Marko 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 3:1-35

Mtu Aliyepooza Mkono Aponywa

(Mathayo 12:9-14; Luka 6:6-11)

13:1 Mt 4:23; Mk 1:21Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono. 23:2 Mt 12:10; Lk 14:1Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki. 3Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”

4Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.

53:5 Yn 11:33Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa! 63:6 Mt 22:16; Mk 12:13; Mt 12:14Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.

Umati Wa Watu Wamfuata Yesu

73:7 Mt 4:25Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata. 83:8 Mt 11:21Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni. 9Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga. 103:10 Mt 4:23; 9:20Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa. 113:11 Mt 4:3; Mk 1:23, 24Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.” 123:12 Mt 8:4; Mdo 16:17, 18Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.

Yesu Achagua Mitume Kumi Na Wawili

(Mathayo 10:1-4; Luka 6:12-16)

133:13 Mt 5:11Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia. 143:14 Mk 6:30Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri 153:15 Mt 10:1na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu. 163:16 Yn 1:42Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro); 173:17 Lk 2Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo); 18Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo, 19na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.

Yesu Na Beelzebuli

(Mathayo 12:22-32; Luka 11:14-23; 12:10)

203:20 Mk 6:31Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula. 213:21 Yn 10:20; Mdo 26:24Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”

223:22 Mt 15:1; 12:24; Yn 10:20; Mt 9:34Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli!3:22 Beelzebuli kwa Kiyunani ni Beelzebubu, yaani mkuu wa pepo wachafu. Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”

233:23 Mk 4:2; Mt 4:10Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani? 24Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama. 25Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama. 26Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia. 273:27 Isa 49:24-25Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake. 283:28 Mt 12:31; Lk 12:10; 1Yn 5:16Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa. 293:29 Mt 12:31-32; Lk 12:10Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.”

303:30 Mk 3:22Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”

Mama Na Ndugu Zake Yesu

(Mathayo 12:46-50; Luka 8:19-21)

313:31 Mt 12:46; Lk 8:19Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita. 32Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”

33Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”

34Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu. 35Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

New International Version – UK

Mark 3:1-35

Jesus heals on the Sabbath

1Another time Jesus went into the synagogue, and a man with a shrivelled hand was there. 2Some of them were looking for a reason to accuse Jesus, so they watched him closely to see if he would heal him on the Sabbath. 3Jesus said to the man with the shrivelled hand, ‘Stand up in front of everyone.’

4Then Jesus asked them, ‘Which is lawful on the Sabbath: to do good or to do evil, to save life or to kill?’ But they remained silent.

5He looked around at them in anger and, deeply distressed at their stubborn hearts, said to the man, ‘Stretch out your hand.’ He stretched it out, and his hand was completely restored. 6Then the Pharisees went out and began to plot with the Herodians how they might kill Jesus.

Crowds follow Jesus

7Jesus withdrew with his disciples to the lake, and a large crowd from Galilee followed. 8When they heard all he was doing, many people came to him from Judea, Jerusalem, Idumea, and the regions across the Jordan and around Tyre and Sidon. 9Because of the crowd he told his disciples to have a small boat ready for him, to keep the people from crowding him. 10For he had healed many, so that those with diseases were pushing forward to touch him. 11Whenever the impure spirits saw him, they fell down before him and cried out, ‘You are the Son of God.’ 12But he gave them strict orders not to tell others about him.

Jesus appoints the Twelve

13Jesus went up on a mountainside and called to him those he wanted, and they came to him. 14He appointed twelve3:14 Some manuscripts twelve – designating them apostles – that they might be with him and that he might send them out to preach 15and to have authority to drive out demons.

16These are the twelve he appointed:

Simon (to whom he gave the name Peter),

17James son of Zebedee and his brother John (to them he gave the name Boanerges, which means ‘sons of thunder’),

18Andrew,

Philip,

Bartholomew,

Matthew,

Thomas,

James son of Alphaeus,

Thaddaeus,

Simon the Zealot

19and Judas Iscariot, who betrayed him.

Jesus accused by his family and by teachers of the law

20Then Jesus entered a house, and again a crowd gathered, so that he and his disciples were not even able to eat. 21When his family3:21 Or his associates heard about this, they went to take charge of him, for they said, ‘He is out of his mind.’

22And the teachers of the law who came down from Jerusalem said, ‘He is possessed by Beelzebul! By the prince of demons he is driving out demons.’

23So Jesus called them over to him and began to speak to them in parables: ‘How can Satan drive out Satan? 24If a kingdom is divided against itself, that kingdom cannot stand. 25If a house is divided against itself, that house cannot stand. 26And if Satan opposes himself and is divided, he cannot stand; his end has come. 27In fact, no-one can enter a strong man’s house without first tying him up. Then he can plunder the strong man’s house. 28Truly I tell you, people can be forgiven all their sins and every slander they utter, 29but whoever blasphemes against the Holy Spirit will never be forgiven; they are guilty of an eternal sin.’

30He said this because they were saying, ‘He has an impure spirit.’

31Then Jesus’ mother and brothers arrived. Standing outside, they sent someone in to call him. 32A crowd was sitting round him, and they told him, ‘Your mother and brothers are outside looking for you.’

33‘Who are my mother and my brothers?’ he asked.

34Then he looked at those seated in a circle round him and said, ‘Here are my mother and my brothers! 35Whoever does God’s will is my brother and sister and mother.’