Marko 15 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 15:1-47

Yesu Mbele Ya Pilato

(Mathayo 27:1-14; Luka 23:1-5; Yohana 18:28-38)

115:1 Mt 27:1-2; Lk 22:66; Mt 5:22Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.

215:2 Mt 2:2Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?”

Yesu akajibu, “Wewe umesema.”

3Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi. 415:4 Mt 27:13Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”

515:5 Mk 14:61Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.

Pilato Amtoa Yesu Asulubiwe

(Mathayo 27:15-26; Luka 23:13-25; Yohana 18:39–19:16)

615:6 Mt 27:15; Lk 23:17; Yn 18:39Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka. 7Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi. 8Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.

9Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?” 1015:10 Yn 11:48; 12:19; Mt 27:38Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu. 1115:11 Mdo 3:14Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.

12Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”

13Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”

14Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?”

Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”

1515:15 Isa 53:6; Mt 27:26; Yn 19:1, 36Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.

Askari Wamdhihaki Yesu

(Mathayo 27:27-31; Yohana 19:2-3)

1615:16 Yn 18:28-33; 19:9Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio,15:16 Praitorio maana yake ni makao makuu ya mtawala; ni jumba la kifalme lililokuwa linakaliwa na Pontio Pilato huko Yerusalemu, palipokuwa na kiti cha hukumu. wakakusanya kikosi kizima cha askari. 17Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani. 18Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!” 19Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki. 2015:20 Ebr 13:12Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.

Kusulubiwa Kwa Yesu

(Mathayo 27:32-44; Luka 23:26-43; Yohana 19:17-27)

2115:21 Mt 27:32; Lk 23:36Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba. 2215:22 Mt 27:33; Lk 23:33; Yn 19:17Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa). 2315:23 Za 69:21; Mit 31:6Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa. 2415:24 Za 22; 18Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.

2515:25 Mt 27:45; Lk 23:44; Yn 19:14Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha. 2615:26 Mt 27:37; Yn 19:19; Mk 15:2Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.” 2715:27 Mt 27:38Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [ 2815:28 Isa 51:12; Lk 22:37Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]” 2915:29 Za 22:7; 109:25; Mk 14:58; Yn 2:19Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu, 30basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”

3115:31 Za 22:7Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! 3215:32 Mk 14:61; 15:2Basi huyu Kristo,15:32 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.

Kifo Cha Yesu Msalabani

(Mathayo 27:45-56; Luka 23:44-49; Yohana 19:28-30)

3315:33 Amo 8:9Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa. 3415:34 Za 21:1; Mt 27:46Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)

35Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”

3615:36 Mk 15:23; Za 69:21Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”

3715:37 Yn 19:30Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.

3815:38 Ebr 10:19-20Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini. 3915:39 Mt 4:3; Mk 9:7Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”

4015:40 Za 38:11; Lk 24:10; Yn 19:25Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome. 4115:41 Mt 27:55-56; Lk 8:2-3Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.

Maziko Ya Yesu

(Mathayo 27:57-61; Luka 23:50-56; Yohana 19:38-42)

4215:42 Mt 27:62; Yn 19:31Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato, 4315:43 Mt 5:22; 3:2; Lk 2:25, 38Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu. 44Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa. 4515:45 Mk 15:39Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili. 4615:46 Mk 16:3Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi. 47Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.

King James Version

Mark 15:1-47

1And straightway in the morning the chief priests held a consultation with the elders and scribes and the whole council, and bound Jesus, and carried him away, and delivered him to Pilate. 2And Pilate asked him, Art thou the King of the Jews? And he answering said unto him, Thou sayest it. 3And the chief priests accused him of many things: but he answered nothing. 4And Pilate asked him again, saying, Answerest thou nothing? behold how many things they witness against thee. 5But Jesus yet answered nothing; so that Pilate marvelled. 6Now at that feast he released unto them one prisoner, whomsoever they desired. 7And there was one named Barabbas, which lay bound with them that had made insurrection with him, who had committed murder in the insurrection. 8And the multitude crying aloud began to desire him to do as he had ever done unto them. 9But Pilate answered them, saying, Will ye that I release unto you the King of the Jews? 10For he knew that the chief priests had delivered him for envy. 11But the chief priests moved the people, that he should rather release Barabbas unto them. 12And Pilate answered and said again unto them, What will ye then that I shall do unto him whom ye call the King of the Jews? 13And they cried out again, Crucify him. 14Then Pilate said unto them, Why, what evil hath he done? And they cried out the more exceedingly, Crucify him.

15¶ And so Pilate, willing to content the people, released Barabbas unto them, and delivered Jesus, when he had scourged him, to be crucified. 16And the soldiers led him away into the hall, called Prætorium; and they call together the whole band. 17And they clothed him with purple, and platted a crown of thorns, and put it about his head, 18And began to salute him, Hail, King of the Jews! 19And they smote him on the head with a reed, and did spit upon him, and bowing their knees worshipped him. 20And when they had mocked him, they took off the purple from him, and put his own clothes on him, and led him out to crucify him. 21And they compel one Simon a Cyrenian, who passed by, coming out of the country, the father of Alexander and Rufus, to bear his cross. 22And they bring him unto the place Golgotha, which is, being interpreted, The place of a skull. 23And they gave him to drink wine mingled with myrrh: but he received it not. 24And when they had crucified him, they parted his garments, casting lots upon them, what every man should take. 25And it was the third hour, and they crucified him. 26And the superscription of his accusation was written over, THE KING OF THE JEWS. 27And with him they crucify two thieves; the one on his right hand, and the other on his left. 28And the scripture was fulfilled, which saith, And he was numbered with the transgressors. 29And they that passed by railed on him, wagging their heads, and saying, Ah, thou that destroyest the temple, and buildest it in three days, 30Save thyself, and come down from the cross. 31Likewise also the chief priests mocking said among themselves with the scribes, He saved others; himself he cannot save. 32Let Christ the King of Israel descend now from the cross, that we may see and believe. And they that were crucified with him reviled him. 33And when the sixth hour was come, there was darkness over the whole land until the ninth hour. 34And at the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, Eloi, Eloi, lama sabachthani? which is, being interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me? 35And some of them that stood by, when they heard it, said, Behold, he calleth Elias. 36And one ran and filled a spunge full of vinegar, and put it on a reed, and gave him to drink, saying, Let alone; let us see whether Elias will come to take him down. 37And Jesus cried with a loud voice, and gave up the ghost. 38And the veil of the temple was rent in twain from the top to the bottom.

39¶ And when the centurion, which stood over against him, saw that he so cried out, and gave up the ghost, he said, Truly this man was the Son of God. 40There were also women looking on afar off: among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome; 41(Who also, when he was in Galilee, followed him, and ministered unto him;) and many other women which came up with him unto Jerusalem.

42¶ And now when the even was come, because it was the preparation, that is, the day before the sabbath, 43Joseph of Arimathaea, an honourable counsellor, which also waited for the kingdom of God, came, and went in boldly unto Pilate, and craved the body of Jesus. 44And Pilate marvelled if he were already dead: and calling unto him the centurion, he asked him whether he had been any while dead. 45And when he knew it of the centurion, he gave the body to Joseph. 46And he bought fine linen, and took him down, and wrapped him in the linen, and laid him in a sepulchre which was hewn out of a rock, and rolled a stone unto the door of the sepulchre. 47And Mary Magdalene and Mary the mother of Joses beheld where he was laid.