Marko 13 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 13:1-37

Dalili Za Siku Za Mwisho

(Mathayo 24:1-2; Luka 21:5-6)

113:1 Mt 24:1; Lk 21:5Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”

213:2 Lk 19:44Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”

Mateso Yatabiriwa

(Mathayo 24:3-14; Luka 21:7-19)

313:3 Mt 21:1; 4:21Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani, 413:4 Mt 24:3; Lk 21:7“Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”

513:5 Yer 29:8; 1Tim 4:1Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye. 6Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi. 7Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado. 813:8 Mt 24:8; Isa 19:2; 2Nya 15:6Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

913:9 Mt 10:17“Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao. 1013:10 Mt 10:19-20Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia. 1113:11 Lk 12:11-12Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.

1213:12 Mik 7:6; Lk 12:51-53“Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe. 1313:13 Yn 15:21; Mt 10:22Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

Chukizo La Uharibifu

(Mathayo 24:15-28; Luka 21:20-24)

1413:14 Dan 11:31; 12:11“Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. 15Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote. 16Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 1713:17 Lk 22:39; 21:23Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! 18Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi. 1913:19 Mk 10:6; Dan 9:26; Yoe 2:2Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe. 20Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo. 2113:21 Lk 17:23; 21:8Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo13:21 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. huyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki. 2213:22 Mt 7:15; Yn 4:48; 2The 2:9-10Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule. 2313:23 2Pet 3:17Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

(Mathayo 24:29-31; Luka 21:25-28)

2413:24 Isa 13:10“Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki,

“ ‘jua litatiwa giza

nao mwezi hautatoa nuru yake;

2513:25 Isa 34:4; Mt 24:9nazo nyota zitaanguka kutoka angani,

na nguvu za anga zitatikisika.’

2613:26 Dan 7:13; Ufu 1:7“Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu. 2713:27 Zek 2:6Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.

Somo Kuhusu Mtini

(Mathayo 24:32-35; Luka 21:29-33)

2813:28 Mt 24:32; Lk 21:29“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 29Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 3013:30 Lk 17:25; Mk 9:11Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 3113:31 Mt 5:18Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

(Mathayo 24:36-44)

3213:32 Mdo 1:7; 1The 5:1-2“Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake. 33Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia. 3413:34 Mt 25:14Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.

3513:35 Mt 24:42, 44“Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko. 36Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala. 3713:37 Lk 12:35-40Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’ ”

Nova Versão Internacional

Marcos 13:1-37

O Sinal do Fim dos Tempos

(Mt 24.1-35; Lc 21.5-37)

1Quando ele estava saindo do templo, um de seus discípulos lhe disse: “Olha, Mestre! Que pedras enormes! Que construções magníficas!”

2“Você está vendo todas estas grandes construções?”, perguntou Jesus. “Aqui não ficará pedra sobre pedra; serão todas derrubadas.”

3Tendo Jesus se assentado no monte das Oliveiras, de frente para o templo, Pedro, Tiago, João e André lhe perguntaram em particular: 4“Dize-nos, quando acontecerão essas coisas? E qual será o sinal de que tudo isso está prestes a cumprir-se?”

5Jesus lhes disse: “Cuidado, que ninguém os engane. 6Muitos virão em meu nome, dizendo: ‘Sou eu!’ e enganarão a muitos. 7Quando ouvirem falar de guerras e rumores de guerras, não tenham medo. É necessário que tais coisas aconteçam, mas ainda não é o fim. 8Nação se levantará contra nação, e reino contra reino. Haverá terremotos em vários lugares e também fomes. Essas coisas são o início das dores.

9“Fiquem atentos, pois vocês serão entregues aos tribunais e serão açoitados nas sinagogas. Por minha causa vocês serão levados à presença de governadores e reis, como testemunho a eles. 10E é necessário que antes o evangelho seja pregado a todas as nações. 11Sempre que forem presos e levados a julgamento, não fiquem preocupados com o que vão dizer. Digam tão somente o que for dado a vocês naquela hora, pois não serão vocês que estarão falando, mas o Espírito Santo.

12“O irmão trairá seu próprio irmão, entregando-o à morte, e o mesmo fará o pai a seu filho. Filhos se rebelarão contra seus pais e os matarão. 13Todos odiarão vocês por minha causa; mas aquele que perseverar até o fim será salvo.

14“Quando vocês virem ‘o sacrilégio terrível’13.14 Dn 9.27; 11.31; 12.11 no lugar onde não deve estar—quem lê, entenda—então, os que estiverem na Judeia fujam para os montes. 15Quem estiver no telhado de sua casa não desça nem entre em casa para tirar dela coisa alguma. 16Quem estiver no campo não volte para pegar seu manto. 17Como serão terríveis aqueles dias para as grávidas e para as que estiverem amamentando! 18Orem para que essas coisas não aconteçam no inverno. 19Porque aqueles serão dias de tribulação como nunca houve desde que Deus criou o mundo até agora, nem jamais haverá. 20Se o Senhor não tivesse abreviado tais dias, ninguém sobreviveria13.20 Ou seria salvo. Mas, por causa dos eleitos por ele escolhidos, ele os abreviou. 21Se, então, alguém disser: ‘Vejam, aqui está o Cristo!’ ou: ‘Vejam, ali está ele!’, não acreditem. 22Pois aparecerão falsos cristos e falsos profetas que realizarão sinais e maravilhas para, se possível, enganar os eleitos. 23Por isso, fiquem atentos: avisei-os de tudo antecipadamente.

24“Mas, naqueles dias, após aquela tribulação,

“ ‘o sol escurecerá

e a lua não dará a sua luz;

25as estrelas cairão do céu

e os poderes celestes serão abalados’13.24,25 Is 13.10; 34.4.

26“Então verão o Filho do homem vindo nas nuvens com grande poder e glória. 27E ele enviará os seus anjos e reunirá os seus eleitos dos quatro ventos, dos confins da terra até os confins do céu.

28“Aprendam a lição da figueira: Quando seus ramos se renovam e suas folhas começam a brotar, vocês sabem que o verão está próximo. 29Assim também, quando virem estas coisas acontecendo, saibam que ele está próximo, às portas. 30Eu asseguro a vocês que não passará esta geração até que todas estas coisas aconteçam. 31Os céus e a terra passarão, mas as minhas palavras jamais passarão.

O Dia e a Hora São Desconhecidos

(Mt 24.36-51)

32“Quanto ao dia e à hora ninguém sabe, nem os anjos no céu, nem o Filho, senão somente o Pai. 33Fiquem atentos! Vigiem!13.33 Alguns manuscritos acrescentam e orem! Vocês não sabem quando virá esse tempo. 34É como um homem que sai de viagem. Ele deixa sua casa, encarrega de tarefas cada um dos seus servos e ordena ao porteiro que vigie. 35Portanto, vigiem, porque vocês não sabem quando o dono da casa voltará: se à tarde, à meia-noite, ao cantar do galo ou ao amanhecer. 36Se ele vier de repente, que não os encontre dormindo! 37O que digo a vocês, digo a todos: Vigiem!”