Marko 3 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 3:1-35

Mtu Aliyepooza Mkono Aponywa

(Mathayo 12:9-14; Luka 6:6-11)

13:1 Mt 4:23; Mk 1:21Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono. 23:2 Mt 12:10; Lk 14:1Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki. 3Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”

4Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.

53:5 Yn 11:33Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa! 63:6 Mt 22:16; Mk 12:13; Mt 12:14Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.

Umati Wa Watu Wamfuata Yesu

73:7 Mt 4:25Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata. 83:8 Mt 11:21Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni. 9Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga. 103:10 Mt 4:23; 9:20Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa. 113:11 Mt 4:3; Mk 1:23, 24Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.” 123:12 Mt 8:4; Mdo 16:17, 18Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.

Yesu Achagua Mitume Kumi Na Wawili

(Mathayo 10:1-4; Luka 6:12-16)

133:13 Mt 5:11Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia. 143:14 Mk 6:30Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri 153:15 Mt 10:1na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu. 163:16 Yn 1:42Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro); 173:17 Lk 2Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo); 18Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo, 19na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.

Yesu Na Beelzebuli

(Mathayo 12:22-32; Luka 11:14-23; 12:10)

203:20 Mk 6:31Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula. 213:21 Yn 10:20; Mdo 26:24Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”

223:22 Mt 15:1; 12:24; Yn 10:20; Mt 9:34Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli!3:22 Beelzebuli kwa Kiyunani ni Beelzebubu, yaani mkuu wa pepo wachafu. Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”

233:23 Mk 4:2; Mt 4:10Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani? 24Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama. 25Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama. 26Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia. 273:27 Isa 49:24-25Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake. 283:28 Mt 12:31; Lk 12:10; 1Yn 5:16Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa. 293:29 Mt 12:31-32; Lk 12:10Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.”

303:30 Mk 3:22Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”

Mama Na Ndugu Zake Yesu

(Mathayo 12:46-50; Luka 8:19-21)

313:31 Mt 12:46; Lk 8:19Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita. 32Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”

33Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”

34Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu. 35Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

New International Reader’s Version

Mark 3:1-35

Jesus Heals on the Sabbath Day

1Another time Jesus went into the synagogue. A man with a weak and twisted hand was there. 2Some Pharisees were trying to find fault with Jesus. They watched him closely. They wanted to see if he would heal the man on the Sabbath day. 3Jesus spoke to the man with the weak and twisted hand. “Stand up in front of everyone,” he said.

4Then Jesus asked them, “What does the Law say we should do on the Sabbath day? Should we do good? Or should we do evil? Should we save life? Or should we kill?” But no one answered.

5Jesus looked around at them in anger. He was very upset because their hearts were stubborn. Then he said to the man, “Stretch out your hand.” He stretched it out, and his hand had become as good as new. 6Then the Pharisees went out and began to make plans with the Herodians. They wanted to kill Jesus.

Crowds Follow Jesus

7Jesus went off to the Sea of Galilee with his disciples. A large crowd from Galilee followed. 8People heard about all that Jesus was doing. And many came to him. They came from Judea, Jerusalem and Idumea. They came from the lands east of the Jordan River. And they came from the area around Tyre and Sidon. 9Because of the crowd, Jesus told his disciples to get a small boat ready for him. This would keep the people from crowding him. 10Jesus had healed many people. So those who were sick were pushing forward to touch him. 11When people controlled by evil spirits saw him, they fell down in front of him. The spirits shouted, “You are the Son of God!” 12But Jesus ordered them not to tell people about him.

Jesus Appoints the Twelve Disciples

13Jesus went up on a mountainside. He called for certain people to come to him, and they came. 14He appointed 12 of them so that they would be with him. He would also send them out to preach. 15And he gave them authority to drive out demons.

16So Jesus appointed the 12 disciples.

Simon was one of them. Jesus gave him the name Peter.

17There were James, son of Zebedee, and his brother John. Jesus gave them the name Boanerges. Boanerges means Sons of Thunder.

18There were also Andrew,

Philip,

Bartholomew,

Matthew,

Thomas,

and James, son of Alphaeus.

And there were Thaddaeus

and Simon the Zealot.

19Judas Iscariot was one of them too. He was the one who was later going to hand Jesus over to his enemies.

Jesus Is Accused by Teachers of the Law

20Jesus entered a house. Again a crowd gathered. It was so large that Jesus and his disciples were not even able to eat. 21His family heard about this. So they went to take charge of him. They said, “He is out of his mind.”

22Some teachers of the law were there. They had come down from Jerusalem. They said, “He is controlled by Beelzebul! He is driving out demons by the power of the prince of demons.”

23So Jesus called them over to him. He began to speak to them using stories. He said, “How can Satan drive out Satan? 24If a kingdom fights against itself, it can’t stand. 25If a family is divided, it can’t stand. 26And if Satan fights against himself, and his helpers are divided, he can’t stand. That is the end of him. 27In fact, none of you can enter a strong man’s house unless you tie him up first. Then you can steal things from his house. 28What I’m about to tell you is true. Everyone’s sins and evil words against God will be forgiven. 29But whoever speaks evil things against the Holy Spirit will never be forgiven. Their guilt will last forever.”

30Jesus said this because the teachers of the law were saying, “He has an evil spirit.”

Jesus’ Mother and Brothers

31Jesus’ mother and brothers came and stood outside. They sent someone in to get him. 32A crowd was sitting around Jesus. They told him, “Your mother and your brothers are outside. They are looking for you.”

33“Who is my mother? Who are my brothers?” he asked.

34Then Jesus looked at the people sitting in a circle around him. He said, “Here is my mother! Here are my brothers! 35Anyone who does what God wants is my brother or sister or mother.”