Marko 5 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 5:1-43

Yesu Amponya Mtu Mwenye Pepo

(Mathayo 8:28-34; Luka 8:26-39)

15:1 Mt 8:28; Mk 8:26Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi. 25:2 Mk 4:1; 1:23Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye. 3Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo. 4Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia. 5Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake. 75:7 Mt 8:29; Mdo 16:17; Ebr 7:1Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!” 8Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”

9Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?”

Akamjibu, “Jina langu ni Legioni,5:9 Legioni maana yake ni Jeshi. kwa kuwa tuko wengi.” 10Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

11Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima. 12Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.” 13Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.

14Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia. 155:15 Mk 5:9; 5:18-19; 4:24Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa. 16Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia. 175:17 Mt 8:34; Mdo 16:39Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.

185:18 Lk 8:38Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja. 195:19 Mt 8:4Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.” 205:20 Mt 4:25; Mk 7:31Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.

Mwanamke Aponywa

(Mathayo 9:18-26; Luka 8:40-56)

215:21 Mt 9:1; Mk 4:1Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari. 225:22 Lk 13:14; Mdo 13:15Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake, 235:23 Mt 19:13akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.” 24Hivyo Yesu akaenda pamoja naye.

Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga. 255:25 Law 15:25-30Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili. 26Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya. 27Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake, 285:28 Mt 5:20kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.” 295:29 Mk 5:34Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.

305:30 Lk 5:17; 6:19Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”

31Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’ ”

32Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa. 33Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote. 345:34 Mt 9:22; Mdo 15:33Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”

Yesu Amfufua Binti Yairo

355:35 Mk 5:22Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”

36Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”

375:37 Mt 4:21Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo. 385:38 Mt 5:22Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa. 395:39 Mt 9:24Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.” 405:40 Mdo 9:40Wale watu wakamcheka kwa dharau.

Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto. 415:41 Mk 1:31; Lk 7:14; Mdo 9:40Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” 5:41 Talitha koum ni lugha ya Kiaramu. (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”) 42Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana. 435:43 Mt 8:4Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.

Słowo Życia

Marka 5:1-43

Uzdrowienie człowieka zniewolonego przez demona

1Gdy przybyli na drugi brzeg jeziora, do krainy Gerazeńczyków, 2i gdy Jezus wysiadł z łodzi, z pobliskiego cmentarza przybiegł człowiek opanowany przez nieczyste duchy. 3Mężczyzna ten mieszkał w grobowcach i był tak silny, że gdy zakuwano jego ręce i nogi w kajdany 4—co zdarzało się bardzo często—rozrywał je i uciekał. Nikt też nie miał dość siły, żeby go obezwładnić. 5Dniami i nocami błąkał się wśród grobów i wzgórz, krzycząc i kalecząc się ostrymi kamieniami. 6Gdy z daleka zobaczył Jezusa, przybiegł, padł przez Nim na twarz 7i głośno krzyknął:

—Czego ode mnie chcesz, Jezusie, Synu Najwyższego Boga? Błagam, nie męcz mnie!

8Jezus zwrócił się do demona:

—Wyjdź z niego, duchu nieczysty!

9Zapytał też go:

—Jak ci na imię?

—Legion, bo jest nas wielu w tym człowieku—odrzekł.

10I błagały Go demony, żeby ich nie wyrzucał z tamtej okolicy. 11A na pobliskim wzgórzu, nad jeziorem, pasło się właśnie wielkie stado świń.

12—Pozwól nam wejść w te świnie—prosiły.

