 5Ivan je krstio vodom, ali vi ćete uskoro biti kršteni Svetim Duhom.”

Isusovo uzašašće

6Apostoli koji su bili s njim upitaju ga: “Gospodine, hoćeš li sada obnoviti izraelsko kraljevstvo?”

7“Ta vremena i prigode određuje Otac svojom vlasti”, odgovori im on, “i nije na vama da ih znate. 8Ali kad na vas siđe Sveti Duh, primit ćete snagu da o meni svjedočite ljudima posvuda—u Jeruzalemu, po svoj Judeji i Samariji i do kraja zemlje.”

9Tek što je to rekao, uznesen je na nebo pred njihovim očima i nestao u oblaku. 10Dok su očiju uprtih u nebo gledali kako odlazi, odjednom se među njima pojave dvojica ljudi u bijeloj odjeći. 11“Galilejci, što tu stojite i gledate u nebo?” rekli su. “Isus je od vas uznesen na nebo, ali jednoga dana će se vratiti jednako tako kao što ste ga vidjeli da odlazi!”

Umjesto Jude izabran Matija

12Bilo je to na Maslinskoj gori. Vrate se zatim do Jeruzalema udaljenoga otprilike kilometar.1:12 U grčkome: jedan subotni hod. 13Čim uđu u grad, odu u kuću u kojoj su boravili, u sobu na katu. Bili su ondje Petar, Ivan, Jakov, Andrija, Filip, Toma, Bartolomej, Matej, Jakov (Alfejev sin), Šimun (zelot) i Juda (Jakovljev sin).

14Svi su se ustrajno i jednodušno sastajali na molitvu s Isusovom majkom Marijom, još nekoliko drugih žena i s Isusovom braćom.

15Kad ih je jednom tako bilo okupljeno sto dvadeset, Petar ustane i reče:

16“Braćo, moralo se ispuniti ono što piše u Svetome pismu za Judu, koji je doveo hramsku policiju da uhiti Isusa. To je odavno, kroz Davida, pretkazao Sveti Duh.

17Juda je bio jedan od nas, dionik naše službe.

18Novcem koji je dobio za svoje zlodjelo Juda je kupio polje. Ondje je pao i rasprsnuo se tako da mu se prosula sva utroba. 19Vijest o njegovoj smrti brzo se pronijela među stanovnicima Jeruzalema pa su to polje prozvali Akeldama, što na aramejskome znači ‘Krvavo polje’.

20To je pretkazano u Knjizi psalama. Ondje piše:

‘Neka njegov dom opusti,

neka nitko u njemu ne stanuje!’

i

‘Neka njegovu službu dobije drugi!’1:20 Psalam 69:26; Psalam 109:8.

21Moramo zato odabrati nekoga da zamijeni Judu—nekoga tko je bio s nama cijelo vrijeme dok smo bili s Gospodinom Isusom 22otkad ga je Ivan krstio pa do uznesenja u nebo. Taj će s nama biti svjedokom Isusova uskrsnuća.”

23Predlože dvojicu: Josipa Barsabu (kojega su zvali i Just) i Matiju. 24Svi se pomole: “Gospodine, ti poznaješ svako srce. Pokaži nam kojega si od ove dvojice izabrao 25da kao apostol zamijeni izdajnika Judu koji nas je napustio i otišao onamo kamo pripada.” 26Zatim bace kocke i kocka padne na Matiju. Tako je on postao dvanaestim apostolom.