Marko 13 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 13:1-37

Dalili Za Siku Za Mwisho

(Mathayo 24:1-2; Luka 21:5-6)

113:1 Mt 24:1; Lk 21:5Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”

213:2 Lk 19:44Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”

Mateso Yatabiriwa

(Mathayo 24:3-14; Luka 21:7-19)

313:3 Mt 21:1; 4:21Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani, 413:4 Mt 24:3; Lk 21:7“Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”

513:5 Yer 29:8; 1Tim 4:1Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye. 6Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi. 7Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado. 813:8 Mt 24:8; Isa 19:2; 2Nya 15:6Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

913:9 Mt 10:17“Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao. 1013:10 Mt 10:19-20Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia. 1113:11 Lk 12:11-12Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.

1213:12 Mik 7:6; Lk 12:51-53“Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe. 1313:13 Yn 15:21; Mt 10:22Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

Chukizo La Uharibifu

(Mathayo 24:15-28; Luka 21:20-24)

1413:14 Dan 11:31; 12:11“Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. 15Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote. 16Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 1713:17 Lk 22:39; 21:23Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! 18Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi. 1913:19 Mk 10:6; Dan 9:26; Yoe 2:2Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe. 20Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo. 2113:21 Lk 17:23; 21:8Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo13:21 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. huyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki. 2213:22 Mt 7:15; Yn 4:48; 2The 2:9-10Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule. 2313:23 2Pet 3:17Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

(Mathayo 24:29-31; Luka 21:25-28)

2413:24 Isa 13:10“Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki,

“ ‘jua litatiwa giza

nao mwezi hautatoa nuru yake;

2513:25 Isa 34:4; Mt 24:9nazo nyota zitaanguka kutoka angani,

na nguvu za anga zitatikisika.’

2613:26 Dan 7:13; Ufu 1:7“Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu. 2713:27 Zek 2:6Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.

Somo Kuhusu Mtini

(Mathayo 24:32-35; Luka 21:29-33)

2813:28 Mt 24:32; Lk 21:29“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 29Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 3013:30 Lk 17:25; Mk 9:11Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 3113:31 Mt 5:18Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

(Mathayo 24:36-44)

3213:32 Mdo 1:7; 1The 5:1-2“Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake. 33Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia. 3413:34 Mt 25:14Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.

3513:35 Mt 24:42, 44“Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko. 36Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala. 3713:37 Lk 12:35-40Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’ ”

King James Version

Mark 13:1-37

1And as he went out of the temple, one of his disciples saith unto him, Master, see what manner of stones and what buildings are here! 2And Jesus answering said unto him, Seest thou these great buildings? there shall not be left one stone upon another, that shall not be thrown down. 3And as he sat upon the mount of Olives over against the temple, Peter and James and John and Andrew asked him privately, 4Tell us, when shall these things be? and what shall be the sign when all these things shall be fulfilled? 5And Jesus answering them began to say, Take heed lest any man deceive you: 6For many shall come in my name, saying, I am Christ; and shall deceive many. 7And when ye shall hear of wars and rumours of wars, be ye not troubled: for such things must needs be; but the end shall not be yet. 8For nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom: and there shall be earthquakes in divers places, and there shall be famines and troubles: these are the beginnings of sorrows.

9¶ But take heed to yourselves: for they shall deliver you up to councils; and in the synagogues ye shall be beaten: and ye shall be brought before rulers and kings for my sake, for a testimony against them. 10And the gospel must first be published among all nations. 11But when they shall lead you, and deliver you up, take no thought beforehand what ye shall speak, neither do ye premeditate: but whatsoever shall be given you in that hour, that speak ye: for it is not ye that speak, but the Holy Ghost. 12Now the brother shall betray the brother to death, and the father the son; and children shall rise up against their parents, and shall cause them to be put to death. 13And ye shall be hated of all men for my name’s sake: but he that shall endure unto the end, the same shall be saved.

14¶ But when ye shall see the abomination of desolation, spoken of by Daniel the prophet, standing where it ought not, (let him that readeth understand,) then let them that be in Judæa flee to the mountains: 15And let him that is on the housetop not go down into the house, neither enter therein, to take any thing out of his house: 16And let him that is in the field not turn back again for to take up his garment. 17But woe to them that are with child, and to them that give suck in those days! 18And pray ye that your flight be not in the winter. 19For in those days shall be affliction, such as was not from the beginning of the creation which God created unto this time, neither shall be. 20And except that the Lord had shortened those days, no flesh should be saved: but for the elect’s sake, whom he hath chosen, he hath shortened the days. 21And then if any man shall say to you, Lo, here is Christ; or, lo, he is there; believe him not: 22For false Christs and false prophets shall rise, and shall shew signs and wonders, to seduce, if it were possible, even the elect. 23But take ye heed: behold, I have foretold you all things.

24¶ But in those days, after that tribulation, the sun shall be darkened, and the moon shall not give her light, 25And the stars of heaven shall fall, and the powers that are in heaven shall be shaken. 26And then shall they see the Son of man coming in the clouds with great power and glory. 27And then shall he send his angels, and shall gather together his elect from the four winds, from the uttermost part of the earth to the uttermost part of heaven. 28Now learn a parable of the fig tree; When her branch is yet tender, and putteth forth leaves, ye know that summer is near: 29So ye in like manner, when ye shall see these things come to pass, know that it is nigh, even at the doors. 30Verily I say unto you, that this generation shall not pass, till all these things be done. 31Heaven and earth shall pass away: but my words shall not pass away.

32¶ But of that day and that hour knoweth no man, no, not the angels which are in heaven, neither the Son, but the Father. 33Take ye heed, watch and pray: for ye know not when the time is. 34For the Son of man is as a man taking a far journey, who left his house, and gave authority to his servants, and to every man his work, and commanded the porter to watch. 35Watch ye therefore: for ye know not when the master of the house cometh, at even, or at midnight, or at the cockcrowing, or in the morning: 36Lest coming suddenly he find you sleeping. 37And what I say unto you I say unto all, Watch.