13A gdy Jezus zgodził się, złe duchy opuściły człowieka i weszły w świnie, po czym całe stado, liczące około dwa tysiące sztuk, rzuciło się pędem ze stromego zbocza wprost do jeziora i utonęło. 14Pasterze stada uciekli wtedy do pobliskiego miasta i okolicznych wiosek, opowiadając wszystkim o tym, co się stało. Ludzie wyszli z domów, aby zobaczyć, co się dzieje, 15i wkrótce wokół Jezusa zgromadził się spory tłum. A gdy dostrzegli szaleńca, który siedział teraz ubrany, spokojny i w pełni władz umysłowych, przestraszyli się. 16Naoczni świadkowie opowiedzieli przybyłym o wszystkim, co się wydarzyło. 17Wówczas tłum zaczął błagać Jezusa, żeby opuścił ich okolicę. 18Jezus wszedł więc do łodzi, a wtedy uzdrowiony zapytał Go, czy może z Nim pozostać. 19Jezus jednak odmówił:

—Wracaj do domu, do swoich krewnych—powiedział—i opowiedz im, co zrobił dla ciebie Pan i jak wielkie okazał ci miłosierdzie.

20Poszedł więc i opowiadał w Dekapolu o tym, co Jezus dla niego uczynił; a ludzie słuchali go pełni zdumienia.

Zmarła dziewczynka i chora kobieta

21Gdy Jezus przeprawił się na drugą stronę jeziora, na brzegu czekał na Niego wielki tłum. 22Był tam także Jair, przełożony miejscowej synagogi, który padł przed Jezusem na twarz i błagał o uzdrowienie swojej córeczki.

23—Jest umierająca—mówił zrozpaczony. —Proszę, połóż na nią ręce i przywróć ją do życia!

24Jezus poszedł więc z Jairem, a za nim—wielki tłum ludzi. 25Wśród nich znajdowała się kobieta, która od dwunastu lat cierpiała na krwotok. 26Lekarze zadali jej wiele cierpień, ale choć wydała na nich wszystkie pieniądze, nie było poprawy—przeciwnie, jej stan się pogorszył. 27Gdy więc usłyszała o nadzwyczajnych cudach Jezusa, przecisnęła się przez tłum i dotknęła z tyłu Jego ubrania. 28Myślała bowiem: „Jeśli tylko dotknę Jego płaszcza, zostanę uzdrowiona”. 29Gdy Go dotknęła, krwotok natychmiast ustał i poczuła, że jest już zdrowa. 30Jezus od razu zorientował się, że wyszła z Niego uzdrawiająca moc. Odwrócił się więc do tłumu i zapytał:

—Kto dotknął mojego płaszcza?

31Na to Jego uczniowie odpowiedzieli:

—Mnóstwo ludzi tłoczy się wokół Ciebie, a Ty pytasz, kto Cię dotknął?

32Lecz On nadal rozglądał się za tym, kto to zrobił. 33Wówczas kobieta, będąc ciągle pod wrażeniem tego, co zaszło, drżąc ze strachu, upadła Mu do nóg i przyznała się do wszystkiego.

34—Córko! Uwierzyłaś, więc zostałaś uzdrowiona. Idź w pokoju i ciesz się zdrowiem!—odrzekł jej Jezus.

35A gdy jeszcze z nią rozmawiał, przybyli posłańcy z domu Jaira z wiadomością, że jego córka umarła i nie ma już po co fatygować Jezusa. 36Lecz Jezus, nie zważając na to, co mówią, rzekł do Jaira:

—Uwierz Mi i niczego się nie bój!

37Powstrzymał idący tłum i udał się do jego domu, biorąc ze sobą tylko Piotra, Jakuba i Jana. 38Panowało tam zamieszanie, słychać było płacz i zawodzenie. 39Jezus wszedł do środka i rzekł:

—Po co ten lament i popłoch? Dziecko przecież nie umarło, tylko śpi!

40Słysząc to, wyśmiewali Go. Lecz On rozkazał, by wszyscy wyszli, a sam z trzema uczniami oraz ojcem i matką dziewczynki wszedł do pokoju, gdzie leżała. 41Wziął ją za rękę i powiedział:

—Talitha kum! (co znaczy: „Dziewczynko, mówię ci: Wstań!”).

42Ona natychmiast wstała z łóżka i zaczęła biegać, miała bowiem dwanaście lat. Rodzice oniemieli. 43Jezus zaś surowo im przykazał, aby nikomu nie mówili o tym wydarzeniu, i polecił, by dano jej coś do jedzenia.