Marko 4 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 4:1-41

Mfano Wa Mpanzi

(Mathayo 13:1-9; Luka 8:4-8)

14:1 Mk 2:13; 3:7Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari. 24:2 Mk 2:11; 3:23Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema: 34:3 Mk 4:26“Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. 4Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila. 5Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba. 6Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina. 7Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao. 84:8 Yn 15:5; Kol 1:16Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”

94:9 Mk 4:23; Mt 11:15Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”

Sababu Za Mifano

(Mathayo 13:10-17; Luka 8:9-10)

104:10 Mt 13:10; Lk 8:9Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake. 114:11 Mt 3:2; 1The 4:12; 1Tim 3:7Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano, 124:12 Isa 6:9-10; Mk 13:13-15ili,

“ ‘daima waone lakini wasitambue,

daima wasikie lakini wasielewe;

wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’ ”

Yesu Afafanua Maana Ya Mfano Wa Mbegu

(Mathayo 13:18-23; Luka 8:11-15)

13Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine? 144:14 Mdo 16:6; Flp 1:14Yule mpanzi hupanda neno. 154:15 Mt 4:10Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao. 16Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha. 17Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani. 18Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno; 194:19 1Tim 6:9-17; 1Yn 2:15-17lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. 20Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”

Mfano Wa Taa

(Luka 8:16-18)

214:21 Mt 5:15Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake? 224:22 Yer 16:17; Lk 12:2Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni. 234:23 Mk 4:9; Mt 11:15Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”

244:24 Mt 7:2; Lk 6:38Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi. 254:25 Mt 13:12; 25:29Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”

Mfano Wa Mbegu Inayoota

264:26 Mt 13:24Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani. 274:27 Yak 5:7Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo. 28Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke. 294:29 Ufu 14:15; Yoe 3:13Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”

Mfano Wa Mbegu Ya Haradali

(Mathayo 13:31-32, 34; Luka 13:18-19)

304:30 Mt 13:24Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza? 31Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini. 324:32 Dan 4:12, 21; Eze 17:23; 31; 6Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”

334:33 Yn 16:25; Mt 13:34Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa. 344:34 Yn 16:25Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.

Yesu Atuliza Dhoruba

(Mathayo 8:23-27; Luka 8:22-25)

354:35 Mt 8:18, 23-27; Lk 8:22-25Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.” 364:36 Mk 5:2, 21; 6:32, 45Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye. 37Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji. 38Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”

39Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.

404:40 Mt 14:31Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”

41Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

马可福音 4:1-41

撒种的比喻

1耶稣又到湖边讲道,周围聚集了许多人,耶稣只好上到湖边的船上坐下,众人都站在岸上。 2耶稣用比喻教导他们许多事,在教导中祂说: 3“听着!有一个农夫出去撒种。 4撒种的时候,有些种子落在路旁,被飞鸟吃掉了; 5有些落在石头地上,因为泥土不深,种子很快就发芽了, 6然而因为没有根,被太阳一晒就枯萎了; 7有些落在荆棘丛中,荆棘长起来便把嫩苗挤住了,以致不能结实; 8有些落在沃土里,就发芽生长,结出果实,收成多达三十倍、六十倍、一百倍!” 9然后祂说:“有耳可听的,都应当听。”

10当耶稣独自一人的时候,十二使徒和追随祂的人来请教比喻的意思。 11耶稣说:“上帝国的奥秘只让你们知道,对于外人,我只用比喻, 12使他们‘看了又看,却不领悟;听了又听,却不明白,免得他们回心转意,得到赦免。’”

13耶稣又对他们说:“你们不明白这个比喻,又怎能明白其他比喻呢? 14农夫撒的是上帝的道。 15种子落在路旁,是指人听了道,撒旦立刻过来夺去了撒在他们心里的道。 16种子落在石头地上,是指人听了道后,立刻欢喜地接受了, 17但他们心里没有根基,不过是暂时接受,一旦为道遭受患难和迫害,就立刻放弃了。 18种子落在荆棘丛中,是指人虽然听过道, 19但生活的忧虑、钱财的迷惑和其他欲望把道挤住了,以致不能结出果实。 20种子落在沃土里,是指人听了道,领受了,又结出果实,收成多达三十倍、六十倍、甚至一百倍。”

灯的比喻

21耶稣继续说:“人会把灯拿来放在篮子底下或床底下吗?当然不会,他一定会把它放在灯台上。 22隐藏的事是不能掩盖的,终会显露出来。 23有耳可听的,就应当听。” 24耶稣又说:“要好好思想你们所听到的,你们用什么量器量给人,就用什么量器量给你们,甚至要多给你们。 25因为凡有的,还要给他更多;凡没有的,连他仅有的也要夺去!”

种子生长的比喻

26祂又说:“上帝的国就像一个人在地上撒种。 27他天天日出而作,日落而息。种子就在他不知不觉中渐渐发芽长大。 28大地会使种子生长,先发苗后吐穗,最终结出饱满的籽粒。 29庄稼成熟后,他就拿起镰刀来收割,因为收成的时候到了。”

芥菜种的比喻

30耶稣说:“我们拿什么比作上帝的国呢?用什么比喻来解释呢? 31上帝的国就像一粒芥菜种。它是种子中最小的, 32但种在地里,却能长得比各样蔬菜都大,有粗大的枝条,可以让飞鸟在它的树荫中筑巢。”

33耶稣用了许多类似的比喻,按照众人所能领悟的,把上帝的道讲给他们听。 34祂总是用比喻对他们讲论,只有单独和门徒在一起的时候,才把一切解释清楚。

平息风浪

35那天晚上,耶稣对门徒说:“我们渡到对面去吧。” 36他们就离开众人,上了耶稣乘坐的船,一起渡到湖的对岸,还有其他船只跟着去。 37忽然,湖面上狂风大作,波浪撞击船身,船内几乎灌满了水。 38耶稣却还在船尾枕着枕头睡觉。门徒叫醒了祂,说:“老师,我们快淹死了,你怎么不管呢?”

39耶稣起来斥责狂风,对着湖面说:“静下来!停下来!”于是就风平浪静了。 40祂对门徒说:“你们为什么这样害怕呢?你们还是没有信心吗?”

41他们极其害怕,彼此议论说:“祂到底是谁?连风浪都听祂的!”